Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Mnisamehe kwa kufukua kaburi hili
Ule ni mgomo wa wachezaji kumuondoa kocha .Hiyo hutokea kila timu.Ilitokea leicester kocha akaondoka,ilitokea man moyes akaondoka,ilitokea chelsea na hata sasa huenda conte akaondoka.
Tofauti ya arsenal na timu nyingine ni kuwa wamechelewa kufanya maamzi wakitegemea kocha ataresign.Kikosi bado ni safi but wenye timu watoa pesa wakiamua hukaa na wachezaji wachache ambao wewe kocha huwezi acha kuwapanga.
Hiyo ndo hali iliyopo sasa kwa arsenal na wenger.Hii si hali ngeni ktk mpira ni ya kawaida.Bado ninaamini arsenal ni timu bora ktk mpira regardless the uncertainity that are present now.
Ili mbegu iote lazima iozeshwe kwanza.Huo ndiyo ukweli.
 
Kama vilabu huamua kuvunja mikataba ya makocha wao ili kunusulu credibility ya club zao,sijui kwanini hili halitokei Emirates licha ya machungu haya yanayotukuta mashabiki zao kipindi hiki.Kocha anaumri wa zaidi ya miaka 65 na ameshaonesha kushindwa lakini wamiliki wa timu hata hawana habari ya kumbadilisha ndio kwanza kocha anaitisha press na kusema hana mpango wa kuondoka mpaka amalize mkataba wake,yaani hata aibu hana kuwa anatuudhi mashabiki wake.U mri alionao Mzee Wenger angekuwa ni mtumishi wa Serikali angeshastaafu miaka 6 iliyopita sisi Arsenal bado tunaye tu utadhani makocha wameisha
Unachoongea ni sawa but yet hawezi kupata matokeo mazuri kwani kuna under ground mgomo na huo ndo unamuondoa.
Wale wamiliki wa timu kwa sasa wako fire na yeye na hali hiyo haiwezi kumuacha salama.
Mbona timu zote zimepitia hali hiyo isipokuwa kwa nyakati tofauti.Hiyo ni ajira tayari but sijui nani atafaa.
 
Tetesi

Everton wanataka Arsene Wenger kuwa meneja wao ikiwa atafutwa na Arsenal. Mmliki wa klabu ya Everton Farhad Moshiri anaamini kuwa Wenger ni bora zaidi kuisaidia Everton kujijenga. (Star)

Arsenal wanataka mrithi wa Wenger kuwa kocha mkuu badala ya meneja, hatua ambayo itampa fursa zaidi ya kufunza.(Sun)

Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thierry Henry, anasema atakubanli ikiwa ataombwa kuchukua mahala pake Arsen Wenger. (Evening Standard)
 
Kwa wachezaji walichokifanya ni hatua nzuri japo walichelewa sana, mnagoma hadi kocha anasepa
 
3860c7de25d73c8b08c18aae2ba6a2d1.jpg


Dogo kaona isiwe shida ameamua kuhama.. wewe kubwa zima unang’ang’ania nini, Arsenal sio baba wala mama yenu..
 
Kama vilabu huamua kuvunja mikataba ya makocha wao ili kunusulu credibility ya club zao,sijui kwanini hili halitokei Emirates licha ya machungu haya yanayotukuta mashabiki zao kipindi hiki.Kocha anaumri wa zaidi ya miaka 65 na ameshaonesha kushindwa lakini wamiliki wa timu hata hawana habari ya kumbadilisha ndio kwanza kocha anaitisha press na kusema hana mpango wa kuondoka mpaka amalize mkataba wake,yaani hata aibu hana kuwa anatuudhi mashabiki wake.U mri alionao Mzee Wenger angekuwa ni mtumishi wa Serikali angeshastaafu miaka 6 iliyopita sisi Arsenal bado tunaye tu utadhani makocha wameisha
Tatizo lenu mkishinda vimechi viwili vitatu au mkumfunga man city mnasahau kabisa kama wenga hafai tena mnamsifia
 
Siri imefichuka kuwa hali ndani ya klabu ya Arsenal sio shwari baada ya baadhi ya wachezaji nyota kunyoosheana kidole.

Kiungo anayelipwa mshahara mnono kuliko wote Mesut Ozil, Henrikh Mkhitaryan na Shkodran Mustafi wameongoza vita ya maneno ndani ya vyumba vya kuvalia nguo kwa kila mmoja kumlaumu mwenzake.

Mustafi aliwekwa kiti moto na wachezaji wenzake akidaiwa amekuwa na tabia ya kuwalaumu uwanjani wakati wa mchezo na ndani ya vyumba vya kuvalia nguo.

Pia, Hector Bellerin amefura baada ya jina lake kuondolewa katika orodha ya wachezaji waliotakiwa kuanza katika mchezo huo saa mbili kabla ya mpira kuanza. Bellerin alimtolea meneno makali kocha wake Arsene Wenger.

Baadhi ya wachezaji nguli wa zamani wa timu hiyo Ian Wright, David Seaman na Sol Campbell wameshtushwa na mwenendo mbaya wa Arsenal msimu huu.

Wenger amekuwa akishutumiwa kila kona akidaiwa ndiye chanzo cha timu hiyo kuboronga, lakini amewajibu akidai hatang’oka kwa kuwa anaheshimu mkataba wake.
 
Back
Top Bottom