Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal
Mchezaji, Olivier Giroud ameonekana kuwa katika mazungumzo mazito na kocha wake Arsenal Wenger wakati wa mazoezi ya mwisho kabla ya kujiunga na Chelsea kwa dau la paundi milioni 35.

View attachment 687043
Mchezaji huyo rai wa Ufaransa akionekana vema kama sehemu ya kikosi kitakacho ingia uwanjani hapo kesho siku ya Jumanne kuvaana na Swansea City mchezo wa ligi kuu ya England.

View attachment 687045
Giroud atalazimika kuondoka Emirates endapo Arsenal itakamilisha usajili utakao weka rekodi ndani ya klabu hiyo wa kumnasa mchezaji wa Borussia Dortmund straika, Pierre-Emerick Aubameyang.

View attachment 687046
Wakati wa mazoezi hayo Giroud ameonekana kuwa mwenye furaha na amani akiwa na kocha wake Wenger huku wakifanyiana maskhara ya hapa na pale.

Arsenal wanafurahia ujio wa Aubameyang kutoka Dortmund ambapo watagharimika kutoa paundi milioni 55.4 huku wakitarajia kunyakuwa paundi milioni 35 juu ya uhamisho wa Giroud kwenda Chelsea.


Arsenal wameshusha dau na sasa Olivier Giroud anasajiliwa na Chelsea kwa pauni milioni 15 tu.
 
Aubameyang-tactics_1_trans_NvBQzQNjv4Bq2oUEflmHZZHjcYuvN_Gr-bVmXC2g6irFbtWDjolSHWg.jpg


Karibu Arsenal Aubameyang.

Wakuu mpooo?

Dah nilipotea sana na tumemshwishi Arsene Wenger abadili msimamo wake kuhusu ubahili na amekubali kwa shingo upande.

Ameambiwa Arsenal ni moja ya timu kubwa duniani kwa uwezo wa fedha na ni lazima mwakani icheze Champions league.

Kwa kweli huyu mzee alitukakisha sana tamaa.

Lakini kwa kasi ya matumizi ya Manchester City ambayo imevuka pauni milioni 450 mpaka sasa ambapo wamemsajili Laporte kutoka Athletico Madrid, Wenger amekubali ukweli na ameanza kutumia pesa.

Ni ukweli usojificha kwamba mchezaji mahiri awe beki, kiungo au mshambuliaji sasa hivi unatakiwa utumie kuanzia wastani wa pauni milioni 47 kwenda juu.

Aubamenyang angalau atatusaidia kwa kipindi kilichobakia lakini Arsenal ya 2018/ 19 itakuwa ni Arsenal mpya.

Aubameyang ana miaka 28 miaka mitatu chini ya Olivier Giroud hivyo yupo kwenye peak na atatusaidia sana ukiondoa kupata majeruhi ya Premier League.

Richard amerudi na wapenzi wa Arsenal tusubiri mechi na Swansea ambao wiki mbili zilizopita waliifunga Liverpool goli 1-0.

Swansea si timu ya kuidharau hata kidogo na wapo kwenye relegation zone.
 
Akitua Abu na mfumo wetu hakika hata timu iwe nzuri vipi lazima wakae tu.Unaanzaje kumzuia lacazate na abu atakuachaje huku ozil yupo ,mhtaryian anakuangalia tu asikudhuru.Angalia nyuma kati hapa kuna viungo wenye akili kama xchaka beki mnapohangaika kuwazuia foward yeye keshamuona golikipa anamuagizia mashine toka kati ya uwanja inagonga post ya juu inarudi uwanjani ozil anamalizia .Duuuuh karibuni emirates kwa burudani safi.
 
Aubameyang-tactics_1_trans_NvBQzQNjv4Bq2oUEflmHZZHjcYuvN_Gr-bVmXC2g6irFbtWDjolSHWg.jpg


Karibu Arsenal Aubameyang.

Wakuu mpooo?

Dah nilipotea sana na tumemshwishi Arsene Wenger abadili msimamo wake kuhusu ubahili na amekubali kwa shingo upande.

Ameambiwa Arsenal ni moja ya timu kubwa duniani kwa uwezo wa fedha na ni lazima mwakani icheze Champions league.

Kwa kweli huyu mzee alitukakisha sana tamaa.

Lakini kwa kasi ya matumizi ya Manchester City ambayo imevuka pauni milioni 450 mpaka sasa ambapo wamemsajili Laporte kutoka Athletico Madrid, Wenger amekubali ukweli na ameanza kutumia pesa.

Ni ukweli usojificha kwamba mchezaji mahiri awe beki, kiungo au mshambuliaji sasa hivi unatakiwa utumie kuanzia wastani wa pauni milioni 47 kwenda juu.

Aubamenyang angalau atatusaidia kwa kipindi kilichobakia lakini Arsenal ya 2018/ 19 itakuwa ni Arsenal mpya.

Aubameyang ana miaka 28 miaka mitatu chini ya Olivier Giroud hivyo yupo kwenye peak na atatusaidia sana ukiondoa kupata majeruhi ya Premier League.

Richard amerudi na wapenzi wa Arsenal tusubiri mechi na Swansea ambao wiki mbili zilizopita waliifunga Liverpool goli 1-0.

Swansea si timu ya kuidharau hata kidogo na wapo kwenye relegation zone.
Kweli ulipotea au Aubamayeng amekuleta mkuu, aje tu huyo tulikuwa tunatia huruma sana, yaani tunashinda kwa bahati tu
 
Akitua Abu na mfumo wetu hakika hata timu iwe nzuri vipi lazima wakae tu.Unaanzaje kumzuia lacazate na abu atakuachaje huku ozil yupo ,mhtaryian anakuangalia tu asikudhuru.Angalia nyuma kati hapa kuna viungo wenye akili kama xchaka beki mnapohangaika kuwazuia foward yeye keshamuona golikipa anamuagizia mashine toka kati ya uwanja inagonga post ya juu inarudi uwanjani ozil anamalizia .Duuuuh karibuni emirates kwa burudani safi.
Dah ulivyoandika kwa kujidai hadi raha
 
Kweli ulipotea au Aubamayeng amekuleta mkuu, aje tu huyo tulikuwa tunatia huruma sana, yaani tunashinda kwa bahati tu

Nimerudi baada ya Arsene Wenger kusikiliza.

Kwakweli Auba na Mkhitaryan watarudisha afya ya Arsenal.
 
Chama la wana hili hapa leo mzigoni
 

Attachments

  • Screenshot_20180130-080009.png
    Screenshot_20180130-080009.png
    31.3 KB · Views: 62
Hii swap ya luiz na giroud sijaielewa jamani maana kuna habari chelsea wanataka kufanya luiz kuwa part ya deal ya kumchukua OG
 
Akitua Abu na mfumo wetu hakika hata timu iwe nzuri vipi lazima wakae tu.Unaanzaje kumzuia lacazate na abu atakuachaje huku ozil yupo ,mhtaryian anakuangalia tu asikudhuru.Angalia nyuma kati hapa kuna viungo wenye akili kama xchaka beki mnapohangaika kuwazuia foward yeye keshamuona golikipa anamuagizia mashine toka kati ya uwanja inagonga post ya juu inarudi uwanjani ozil anamalizia .Duuuuh karibuni emirates kwa burudani safi.
we jamaa una kipaji vha utangazaji, Tido matatizo yake yakiisha akuchukue tu!
 
Kufanikiwa kwa Arsenal kumnunua mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang kwa £60m kutategemea makubaliano kuhusu wachezaji wengine wawili.
Na mshambuliaji wa Gunners Olivier Giroud ndiye huenda akawa na usemi zaidi kuhusu iwapo mkataba wa kuhama kwa Aubameyang utakamilishwa kabla ya muda wa mwisho wa kuhama wachezaji kipindi hiki, Jumatano saa 23:00 GMT.
Arsenal wamekubali kulipia gharama na mikataba ya kibinafsi ya mchezaji huyo kutoka Gabon mwenye umri wa miaka 28.
Lakini Dortmund itaidhinisha hatua hiyo kama watapata mchezaji wa kuchukua nafasi yake.

Mchezaji soka wa kimataifa wa Ufaransa Giroud, mwenye umri wa miaka 31, aliorodheshwa kuwa ndiye mchezaji atakayechukua nafasi hiyo, lakini binafsi angependelea kubaki London.
Hatua ya Chelsea kuanza kumtafuta ilimpatia nafasi hiyo ya kusalia London muda unaomfaa - na hivyo basi Dortmund wameelekeza matumaini yao kwa mshambuliaji wa Chelsea Mbelgiji Michy Batshuayi, ambaye anaweza kuwa tayari kuhama.
Batshuayi akahamia Dortmund basi Chelsea wanaweza kufanikiwa kumchukua Giroud.

Batshuayi, mwenye umri wa miaka 24, amekuwa akichezeshwa sana kama mchezaji wa kuongeza nguvu mpya katika kikosi cha Chelsea na anataka kucheza zaidi kikosi cha kwanza katika mwaka wa Kombe la Dunia.
Hata hivyo, the Blues wanasita kukubali bei ya Arsenal ya kumnunua Giroud ambayo iliripotiwa kuwa ni kati ya £30m-£35m.

Matokeo yake Chelsea ilifanya mazungumzo na Tottenham Hotspur ikitaka imchukue Batshuayi na kuipatia Chelsea mmshambuliaji wake Fernando Llorente raia wa Uhispania mwenye umri wa miaka 32.
Spurs wako makini kuingia mkataba wa kudumu, ingawa Chelsea inapendelea uhamisho wa mkopo
Bado hilo limetatizwa na haja ya Batshuayi kuwa katika timu ya kwanza ya soka.

Hii ni kwa sababu ana nafasi ndogo sana yake yeye kumuondoa mshambuliaji mkuu wa Spurs Harry Kane - ambaye ndiye mchezaji mwenye magoli mengi.
Batshuayi hataki kuwa mshambuliaji wa akiba katika klabu nyingine.
Kama Arsenal haitaweza kufikia mkataba na Chelsea kumhusu Giroud, hatua ya Aubameyang itategemea kama Dortmund watapata mchezaji mwingine mbadala kwingine.

Kama hapatapatikana mtu wa kuchukua nafasi yake, atabakia Dortmund - kama klabu hiyo ya Ujerumani ilivyoelezea.
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger anampenda Giroud, lakini Mfaransa huyo amekwishaambiwa kuwa hatapata muda wa mchezo katika uwanja wa Emirates na anajua anahitaji kuwa anacheza ikiwa anataka kushiriki katika Kombe la Dunia.
Arsenal wanamtafuta Aubameyang kuchukua nafasi ya mshambuliaji wa Chile Alexis Sanchez ambaye alijiunga na Manchester United mapema mwezi huu, kwa kubadilishana na kiungo wa kati Henrikh Mkhitaryan.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Aubemiyang yupo london tangu jana ucku na anaweza tangazwa either leo au kesho na mpaka sasa taarifa zilizopo ni kwamba Arsenal wameachana na Evans kwasababu WB wanataka hela nyingi na arsenal wamesema hawapo tayar kulipa hyo hela mpaka saaivi Arsenal wanaongea na As Roma kumsajili Kostas Manolas na pia beki mwingne ambaye ni option ya 2 ni Abou Diallo wa Mainz
 
Duh so far nimepitia kila taarifa nimekatiza vichochoro vyote vya habari imefika time watuambie ukweli ANAKUJA au HAJI maana tunaambiwa kapanda ndege kwenda London mara kaonekana uwanja wa mazoezi(Arsenal)
ad11c580d4253e105467eda8ab1eaf7b.jpg

C'mooooon you Gunners malizeni hii kadhia maana bia ya baridi imekua ya moto sasa.
 
Duh so far nimepitia kila taarifa nimekatiza vichochoro vyote vya habari imefika time watuambie ukweli ANAKUJA au HAJI maana tunaambiwa kapanda ndege kwenda London mara kaonekana uwanja wa mazoezi(Arsenal)
ad11c580d4253e105467eda8ab1eaf7b.jpg

C'mooooon you Gunners malizeni hii kadhia maana bia ya baridi imekua ya moto sasa.
fd4e929b461f9eadf3dcf891c69e8b68.jpg
 
Back
Top Bottom