Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee watu wameanza kuweweseka na kubadili mikakati badala ya mashambulizi ya nguvu sana wameshatonywa kwamba wasisahau kudefend pia maana safu ya mashambulizi ya Arsenal haitabiriki inaweza kukutundika goli za haraka haraka na kubadili kabisa mchezo....MO NO na kikosi chake wanaweweseka!!!!

Oopppsss...nani anayeweweseka hapa...
 

Attachments

  • ad696e64399fab1f5637d1b83db107e2.jpg
    ad696e64399fab1f5637d1b83db107e2.jpg
    58.7 KB · Views: 94
  • Thanks
Reactions: BAK
Wakuu wenzangu wa Gunners mpoo!

Kesho tunaingia Old Traford tukiwa na lengo moja tu kupata 3 points na kutimiza malengo ya kucheza vizuri kwenye mwezi huu wa November.

November kwa kawaida si mwezi wa kheri kwa Arsenal ukiangalia rekodi ya huko nyuma lakini mwezi huu tumefanya vema tena kwa asilimia karibu 60.

Tukicheza na Man Utd,tunakumbana na Southampton, halafu Marseille na tutamaliza mechi za mwezi kwa kucheza na Cardiff City ya Wales.

Kesho tunaingia Old Traford tukiwa na rekodi nzuri ya ushindi dhidi ya Liverpool na Borussia Dortmund ya Germany.

Timu yetu itaingia uwanjani ikiwa na imani na kujiamini kwamba itapata ushindi kwa kumiliki mpira na kuuchezea watakavyo na kufunga magoli pindi wapatapo nafasi.

Arsenal kesho tunaingia Old Traford tukiwa hatuna shinikizo lolote kwani tunawazidi Man Utd kwa 8 points na ni wao wenye shinikizo la kuhakikisha hawamalizi mchezo wakiwa nyuma yetu kwa 11 points.

Kuhusu timu inayotarajiwa kuingia dimbani kwenye "theatre of dreams" ni ile ile ya kikosi cha kwanza iliyoifunga Liverpool na Borussia Dortmund, ingawa kama Flamini ataanza itabidi Thomas Rosicky apishe na aanze kwenye bench.

Hivyo basi timu inayotarajiwa ni ileile "killer machine" inayoundwa na wachezaji wafuatao:

Szczesny; Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs; Arteta, Flamini; Ozil, Ramsey, Cazorla; Giroud.

Tukutane tena hapa kesho jioni kwenye mida ya saa 12 za jioni kwa saa za Afrika Mashariki au saa 10 za jioni kwa saa za Ulaya hasa Uingereza.
 
Naona dalili za ushindi. MU wanaonekana kuwa highly intimidated na performance ya Arsenal. Hii inaweza kuwa zana nzuri ya kivita ya kumshinda Moyes. Arsenal ana nafasi kubwa ya kushinda leo hasa ukizingatia record yake ya siku za karibuni ya kushinda mechi nyingi zikiwemo za ugenini. Wakishinda leo itaongeza morali wao wa kutwaa EPL title mwaka huu na kumaliza vema mwaka. Kila la heri Arsenal.
 
.... siwaamini sana na wasiwasi na nyie kwanza j2 old trafford .

Msimu huu ni wakuvunja miiko....leo jumapili tunavunja mwiko wa Rooney kutuvurugia rekodi zetu...si unakumbuka alivyotuvurugia rekodi ya kutofungwa tukiwa tumiefikia mech 49..! Sasa hatutaki leo atuvurugie rekodi ya kutofungwa ugenini....na pale Trafford tuchukua point tatu kiulaiiniii...! Usikose mkuu.
 
Yaaani leo arsenal vigelegele kama mnamtoa mwali...mweeee
 
3 Free Points For the Gunners. Manyoo Lazma tumle Witi Leo. Arsenal 4-0 Manure.
 
Full Kikosi, No Mercy #Arsenal team: Szczesny, Sagna,
Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta,
Flamini, Ramsey, Cazorla, Ozil, Giroud
 
Full Kikosi, No Mercy #Arsenal team: Szczesny, Sagna,
Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta,
Flamini, Ramsey, Cazorla, Ozil, Giroud
 
Wakuu naona timu zipo uwanjani zinafanya mazoezi madogomadogo.

Timu ni nzuri na Thomas Rosicky amempisha Mathew Flamini pale katikati ili kuongeza uimara wa safu ya ulinzi kwenye sehemu ya kiungo.
 
half-scarf_2729599a.jpg


Mmoja wa wachuuzi wa vifaa na vikorombwezo vya mavazi wa timu hizi mbili akiwakaribisha mashuhuda kwenye "Theatre of Dreams" ya Old Traford.
 
Back
Top Bottom