Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Bayern-Fans_2903170.jpg
 
Nimekubali mtoto halali na hela........
Zaidi ni nepi ya mkojo tu.....yaani 3
Tatizo Arsenal wanajikanyaga sana.
 
Yeyote anaeongea kinyume na mawazo ya Arsenal hapa anakaribishwa lakini ndio ushabiki huo.

Sisi ndio wapenzi wa Arsenal na hatutaicha timu yetu itetereke.

Tunaamini kuwa timu ipo kwenye kipindi cha mpito na Arsene Wenger anaunda timu mpya ya kuja kuwa Invisibles kwa mara ingine.

Pesa ipo na tutatumia miezi ya June na July.
 
Yeyote anaeongea kinyume na mawazo ya Arsenal hapa anakaribishwa lakini ndio ushabiki huo.

Sisi ndio wapenzi wa Arsenal na hatutaicha timu yetu itetereke.

mpira mmecheza kweli ila mbinu za kufunga hamna na beki yenu ndio mbovu kama ya barca..
 
3-1 ndo results.... so far sina hope hata chembe.... Its time up for mr. WENGER.... he has done enough and this is it....
 
Afadhali yako wewe unayejikubali mwenzio Wacha1 huwa haonekani kabisa, hapa atakuja kesho kutwa na mambo ya bahasha

Mimi ni mpenzi hasa wa Arsenal na mtu haniambii kitu. Nipo na Arsenal tangu nikiwa mdogo na hii timu imepata meneja ambae anafahamu anafanya nini pale na hata Arsenal siku ikishuka daraja mimi ntashuka nayo.

Ni kipindi cha mpito na Arsenal inaundwa upya, tutarudi tu kusukumana na Man Utd, Chelsea na Man City.

Man Utd walienda kucheza Europa ligi na hakuna alieongea, Man City nao wametolewa mapema tena kwenye mzunguko wa kwanza hakuna aliesema na sasa hata mabingwa Chelsea wanacheza Europa ambayo ni ligi ya failures na hakuna anaesema.

Nimeamini hii timu ipo kwenye nafasi nzuri sana kujiandaa kwa msimu ujao.

Achana na vyombo vya habari vya UK na washirika wao ndio vinapika majungu vikisaidiwa na bahasha za Usmanov ambae ndie yupo nyuma ya kampeni lakini bodi ya Arsenal inafahamu hilo.
 
huu ndio mwanzo wa mwisho wa arsenal kwa msimu huu 2012-2013 ucl
 
Ni kipindi cha mpito na Arsenal inaundwa upya, tutarudi tu kusukumana na Man Utd, Chelsea na Man City.

Man Utd walienda kucheza Europa ligi na hakuna alieongea, Man City nao wametolewa mapema tena kwenye mzunguko wa kwanza hakuna aliesema na sasa hata mabingwa Chelsea wanacheza Europa ambayo ni ligi ya failures na hakuna anaesema.

Nimeamini hii timu ipo kwenye nafasi nzuri sana kujiandaa kwa msimu ujao.
Tatizo lenu kila mwaka mnakuwa kwenye kipingi cha mpito, huo mpito hauishi tuu..! Ona sasa mmepigwa LIBOLO kama simba vile
 
Tatizo lenu kila mwaka mnakuwa kwenye kipingi cha mpito, huo mpito hauishi tuu..! Ona sasa mmepigwa LIBOLO kama simba vile

Mkuu sasa nawe usiwe Muppet.

Arsenal ipo kwenye kipindi cha mpito na kipindi hiki mwisho wake ni mwaka huu.

Tayari wachezaji kadhaa wameondolewa kama Chamakh, Bendtner, Squillaci, Arshavin na wengine wengi tu akiwemo Bacary Sagna.

Mwaka huu wachezaji hao wengi wao hawatasaini tena mikataba yao na watanunuliwa wachezaji wengine kuziba nafasi zao.

Kwahio hapo unakuwa umeondokana na mzigo wa kulipa mishahara wachezaji ambao hawachezi kwa viwango vinavyotakiwa.

Ni wakati wa mpito kwasababu tumeweza kucheza kwenye level ya juu (sawa bila kunyakua vikombe) lakini hatujaweza kutumia pesa nyingi kununua wachezaji ambao wangeleta matatizo.

Hii tunafahamu ni kampeni inafanywa na yule mrusi anaetaka kuingia kwenye klabu hii na anawapa bahasha kila mtu kuongea uchochezi uliokosa heshima kwa Wenger.

Man Utd ilipokwenda kucheza Europa hakuna alieinua mdomo kuongea pumba lakini kwa sababu timu ina meneja mgeni tena mfaransa basi watu wanabwabwaja tu maneno.
 
Kuna haja ya kuwarudisha Liverpool kwenye haya mashindano
 
Back
Top Bottom