Anayejua sehemu yoyote penye ujenzi wa barabara kwa sasa anistue. Mimi sijaona tangu awamu ya 6 iingie madarakani


Kipindi cha miezi mitatu iliyopita nilikuwa katika mikoa hi, na hiki ndicho nilichoshuhudia.

Dar- Daraja la juu ( flyover) ya Uhasibu inajengwa. Shule zote za kata zina madarasa.

Mbeya- Kyela ,Shule za kata karibu zote zina majengo/ madarasa mapya. Mafundi wa kawaida wametumika.

Mwanza- Kisesa pamejengwa kambi ya ujenzi wa reli ya Mwendokasi)umeme inayoanzia Mwanza-Shinyanga-Tabora-Singida. Nahisi ni wachina

Dodoma- Bahi reli ya umeme inajengwa, tuta limepandishwa na reli imewekwa. Nembo za vifaa vya muhandisi vinasoma Yap Merkaz

Mara- Barabara za Bunda-Ghuta -Chisorya, Bunda- Nyamswa, Salama - Nata- Mugumu mkandarasi wa kichina yupo kazini.
 
Kuanzia Magomeni kuelekea Mbagala wanajenga mwendokasi. Mataa ya VETA wanajenga flyover, kuna SGR inajengwa vipande mbalimbali, bwawa la umeme na Feb moja wamemaliza ujenzi wa daraja Agha Khan
Zilianza pindi. Baba akiwa madarakani so lete za after alipotoka madarakani
 
Zilianza pindi. Baba akiwa madarakani so lete za after alipotoka madarakani
Baba yako aliacha pesa za kujengea? Kwa nini hakuzimaliza kwa miaka 6? Alitaka aje azimalize Samia kwa mwaka mmja?

Ikumbukwe mwezi huu Samia atatimiza mwaka mmja mara baada ya kula kiapo cha kuwa Rais,kwa hiyo ulitaka Kazi ambayo haikumalizika kwa miaka 6 amalize ndani ya mwaka mmja?
 
Ijapokuwa mimi si mshabiki wa kijani lakini juzi wakati natokea Kigoma kwenda Kampala uganga nimeona wakandarasi kuanzia Makele Kigoma mpaka Kakonko wana magari mengi yameandikwa sharkman. Ni makampuni ya wachina ila sikuwa makini sana kuyasoma sababu nilichoka sana kwa kupita kwenye njia za mchepuko lakini kwingineko sijaona
Nilipita hapo June 2020 walikuwepo. Nakumbuka watu wa Kakonko walikuwa positive sana. Tulisimama pale kula chakula

Sent from my Lenovo L38111 using JamiiForums mobile app
 
Huku makongo kuna kikampuni kinajenga kilometa moja ya barabara mwaka wa kumi huu wanahangaika hapo hapo, mara wamwage maji, kifusi, kokoto, watifuetifue, wanaanza hapa wanaacha, wanahamia kwingine wanaacha, wanaweka pale lami wanaacha, wanarudi tena baada ya mwaka wanachimba mashimo. Kifupi ni kwamba wanahangaika tu na barabara haiishi...........sasa nikawa najiuliza hawa wakipewa kilometa 500 wanaweza kutumia karne nzima kukamilisha.​
 
Kiukweli wapigania legacy wamekwama kiasi kwamba hawajui hata pakutokea, yaani wamechanganyikiwa. Ushahidi ni huu uzi wa huyu mlinda legacy aliyezunguka kitongoji cha kilolo huko na kisha kudhani kuwa amezunguka Tanzania nzima.....wanachekesha sana!!

Mama ukimaliza kuhitimisha hii miradi ya marehemu jpm, shughulikia, kwa nguvu zote na kwa uhakika, kero ya jangwani wazidi kuchanganyikiwa.......tunataka kuona kiwango cha mwisho cha kuchanganyikiwa kinakuwaje!!
 
Kiukweli wapigania legacy wamekwama kiasi kwamba hawajui hata pakutokea, yaani wamechanganyikiwa. Ushahidi ni huu uzi wa huyu mlinda legacy aliyezunguka kitongoji cha kilolo huko na kisha kudhani kuwa amezunguka Tanzania nzima.....wanachekesha sana!!

Mama ukimaliza kuhitimisha hii miradi ya marehemu jpm, shughulikia, kwa nguvu zote na kwa uhakika, kero ya jangwani wazidi kuchanganyikiwa.......tunataka kuona kiwango cha mwisho cha kuchanganyikiwa kinakuwaje!!
Maneno matupu bila picha/ video??
 
Huku makongo kuna kikampuni kinajenga kilometa moja ya barabara mwaka wa kumi huu wanahangaika hapo hapo, mara wamwage maji, kifusi, kokoto, watifuetifue, wanaanza hapa wanaacha, wanahamia kwingine wanaacha, wanaweka pale lami wanaacha, wanarudi tena baada ya mwaka wanachimba mashimo. Kifupi ni kwamba wanahangaika tu na barabara haiishi...........sasa nikawa najiuliza hawa wakipewa kilometa 500 wanaweza kutumia karne nzima kukamilisha.​
🤣🤣🤣🤣wachovu hao.
 
Kuanzia Magomeni kuelekea Mbagala wanajenga mwendokasi. Mataa ya VETA wanajenga flyover, kuna SGR inajengwa vipande mbalimbali, bwawa la umeme na Feb moja wamemaliza ujenzi wa daraja Agha Khan
Weka picha
 
Kuanzia Magomeni kuelekea Mbagala wanajenga mwendokasi. Mataa ya VETA wanajenga flyover, kuna SGR inajengwa vipande mbalimbali, bwawa la umeme na Feb moja wamemaliza ujenzi wa daraja Agha Khan
Nina mashaka na hii.mwendokasi inaweza ikaisha 2027. Binafsi kwa jinsi navyoona uendeshaji wa BRT ulivofeli vibaya ninashauri zingejengwa barabara nyingi tuu lakini sio mwendokasi tena .

Sent from my Infinix X605 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom