Anguko sasa ni dhahiri

Anguko sasa ni dhahiri

Hii mada haistahili kuleta hamasa za kisiasa.
Muachie mkuu Mshana aendeleze mada yake.
Na katika post zote nilizoweka kwenye uzi huu hakuna mahali nimemtetea mwanasiasa yeyote.
Kwa upande wa barabara ni aibu sana kuwa na barabara kama zile kwa nchi kama yetu hii.
Hebu fikiria maendeleo ya uzalishaji na kiuchumi kama barabara hii ingekuwa nzuri
Haya powiche khovolongwa nava policcm vanyibate enamba yango ya khemobiteli eye apa andekha.
075486984
 
kuna sababu ya kumdhibiti huyu jamaa bila hivo ataipeleka pabaya hii nchi...

kwa taarifa yako inchi inaendelea kunyooshwa ili kufikia maendeleo,porojo,kubebembelezwa peleka kibarazani.Hizo ramri utazipiga sana,mbaya zaidi huna hata uwezo wa kuzidhibiti tamaa zako mwenyewe.
haya ndiyo madhara ya kushindia chips harafu uko mwanaume,lazima akili idumae tu.
 
Kiongozi mwenye busara na hekima hawezi kumnyima mkono wa heri hata adui yake kisiasa, Nd mshana jr

Kiongozi mkweli hawezi kusita kusema na kutenda yaliyo kweli.

Mwanasiasa huishi kwa si hasa.

mshana jr wewe ndani mwako ni mangapi umeyasamehe na ni mangapi umeshindwa kuyasamehe!

Lipi husameheka? Lipi hufichwa moyoni? mshana jr, naomba TUTAFAKURI, kabla ya kunyoosha kidole cha lawama
mwengeso nipe tofauti ya kiongozi na raia! Kwanini kila mtu ni raia lakni si kila mmoja ni kiongozi?
Dhima ya kiongozi ni nini kutengeneza au kuharibu?
Kujenga ama kubomoa?
Kuponya ama kutia jeraha?
Tunapozungumzia busara na tafakuri kwa viongozi ni kwenye mambo kama na si visasi utemi na vitisho
 
Kiongozi mwenye busara na hekima hawezi kumnyima mkono wa heri hata adui yake kisiasa, Nd mshana jr

Kiongozi mkweli hawezi kusita kusema na kutenda yaliyo kweli.

Mwanasiasa huishi kwa si hasa.

mshana jr wewe ndani mwako ni mangapi umeyasamehe na ni mangapi umeshindwa kuyasamehe!

Lipi husameheka? Lipi hufichwa moyoni? mshana jr, naomba TUTAFAKURI, kabla ya kunyoosha kidole cha lawama

Ndio tungeona hapo busara, mwenzio kamwaga mboga we usimwage ugali, chukua maji karoga na chumvi halafu mkaribishe tena. Busara yako itafanya anaekupinga akukubali tu bila kutumia nguvu
 
Wanaowasiliana na kamati kuu ya CCM wawaambie kuwa next time wanapotafuta mtu wa kuja kuwa rais wazingatie haya:
1. Mental and psychological assessment
2. Personal background, especially childhood
3. Exposure to the world outside Tanzania
4. People skills
5. Communication skills
6. The ability to read
7. An understanding of the Constitution and the laws of the country
8. Etiquette
9. A receptive mind
10. The ability to unite all people as one nation

Kama ulivyo mchezo wa drafti tumeliwa king.
 
wewe na wew Mtoto akiongea ujinga na baba naye aige sio? nani mkubwa hapo nani anayepaswa kumfunza mwenzake ni baba ama ni Mtoto? nani wakukemea ubaguzi wa kikabila kinchi, kivyama ni baba ama ni Mtoto? Nani anayepaswa kuunganisha watu wake wawe wamoja katika familia yenye kuwa na upendo ni baba ama ni Mtoto? Shame on you.

Your example is irrelevant.

Hakuna cha mtoto wala Baba hapo wote wazima wanatakiwa wakemee viashilia vya ubaguzi na utengano.
 
Wanaowasiliana na kamati kuu ya CCM wawaambie kuwa next time wanapotafuta mtu wa kuja kuwa rais wazingatie haya:
1. Mental and psychological assessment
2. Personal background, especially childhood
3. Exposure to the world outside Tanzania
4. People skills
5. Communication skills
6. The ability to read
7. An understanding of the Constitution and the laws of the country
8. Etiquette
9. A receptive mind
10. The ability to unite all people as one nation

Kama ulivyo mchezo wa drafti tumeliwa king.
mbavu zangu
Tumeliwa king
 
Kwani hekima ni nini? Inategemea na tafsiri ya kila mtu na mazingira aliyopo. Hekima kwa mwingine siyo lazima iwe hekima kwa kila mtu. Tusidanganyane. Ni mtazamo tu wa kila mtu na kila mtu yuko huru kufikiri atakavyo. Watu wanategemea wanyenyekewe hali wao hawana unyenyekevu wowote. Lazima wavune wanachopanda.
Tafsiri ya Hekima au (Wisdom) is the right application of knowledge. Sasa wewe tueleze hapa kwamba hayo ni matumizi sahihi ya Madaraka?
 
mwengeso nipe tofauti ya kiongozi na raia! Kwanini kila mtu ni raia lakni si kila mmoja ni kiongozi?
Dhima ya kiongozi ni nini kutengeneza au kuharibu?
Kujenga ama kubomoa?
Kuponya ama kutia jeraha?
Tunapozungumzia busara na tafakuri kwa viongozi ni kwenye mambo kama na si visasi utemi na vitisho
Sifa kuu ya kiongozi ni ni kuwa mkweli na mnyenyekevu (honest). Kuonesha kiwango cha juu cha ukweli na unyenyekevu kwa unaowaongoza. Kukemea waziwazi kila lisilo sahihi. Kuchukua hatua pale jambo lisilo sahihi linapotendeka. Asipofanya hivyo mara nyingi ni dalili ya woga na/au kutokujiamini.
 
Ni aibu sana kwa Rais aliechaguliwa kwa demokrasia kubaka demokrasia na kuchochea chuki dhidi raia wengine! Rais anayetamani kuua kila dakika sababu tu hataki kukosolewa! Koo lake limejaa kiu ya damu tu!! Tumekosea wapi? Mungu atusaidie! Haya sio maendeleo! Libya ndio mfano mkuu hajui kw nini watu wa Libya walichoka utawala ule! Yeye anashikilia kitu kisicho mashiko! Amani! Hakuna amani kama haki imekandamizwa na kubakwa! Libya hawakuwa na furaha zile vitu vya bure haikuwa favor ni mali zao! Walitaka haki yao uhuru na demokrasia hasa kuamua na kukosoa na kuchangia........
 
Sifa kuu ya kiongozi ni ni kuwa mkweli na mnyenyekevu (honest). Kuonesha kiwango cha juu cha ukweli na unyenyekevu kwa unaowaongoza. Kukemea waziwazi kila lisilo sahihi. Kuchukua hatua pale jambo lisilo sahihi linapotendeka. Asipofanya hivyo mara nyingi ni dalili ya woga na/au kutokujiamini.
Hapo kwenye unyenyekevu ni humbleness...umeongea vizuri sana..tukiwa na viongozi wa namna hii taifa litashamiri katika nyanja zote...na tungeshuhudia mabadiliko chanya na ustawi wa jamii....bahati mbaya sana wengi wetu tunadhani tumepata kumbe tumepatikana
 
Ngoma ikivuma sana hupasuka na mwenye kiburi akishupaza sana shingo huvunjika mara
Tuwe na tuo tuwe na tafakuri kwenye maneno yetu...mtu anayejisifia rohombaya wazi wazi sio kwamba hana tu hekima lakini pia hana saburi na hatafakari matokeo ya kauli zake..huyu ni mwovu
Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri, bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu, huchochea ghadhabu huchochea visasi chuki na ubabe....dhima ya kiongozi ni kuleta umoja na maridhiano sio kuchochea chuki na visasi
Kiongozi mwenye hekima kamwe hawezi kuongea karaha..karaha huleta simanzi na majonzi, mtu wa karaha hana ogofyo lolote, ni kiburi na kiburi chake ni anguko
Nuru ya mtu mbaya huzimika ghafla bila tahadhari bila taarifa...mtu wa hekima hutengeneza patano kwa njia ya mashauriano
Je tunatengeneza ama tunabomoa?
Je tunahubiri amani ama visasi?
Je tunaeneza ustawi au anguko?
Je Tunafundisha hekima au upuuzi?
-hakuna kitu kibaya kama kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi
Brother siku nikija dar naomba nikutafute pls.
 
Back
Top Bottom