Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 348,109
- 1,249,102
Ligi kuu ya England imeendelea hii leo kwa michezo kadhaa kupigwa kwenye viwanja mbalimbali huko Emirates klabu ya Arsenal imeweza kuchomoza na ushindi mnono wa mabao 4 – 1 bila mshambuliaji wake raia wa Chile Alexis Sanchez ambaye yupo mbioni kujiunga na Manchester United.
Wachezaji waliyokuwa mwiba katika mechi hiyo ni Monreal akiiyandikia The Gunners bao la mapema kabisa dakika ya 6 kabla ya Iwobi kutupia dakika ya 10, Koscielny na Lacazette kila mmoja akishindilia msumari wa moto kwa Crystal Palace na kuifanya timu hiyo kupoteana kabisa uwanjani.
Kwa matokeo hayo Arsenal anakuwa na pointi 42 ikishika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi ya England huku wakiwa wamecheza michezo 24.
Wachezaji waliyokuwa mwiba katika mechi hiyo ni Monreal akiiyandikia The Gunners bao la mapema kabisa dakika ya 6 kabla ya Iwobi kutupia dakika ya 10, Koscielny na Lacazette kila mmoja akishindilia msumari wa moto kwa Crystal Palace na kuifanya timu hiyo kupoteana kabisa uwanjani.
Kwa matokeo hayo Arsenal anakuwa na pointi 42 ikishika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi ya England huku wakiwa wamecheza michezo 24.
