Wenger out conte in
" Arsenal wamchukue Conte "
Arsenal wafanye maamuzi haraka sana na kumnasa Antonio Conte kama mbadala wa Arsene Wenger kama Muitaliano huyo akiondoka Chelsea, kwa mujibu wa mchezaji wa zamani wa Arsenal, Paul Merson.
Licha ya kutwaa taji la ligi kuu ya soka ya Uingereza msimu uliopita, Conte yupo kwenye presha kubwa sana ndani ya Chelsea baada ya mfululizo wa matokeo mabovu - hivi karibuni ikiwa kichapo cha 4-1 dhidi ya Watford.
Wenger alisaini mkataba wa miaka miwili majira ya kiangazi yaliyopita, lakini Merson anafikiri kwamba mambo yanayoendelea nyuma ya pazia yanaonyesha kwamba utawala wa Wenger unafikia kikomo mwishoni mwa msimu huu.
" Siku ambayo Conte ataondoka Chelsea , kama ningekuwa pale Arsenal , haraka sana ningekuwa kwenye simu ."
" Kocha kama Conte huwa hawapatikani kirahisi"
" Arsenal wanahitaji mtu ambaye ataenda pale na kuwaudhi watu . Conte anaudhi watu kwa chanya lakini. Anataka wewe ucheze kwa utaratibu fulani na atakufanya uwe mgumu katika safu ya ulinzi. Pindi Arsenal watakapokuwa wagumu kwenye safu ya Ulinzi, watakuwa hatari sana."
" Nafikiri Arsenal wangesema," Tutakuwa na wewe msimu ujao " Nafikiri watakuwa machizi kama watamkataa."
" Nafikiri Conte atanatiki visanduku vyote. Arsenal hawawezi kuendelea kukosa makocha wote kama hawa. Huwezi kuniambia eti Guardiola asingependa kufundisha Arsenal. Kama angekuwa na fursa kwa maoni yangu angeenda Arsenal."
"Jurgen Klopp, Jose Mourinho wote wameenda kwa wapinzani wa Arsenal kwasababu Wenger alikuwa pale amekalia kiti cha Meneja badala ya kusema muda sahihi umefika wa mimi kuachia ngazi."
" Na pia kuna makocha wa daraja la juu kama Massimiliano Allegri ndani ya Juventus , lakini anaweza kuja na inaweza kumchukua mwaka mmoja kuzoea ligi ya Uingereza - kama ilivyokuwa kwa Klopp."
Merson anafikiria kwamba Wenger huenda akaondoka mwishoni mwa msimu hasa kwa kuangalia usajili wa Pierre-Emerick Aubameyang kama Mfano wa Wenger kupoteza umiliki wake na nguvu ndani ya klabu.
" Kwangu mimi huu usajili hauonekani kama wa Arsene Wenger."
" Ni lini aliwahi kununua mchezaji mwenye umri wa miaka 29 kwa Pauni Milioni 60 ?
" Sir Alex Ferguson alifanya hivyo miaka kadhaa iliyopita, alisema kwamba anataka kutwaa taji la EPL na akaenda kumnunua Robin van Persie kumfungia magoli na kumaliza Juu ya Manchester City."
"Alimsajili kutwaa taji, halafu akapanga kustaafu. Usajili wa Aubameyang kwangu mimi unasema," Huu ni usajili wa kunipa nafasi nne za juu halafu tutaonana baadae."