Lukataluko
JF-Expert Member
- Nov 20, 2017
- 1,345
- 1,572
Mimi niwakumbushe tuu ccm wenzangu kuwa mwisho wa ubaya niaibu.
Mkuu Herry James naye ni mjumbe wa kamati ya ulinzi na usalama?. Halafu hoja siyo ujumbe kwa mwenye akili hoja ni yaliyojadiliwa na wajumbe. Kwani watu sahihi hawawezi kujadili na kupanga upuuzi, au wajumbe sahihi wakikutana na kupanga mambo ya hovyo siyo kosa wala hakuna shida kwasababu ni wajumbe sahihi?. Wewe ni hopeless , huna uwezo wa kufikiri ,umepofushwa na njaa ya kutaka uteuzi na kwa unafiki huu utakufa mdomo wazi kama mzoga.Mmeanza drama!
Fictional short story mixed with propaganda!
Ukiisoma habari yenyewe utagundua ni habari iliyojaa uwongo ambao kama hutumii fikra pana huwezi kugundua.
Ukiangalia kwa jicho la pili utagundua kuna uwezekano CHADEMA wanataka kufanya maovu au kumteka/kumficha mgombea/wagombea wao ili waseme, mmeona tuliwaambia mapema kuwa haya yatatokea.
Baadhi ya viongozi wa CHADEMA wameanza kuwajenga kisaikologia ''makamanda'' katika mipango yao.
Wajumbe aliowataja ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ambayo ni kawaida kukaa ili kutathmini hali ya usalama katika mkoa.
Tokea mwaka 1996 mmnatuambia taifa linaelekea kubaya! huko kubaya ni wapi ambako hatufiki?
Ninajua baada ya uchaguzi mtakuja na nyimbo zilezile za kuibiwa kura.
hahahahaha kwani Da Mange kasemaje? ukiona chadema wanaanza haya mambo ya story ujue wameona dalili ya kushindwa sasa wana tafuta sababu ,,,,
Kamanda, inaelekea wewe unawajua waliomuua, na ni kwa nini ameuawa?!
Na wewe mayala amuamoja kutumia kiingereza chao au kiswahili chako,habari ya kutuchanganyia lugha humu ni upuuzi kabisa,tambua jamii yako ndiyo wahusika wa hii habari zaidi siyo wazungu.Kiukweli mimi ni kama Tomaso, siiamini taarifa hii yote hivi hivi ilivyo. Kuna maeneo nakubaliana na Ngurumo, lakini hoja hii ya Lissu,
"Wakatoa mfano wa shambulizi dhidi ya Lissu (Dodoma) na mgombea wa Muleba; kwamba walipaswa kufa, lakini waliotumwa *walifanya makosa.*", sorry jamani siiamini kabisa kuwa hiki kilijadiliwa, kwa sababu siamini hawa watu wanaweza kuwa vichaa hivi!.
Sababu ya kutoiamini kauli hii ni kwa sababu inabeba criminal liability za aina mbili
Accessories After The Fact: Lissu ameshambuliwa na watu wasiojulikana, Jeshi letu la polisi limeshindwa kufanya chochote kwa sababu limekosa pa kuanzia baada ya kukosa shuhuda yoyote wa kumuhoji, na kuna camera za CCTV zilirekodi, zimetoweka, hivyo hakuna kabisa pa kuanzia uchunguzi!.
Kumbe kuna watu wamejifungia katika ukumbi wa BOT Mwanza akiwemo RC na RPC ambao ndio walihusika na shambulio lile!.They are all, accessories after the fact, wanapaswa kukamatwa na kuhojiwa kuhusu sambulio la Lissu!.
Kwa vile RPC nae ni mhusika, hivyo hakuna mahali pa kuanzia, ila naamini kwa vile Mwigulu ni member wetu humu, atawatuma vijana wake wakawahoji wahusika waliotajwa, tena nawaomba wasimsumbue kabisa Ngurumo kumtaja source wake, kama ameitoa taarifa hii kwa kofia yake ya uandishi wa habari, kwa sababu sisi waandishi tuna kinga ya kihabari ya "the confidentiality of the source".
Kama ameitoa kama Makamo Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Ziwa, alipaswa kesho yake kuondoka Mwanza kwa ndege ya kwanza na kufikia mezani kwa Mwigulu, kisha kwenda mezani kwa Kipilimba kuripoti, halafu ndipo ailete humu!.
Criminal liability ya aina ya pili, ni accessories before the fact, ambapo watu wakubwa, wazito wa mkoa wamekutana kupanga kufanya jinai!.
Any good citizen akisikia ni wajibu wake kuripoti, kwa vile RC na RPC ni wahusika, waliosikia wakaripoti kwa Ngurumo, kwa vile Ngurumo sio Mlinzi wa Amani, tariffs hiyo ni very sensitive ilibidi Ngurumo amuongoze mtoa taarifa wake kwa mlinzi wa amani, Waziri aelezwe, IGP aelezwe, na Amiri Jeshi aelezwe, ili wahalifu hawa, watiwe mbaroni haraka kabla hawajatekeleza jinai hii!.
NB, karibu wote waliotajwa ni wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama, ambao wana mamlaka ya kumkaribisha mtu yoyote kwenye kikao chao hata kama sio mjumbe. Hivyo hii isijekuwa ni leakage ya taarifa ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mila, imeleak kwa Ngurumo, naye kaileta JF, taarifa za kamati ya ulinzi na usalama ni siri!. Hivyo this leaves much to be desired, kumbe hizi ndizo kazi za kamati zetu za ulinzi na usalama za mikoa!. Nimemkumbuka Kamanda Mawazo!' RIP Kamanda Alphonce Mawazo, damu yako haitapotea bure, sasa imeanza kuchemka na kuibua madudu yanayofanyikaga!.
Ila pia sisi raia wema wa nchi hii, tufanye responsible blogging kwa self censorship ya sensitive info, tuwe makini na waangalifu sana na hizi taarifa za wanasiasa, nyingine ni political capitalization tuu!, tusije tukalishwa matango pori na kuingizwa ...cha kike!.
P
Kuhusu madudu ya Kamati za Ulinzi na Usalama, nimeyazungumza hapa
TISS ni Watekaji, Watesaji na Wauaji!. Wasijadiliwe na Bunge bali Wachunguzwe, Wafumuliwe!
Swali la Morality: Je ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele maslahi ya Taifa?
Paskali
Huyu Ansbert anapaswa KUMPA MSAADA Kamanda MSANGI kwani hayo aliyoyaeleza hasa kuhusu LISSU yanahitaji UFAFANIZI WA KINA, " WALIPANGA KUMUUA" ???
Hata hili unalolisema linawezekana maana huenda wako ambao hawaridhishwa na mambo haya ingawa wako kimya.Wala msiwasingizie hao waliohamia, kwani mnafikiri miongoni mwetu wote tunawaza pamoja kama mazombie?
Hata miongoni mwetu kuna migawanyiko mikubwa unatafutwa muda sahihi tu. Katika siasa mkakati ni tafuta taarifa, kamata taarifa, hakiki taarifa , tunza tasrifa na ushahidi juu ya taarifa.
Then relax, subiri muda na wakati sahihi.
Pascal mayala unachanganya"Wakatoa mfano wa shambulizi dhidi ya Lissu (Dodoma) na mgombea wa Muleba; kwamba walipaswa kufa, lakini waliotumwa *walifanya makosa.*".
Hii siamini!.
P
Siyo huenda, hivyo ndivyo hali ilivyo mkuu.Hata hili unalolisema linawezekana maana huenda wako ambao hawaridhishwa na mambo haya ingawa wako kimya.