Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

he is speculated to join Arsenal although there is a spanish young DM currently playing at 3rd placed La liga team Real Sociedad called Irralamendi he is 21 year-old but very dirty in midfield, he is also linked if Fellain's deal will hit the rock as we all know the rumuors of Golalons of Lyon have cooled down...let's wait and see

I can't wait...wouh.........!!!!!!
 
Wakuu mambo vipi naona kila kona kuna browsing maana Arsenal wamefunga midomo kwa sasa.

Mpaka sasa ni wachezaji watatu ambao kama ikithibitishwa kuanzia jumatatu, basi watachezea Arsenal msimu ujao.

Wachezaji hao ni Higuain, Fellaini na Julio Cesar ukiondoa Yaya Sanogo ambae inajulikana pia atathibitishwa wiki ijayo.

Ikiwa itakuwa hivyo basi naweza the most likely line-up ya msimu ujao kwenye ligi na kwenye CL;

Szczesny au Cheza


Merts Kos


Jenkinson Gibbs


Fellaini


Jack

Theo Santi

Rooney


Higuain au Higgy

Wachezaji wa akiba :Cesar, Verms, Sagna, Monreal, The Ox, Arteta, Pods, Giroud.

Wayne Rooney nimemuweka tu kama ikilazimu maana pesa ipo.

Wakuu, this will be a proper Arsenal team.

Rooney no no nooo....!!
 
Pre season imeanza, Sanogo in. I hope a stellar signing is on the way before we go on tour :becky:
 
Huna anyeuzika kati ya waliobaki.

Andrey Arshavin - Zenit St Petersburg (Russia)

Vito Manone- Sunderland (English Premier League)

Johan Djourou- Hamburga SV (Germany) Bundesliga

Carlos Vela - Real Sociedad (Spain)

Francis Coquelin- SC Freiburg (Germany) Bundesliga

Nicklas Bendtner - kwenda Eintracht Frankfurt ya Germany (Bundesliga ) kama akikubali pay cut.
 
Wakuu, baada ya pilikapilika za hapa na pale na mazungumzo ya muda mrefu mchezaji Gonzalo Higuain ameweka saini kwenye mkataba na Arsenal FC na atakuwa akilipwa paundi 130,000 kwa wili pamoja na "adds on" kama matumizi ya jina na mengine kufikia paundio 150,000 kwa wiki.

gonzalo-higuain-767745.jpg

Higuain anavunja rekodi ya usajili uliofanywa kwa Andrey Arshavin mwaka 2008 ambao uligharimu kiasi cha paundi milioni 15.

Arsenal inaweza kutangaza mchezaji huyo siku ya Ijumaa au Jumatatu na anakuwa ni mchezaji wa pili kusajiliwa msimu huu baada ya Yaya Sanogo ambae anatoka Auxerre ya France.

Muda wa usajili ukiwa ndio unapamba moto bado inasemwa kwama Arsene Wenger anafikiria kumsajili Wayne Rooney wa Man Utd au Luis Nani pia wa Man Utd na pia Marouane Fellaini bado anazungumzwa.

Arsenal ina kiasi cha paundi 100 milioni za kutumia kwenye usajili wa sasa na January 2014 kama ikibidi na hiyo ni majumuisho ya milioni 70 zilizoko benki na milioni 30 ambazo zimetokana na kuondoa wachezaji wasiotakiwa kama Arshavin na Squillaci.

Maskauti wa Arsenal wamekuwa na muda mgumu katika soko la wachezaji huku kukiwa na taarifa kwamba mfumo wa kutambua vipaji unaofanywa kwenye mtandao maalum wa OPTA INDEx kuingiliwa na "hackers" ambao wamekuwa wakivumisha habari za usajili ziizo za kweli.

This is it na huu ndio usajili wa maana tuliotaka na inaonyesha jinsi miaka 8 ya bila kikombe ilivyokuwa ikiandaliwa.

Anaefuata ni Cesc Fabregas au Marouane Fellaini.

COYG.

Update- Huguain yupo London kwa medical.

Mchezaji Gonzalo Higuain yupo jijini London kufanyiwa uchunguzi wa afya yake na baadae kumalizia taratibu za usajili wake kuchezea timu ya Arsenal.

Hizi ni habari ambazo zimekuwa zikisubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa timu yetu hii na inasemwa kwamba kulikuwa na matatizo kwenye makubaliano ya ada ya usajili na mawakala ambao ni baba yake na kaka yake.

ay_113072594.jpg

Mshambuliaji Gonzalo Higuain.

Kama mambo yakienda sawia na usajili wa Julio Cesar wa QPR basi tutakuwa angalau tumefikia asilimia 90 ya usajili muhimu kwa timu yetu na huenda wachezai hawa wawili wakatangazwa siku ya Ijumaa.

COYG.
 
Update:

Mchezaji wa nafasi ya ushambuliaji Yaya Sanogo kutoka timu ya Auxerre nchini Ufaransa leo hii amekamilisha taratibu za kujiunga na Arsenal na amefanyiwa uchunguzi wa afya yake kwenye kituo cha mazoezi cha London Colney kaskazini mwa London.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 anatarajiwa kutangazwa mwishoni mwa mwezi Juni atakapomaliza mkataba wake rasmi na Auxerre.

Mchezaji huyo anachezea timu ya taifa ya Ufaransa ya vijana wa umri chini ya miaka 21 na ni mchezaji wa tatu kutoka kwenye timu hiyo ya Auxerre ambayo inashiriki ligi ya pili ya nchi hiyo. Abu Diaby na Bacary Sagna pia walitokea kwenye timu hiyo walipojiunga na Arsenal ni uwezo wake wa kumiliki mpira, mwendo na uwezo wa kiufundi ndivyo vilivyowavutia Arsenal.

Auxerre%27s%20French%20forward%20Yaya%20Sanogo%20celebrates%20after%20scoring%20a%20goal%20during%20the%20French%20L1%20football%20match%20Auxerre%20vs%20Toulouse-1749553.jpg

Yaya Sanogo

Huu utakuwa ni usajili wa kwanza kwa msimu wa 2013/14 kwa kutumia pesa kidogo iliyotokana na mauzo ya Cesc Fabregas na Alex Song na bado jumla ya kitita halisi cha zaidi ya paundi milioni 100 zinazotarajiwa kutumiwa kusajili wachezaji zaidi hakijatolewa kwa meneja Arsene Wenger.

Karibu Arsenal Yaya Sanogo.

COYG!

CC: Ulimakafu, Kuntakinte.
 
Salama mkuu?

Na hii ya Luis Suarez kutakiwa na Arsenal imekaaje?

Hii inawezekana tatizo Suarez tayari ana matatizo ya nidhamu.

Lakini lolote linaweza kutokea ingawa leo kwenye mazoezi ambayo vijana wameanza, Marouane Shamakh ameonekana hivyo amerudi na inaonyesha Wenger bado ana mipango nae.

Tumebakiza wachezaji wawili lakini wa muhimu ni Higuain na Fellaini na kama sio Fellaini basi Lars Bender.

Washambuliaji tutakuwa nao ukijumlisha huyu Higuain na Sanogo nafikiri ameajiliwa kusaidia kampeni za Carling Cup na FA Cup sio sana kwenye ligi kuu.
 
Wakuu wa Gunners mambo niaje? Vijana walikuwa Colney leo kujiandaa na safari ya kwenda Vietnam pamoja na nchi kadhaa kule Far-East. Vijana watakaotua Emirates tayari wanajulikana na baadhi watakuwepo kwenye msafara wiki ijayo. Prof kamaliza likizo yake na sasa yupo ready kunoa ushambuliaji na defence.

Wanoko wameshaanza kuweweseka nasikia walijaa tele humu kama pishi la udaga wakati chichi wengine tulikuwa bado tuna-enjoy summer. Wimbles mwaka huu imekuwa mbovu sana kutokana na all England club kupanga ratiba mbovu, tunachubiri kuona kama wiki mbili zijazo Tiger ataweza kuchukua British open kule Scotland.




article-0-1AA8949E000005DC-893_634x549.jpg



Theo akinyanyua vyuma ... ... ..




article-0-1AA902B8000005DC-603_634x473.jpg




Frimpong akiwa na Jack .... ...




article-2355998-1AA89C14000005DC-57_634x378.jpg




article-0-1AA89BC4000005DC-447_634x397.jpg




article-0-1AA89C8B000005DC-513_634x453.jpg



Fitness coach Tony akifanya vitu vyake ... ...


article-0-1AA895F3000005DC-446_306x423.jpg


Ryo na Fabianski


article-0-1AA8961B000005DC-794_306x423.jpg


The Ox ...... ..


article-0-1AA89D46000005DC-938_634x460.jpg


the Morocan was there ... ... ..
Next new signings ..... ..... .... .... ....
 
Tupo mkuu naona mzee Wenger safari hii anataka timu hasa.

Nimeweka hapo juu wachezaji ambao mpaka leo hii wataondoka akiwemo Francis Coquelin na Ryo Miyaichi ambae atakwenda Feneyoord kwa mkopo.

Coqueilin ana matatizo ya experience na Wenger anataka akacheze mechi nyingi zitakazomfanya awe ngangali uwanjani na kuleta imani kwamba anaweza kucheza vizuri kwenye midfield.

Ryo Miyaichi ana tatizo moja kubwa kwamba hapati work permit kwa sababu hajacheza sana mechi za kimataifa chini kwake, hivyo kumfanya asitimize masharti ya kucheza mechi za kimataifa kwa asilimia 75.

Lakini akienda tena Feneyoord na akacheza hadi mwakani atahesabika kama home grown player kwa sheria za FIFA na ataweza kupata work permit akiwa na umri wa miaka 21.

Ila kwa kweli mzee Wenger amefanya clearence ya hali ya juu.

ARSENAL INS AND OUTS.

INS- Yaya Sanogo

Outs- Craig Eastmond (Colchester, free), Jordan Wynter (Bristol City, free), Andrey Arshavin (Zenit, free), Sanchez Watt

(Colchester, free), Sebastien Squillaci, Denilson, Conor Henderson, Jernade Meade, James Shea, Reice Charles-Cook,

Sead Hajrovic, Philip Roberts, Nigel Neita, Samir Bihmoutine, Josh Rees (all released)


 
Hii inawezekana tatizo Suarez tayari ana matatizo ya nidhamu.

Lakini lolote linaweza kutokea ingawa leo kwenye mazoezi ambayo vijana wameanza, Marouane Shamakh ameonekana hivyo amerudi na inaonyesha Wenger bado ana mipango nae.

Tumebakiza wachezaji wawili lakini wa muhimu ni Higuain na Fellaini na kama sio Fellaini basi Lars Bender.

Washambuliaji tutakuwa nao ukijumlisha huyu Higuain na Sanogo nafikiri ameajiliwa kusaidia kampeni za Carling Cup na FA Cup sio sana kwenye ligi kuu.

23 Million for Madrid's Bench Warmer...lol crazy stuff from poor Wenger. Lambda atasaidia mmalize juu ya Tottenham
 
Tupo mkuu naona mzee Wenger safari hii anataka timu hasa.

Nimeweka hapo juu wachezaji ambao mpaka leo hii wataondoka akiwemo Francis Coquelin na Ryo Miyaichi ambae atakwenda Feneyoord kwa mkopo.

Coqueilin ana matatizo ya experience na Wenger anataka akacheze mechi nyingi zitakazomfanya awe ngangali uwanjani na kuleta imani kwamba anaweza kucheza vizuri kwenye midfield.

Ryo Miyaichi ana tatizo moja kubwa kwamba hapati work permit kwa sababu hajacheza sana mechi za kimataifa chini kwake, hivyo kumfanya asitimize masharti ya kucheza mechi za kimataifa kwa asilimia 75.

Lakini akienda tena Feneyoord na akacheza hadi mwakani atahesabika kama home grown player kwa sheria za FIFA na ataweza kupata work permit akiwa na umri wa miaka 21.

Ila kwa kweli mzee Wenger amefanya clearence ya hali ya juu.

ARSENAL INS AND OUTS.

INS- Yaya Sanogo

Outs- Craig Eastmond (Colchester, free), Jordan Wynter (Bristol City, free), Andrey Arshavin (Zenit, free), Sanchez Watt

(Colchester, free), Sebastien Squillaci, Denilson, Conor Henderson, Jernade Meade, James Shea, Reice Charles-Cook,

Sead Hajrovic, Philip Roberts, Nigel Neita, Samir Bihmoutine, Josh Rees (all released)




I hear chickens trembling here. Now Arsenal will do the Quadruple and be named the greatest team of all time. Hahahahahahahahahahahahahahahhhhhhh
 
Back
Top Bottom