Andrew Chenge achukua fomu ya kugombea Uspika. Fahamu kuhusu wasifu wake

Hili Nchi iwe mikono salama kwa Mama Samia Bora Masele , huyu chenge Maghufuli na ukali wote alimshindwa mjuaji, fisadi na Umri umeshaenda

Hachelewi kumpindua Raisi akitumwa na genge la wahuni
Unakosea sana, huu ni mhimili mwingine, hauihitaji mtu mtiifu kwa rais bali mtu mwenye misimamo thabiti kusimamia bunge kama muhimili na taasisi inayojitegemea
 
Chenge afai kuwa kiongozi hana maadili,ni mwizi,mbadhilifu atapisha hoja za mikataba ya upigaji bungeni
 
Habari ndio kama mnavyoisikia ndugu zangu, mzee wa vijisenti ambaye inasemekana ana akili nyingi kuliko wagombea wengine wote waliokwishachukua fomu, leo tarehe 12/01/2022 amejitosa kwenye kinyang'anyiro hicho.

WASIFU

KUZALIWA

- Mbobezi wa Sheria Barani Afrika na "Alumni" wa Chuo kikuu bora Duniani- Havard cha Nchini Marekani Mh.Andrew John Chenge alizaliwa mwaka 1947 nchini Tanzania (Tanganyika wakati huo).

ELIMU

- Nguli huyu wa Sheria alianza safari ya kitaaluma katika Shule ya msingi Sasago (Musoma) kati ya mwaka 1955- 1958

- Kisha akajiunga na St. Pius Seminary Makoko Musoma kati ya mwaka 1959-1962

- Kisha akajiunga na St.Mary's Seminary Nyegezi mwanza kati ya mwaka 1963-1966 kwaajili ya masomo ya Sekondari.

- Kati ya mwaka 1967 - 1968 alijiunga na Mkwawa High school.

- Mwaka 1969 alikuwa kati ya wanafunzi wachache waliojiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kwaajili ya masomo ya Sheria (LL.B) na kufanikiwa kuhitimu kwa ufaulu wa juu mwaka 1972.

- Mwaka 1974 - 1975 alibahatika kuwa kati ya wanasheria wachache Duniani kujiunga na Chuo Kikuu cha Havard kwaajili ya Shahada ya uzamili aliyohitimu kwa ufaulu mkubwa.

UTUMISHI NA UZOEFU SERIKALINI

- Kati ya mwaka 1972 - 1990 alihudumu kama mwanasheria wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

- Kati ya mwaka 1990- 1992 alihudumu kama Naibu Mwanasheria Mkuu (D/AG)

- Kati ya mwaka 1993 -2005 alihudumu kama Mwanasheria mkuu wa serikali.

- Mwaka 2006 alihudumu kama Waziri wa Kwanza wa Ushirikiano wa Afrika mashariki

- Kati ya 2006-2008 alihudumu kama Waziri wa miundombinu katika serikali ya awamu ya nne.

UZOEFU KATIKA BUNGE

- Kati ya mwaka 2005 - 2020 alihudumu kama Mbunge wa Jimbo la Bariadi Magharibi

- Kati ya mwaka 2008 - 2010 alihudumu kama mjumbe wa kamati ya Bunge ya Uchumi na Fedha.

- Kati ya mwaka 2012-2013 alihudumu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi na Fedha

- Kati ya mwaka 2013-2015 alihudumu kama Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti

-Kati ya mwaka 2015- 2020 alihudumu kama Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Sheria na pia kama mmoja wa Wenyeviti 3 wa Bunge.
umesahau kashifa mbalimbali alipokua mwanasheria mkuu serikali ya ccm Chini ya benjamini mkapa .....malizia ndg kuhusu joka lenye makengeza
 
Unakosea sana, huu ni mhimili mwingine, hauihitaji mtu mtiifu kwa rais bali mtu mwenye misimamo thabiti kusimamia bunge kama muhimili na taasisi inayojitegemea

Hatutaki mtu atakaemsumbua Mh Raisi hatutaki speaker ataemvimbia Mh Raisi , hatutaki mtu mwenye mipango miovu ya kumpindua mh Raisi
Tunataka mtu watakaelewana na mama Samia tunataka Tanzania ya Amani na Furaha kwa sisi Wananchi na viongozi wetu
 
Mpaka leo bado huwa najiuliza maana ya kujiita joka la makengeza!

Maana yake nini na joka lenye makengeza linafanya nn
Kwamba wewe ukiona lina tazama kushoto, ila kiuhalisia lina tazama kulia. Kwamba huwezi jua uelekeo wake linapokua kwenye mission
 
Huyu sasa ndio atakuwa Spika,, kwanza ashakuwa mwenyekiti sana..

Ila sasa ndio keki ya taifa ijiandae,,,Mapande anayokula chenge ni makubwa makubwa sana
 
Mkakati umeshamalizika na umesukwa jinsi ulivyotakiwa baada ya Kufanikisha lile Kubwa la tarehe 17 Machi, 2021 sasa wanaenda Kukamilisha la kumuweka Fisadi wa Kinyantuzu kuwa Spika Mpya ili CCM Mtandao ya Upigaji irejee tena.
 
Mkakati umeshamalizika na umesukwa jinsi ulivyotakiwa baada ya Kufanikisha lile Kubwa la tarehe 17 Machi, 2021 sasa wanaenda Kukamilisha la kumuweka Fisadi wa Kinyantuzu kuwa Spika Mpya ili CCM Mtandao ya Upigaji irejee tena.
Wanyantuzu ni Wasukuma wenyeji wa Wilaya za Bariadi na Itilima mkoani Simiyu.
 
Mbona unamsifia nusu nusu?! Hebu tupe na wasifu wake kuhusu ESCROW ili tupate kumjua vizuri.
Kwani Chenge kwenye Escrow alifanya nini? Kupewa pesa na rafiki yake Rugemalira ndiyo kosa? Na kama ni kosa mbona hakuzirudisha na hakuna aliyempeleka Mahakamani,na mwenye pesa zake mwisho wa siku si ameachiwa huru,acheni chuki zisizo kuwa na mashiko.Go Mtemi Chenge,kiti cha uspika ni chako,hakika unastahili.
 
Back
Top Bottom