Usifanye juhudi za kijinga za kuwatoa watu kwenye mada husika...kama unaona kuna hilo hitaji unaweza tu kulianzishia mada
Asante sana kwa ushauri sina kikwazo cha kupokea ushauri hata uwe wa kipuuzi kiwango cha lamiKamanda huo nakupa ushauri wa bure. Agenda yenu kubwa bado ni ukuta na kwa mujibu wa Mwenyekiti maandamano yenu ni 01/10. Sasa Mwenyekiti naye kwa sasa anagombana na baba mwenye nyumba. Ndio maana ushauri wa huu ni muhimu sana kwenu, tunzeni nguvu ili msije pata kisingizio cha kuahirisha tena. Magufuli yuko kazini na nchi inaenda inavyotakiwa.
Wao wenyewe wanatetemeka kila dakika, wanahisi anaweza akawachenjia muda wowote, yani "kimba" linagonga "kofuli" linarudi.Hata waliompa kijiti wamebaki kushangaa
Mshana nimekuelewa vibaya sana hadi mwili umesisimka. Ubarikiwe sana kwa kueleza ukweli. Japo wapi watakaosemaNgoma ikivuma sana hupasuka na mwenye kiburi akishupaza sana shingo huvunjika mara.
Tuwe na tuo tuwe na tafakuri kwenye maneno yetu...mtu anayejisifia rohombaya wazi wazi sio kwamba hana tu hekima lakini pia hana saburi na hatafakari matokeo ya kauli zake, huyu ni mwovu.
Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri, bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu, huchochea ghadhabu huchochea visasi chuki na ubabe.Dhima ya kiongozi ni kuleta umoja na maridhiano sio kuchochea chuki na visasi
Kiongozi mwenye hekima kamwe hawezi kuongea karaha.Karaha huleta simanzi na majonzi, mtu wa karaha hana ogofyo lolote, ni kiburi na kiburi chake ni anguko.
Nuru ya mtu mbaya huzimika ghafla bila tahadhari bila taarifa. Mtu wa hekima hutengeneza patano kwa njia ya mashauriano.
Je, tunatengeneza ama tunabomoa?
Je, tunahubiri amani ama visasi?
Je, tunaeneza ustawi au anguko?
Je, Tunafundisha hekima au upuuzi?
- Hakuna kitu kibaya kama kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi
jifunze kuweka akiba ya maneno.Usipende kutuletea mawazo mgando na fikra zinazotokana na inferiority complex.
Asante sana kwa ushauri sina kikwazo cha kupokea ushauri hata uwe wa kipuuzi kiwango cha lami
Kwa mimi neno "kukurupuka" ni jipya katika medani ya kisiasa na sijui maana yake labda ukinisaidia ndo naweza kuchangia hoja yako mpya uliyoijenga kwa hayo maswali.Sasa tunaenda vizuri sana....ni nani anapata madaraka gani kwa vigezo gani na kwa sababu zipi? Na je anakuwa ameandaliwa au kakurupushwa tu na kupewa mikoba asiyoweza kuibeba?
Umeandika mengi sana lakini hata sijui umeandika nini na hata nikikwambia nifafanulie ulichoandika utaishia kutoa macho kama si vijembe
Siku mama yako akitusiwa, unachagua kufanya lipi kati ya hayo mawili?"UKIONA WATU WANAKUCHEKEA UJUE UMEKOSEA MAHALA ILA UKIONA WATU WANAKUCHUKIA UJUE UKO SAWA KABISA"
Yani kinachoumiza zaidi wakina Pengo na Mufti wanazidi "kumkenulia gego" tu, hivi tutegemee nini hapo?Kiukweli huyu mheshimiwa ni mchapakazi ila anakosa HEKIMA ya kiuongozi, anaropoka MNO. Ni mkatoliki huyu tena mhudhuriaji mzuri sana wa ibada, sasa sijui anatumia maandiko yapi huko kanisani yanayofundisha VISASI na KUTOKUSAMEHE! Suleiman hakuwa ******** kumuomba Mungu HEKIMA kabla ya kitu chochote mara tu baada ya kupata ufalme. Ni huyu huyu anayesema eti "Tumuombee" kila siku. Kama anaamini Mungu aanze basi kwanza kuyaishi yale yaliyo katika vitabu anavyoamini kabla hajaombewa.
Kiukweli tunawabebesha wengine, Mungu na atujalie hekima ya kutambua makosa yetu na kumrudia yeye. Asante kwa Neno mkuuMaisha yote ya Yesu yalikuwa kukemea maovu kwa vitendo. Luka 14:27, 28, aliwaambia makutano "27:Mtu yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, si mwanafunzi wangu; 28:Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kumalizia ".
Je, mimi na wewe misalaba yetu tunaibeba au tunawabebesha wengine!
Ungekuwa hujakielewa ungeniuliza in the first place hukufanya hivyo....!mimi sijakuelewa ndio maana nikakuomba ufafanuzi...hivi vingine ulivyoandika havikusaidii hata wewe mwenyeweFafanua ulichoandika wewe kwanza, siku zote huwezi elewa mawazo tofauti na yenu. Nyie ni loosers na hamuwezi toa credit wala dictate terms nyie subirini muambiwe, muelekezwe na muamrishwe nini cha kufanya ndio anguko lenu.
Poa poa mkuu.....tujadili kwa...mtindo huo....wa kujengana kifikra huku....ujumbe ukifika kwa ka muelewa...Sawa ila kwakuwa sijamtaja yoyote basi tuachane na ramli tubaki na mjadala na twende nao kwa nia ya kujengana kifikra...hebu angalia ninavyoenda na mwengeso tunapingana kwa hoja heshima na hekima bila kutunishiana misuli wala kuonyeshana umahiri wa mipasho
Nikishika ile "mboga" nikaiweka kwenye mzani wenye uzito wa hayo mawe, naona ni jinsi gani ilivyo nyepesi kuliko hata mnavu.Wanaowasiliana na kamati kuu ya CCM wawaambie kuwa next time wanapotafuta mtu wa kuja kuwa rais wazingatie haya:
1. Mental and psychological assessment
2. Personal background, especially childhood
3. Exposure to the world outside Tanzania
4. People skills
5. Communication skills
6. The ability to read
7. An understanding of the Constitution and the laws of the country
8. Etiquette
9. A receptive mind
10. The ability to unite all people as one nation
Kama ulivyo mchezo wa drafti tumeliwa king.