Assessment ya Utawala wa Awamu ya 6 tangu Machi hadi leo Desemba 31, 2021. So far so good, hongera Samia!

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Utawala wa Awamu ya sita ulianza rasmi tarehe 17 mwezi machi mwaka 2021, Rais Samia alichukua kiti cha Uongozi baada ya kifo cha JPM.

Katika miezi hii 9 na ushee Mama huyu alipochukua kiti cha Uongozi napenda kusema nimeridhika kwa namna ambayo analiongoza Taifa letu pendwa la Tanzania. Amepata mafanikio mengi pamoja na kuwepo kwa changamoto za hapa na pale.

Mafanikio

1. Kiuchumi

Baada ya mkwamo wa miaka kadhaa kutokana na magomvi baina ya Tanzania na majirani zake. Rais Samia alipoingia madarakani jambo la kwanza alilofanya lilikuwa ni kuboresha mahusiano baina ya Tanzania na majirani zake. Kuboreshwa kwa mahusiano haya kumeenda kusababisha Tanzania kuongoza Kwa kuuza bidhaa kwenye Mataifa ya Uganda na Kenya kwa Mara ya kwanza kwenye historia za mataifa haya. Ripoti za Benji kuu za Uganda na Kenya katika mwezi July na Agosti zilisema haya. Haya ni mafanikio

Katika kipindi cha miezi michache aliyokaa madarakani fedha ya Tanzania imepata nguvu zaidi dhidi ya Sarafu ya marekani jambo ambalo Kwa wabashiri wa masuala ya kiuchumi wanasema ni taa ya kijani kwake katika kuipa Tanzania Uchumi mkubwa na kuongoza kiuchumi katika kanda hii ya Afrika Mashariki na Kati katika siku zijazo!

Kwa upande wa hifadhi yetu ya fedha za kigeni chini ya Utawala wake ameomgeza zaidi hifadhi yetu na kutufanya tuongoze kwa Mataifa ya Afrika Mashariki kwa sasa!

2. Kiutalii
Kutokana na kufuata taratibu mbalimbali za kuepukana na corona Tanzania ilishuhudia kupokea watalii wengi zaidi katika kipindi hiki kuliko ilivyokuwa mwaka jana kipindi hiki. Taarifa zinasema mapato ya italii kwa kipindi hiki tu yamepanda kwa zaidi ya Trilioni 1 baada ya Tanzania kupokea watalii laki Saba na ushee ikiipiku kenya katika kipindi cha mwisho cha mwaka huu!

3. Elimu!
Kwenye Elimu katika kipindi hiki kifupi cha Awamu ya sita , Taifa limeshuhudia ujengwaji wa madarasa Bora kabisa Kwa ajiri ya kusomeshea watoto wetu! Ilionekana Kama masikhara ila kwenye kipindi kifupi sana, Taifa letu limeshihudia madarasa mazuri yenye mazingira mazuri sana yakijengwa Kwa ajiri ya watoto wetu. Ingawa watu wanasema pesa hizi ni za mkopo ila ukweli lazima usemwe! Haya ni matumizi safi na Bora zaidi katika kuboresha mazingira ya elimu yetu . Amefanya vizuri sana kwenye hili

4. Miundombinu!
Katika miundombinu amerudi kufanya vizuri sana! Hakuna mradi hata mmoja aliorithi kutoka kwa mtangulizi wake ambao umesimama. Amekamilisha ujenzi wa daraja la Tanzanite, Ujenzi wa Barabara ya Morroco - Mwenye, ujenzi wa Barabara za mji wa Serikali Mtumba ambazo Mtangulizi wake alifariki akiziacha sehemu kubwa zikiwa za vumbi. Ameendeleza ujenzi wa Awamu wa pili wa mji wa serikali na sasa ukiwa Mtumba kila sehemu utakuta ni mabati ujenzi ukiwa unaendelea.

Kwenye Bwawa la Nyerere nako hakujasimama, mafundi wako site wanaendelea na kazi, SGR nako hakujapoa kipande cha Dar - Moro amekikamilisha na sasa kinatarajiwa kufunguliwa muda si mrefu. Amesaini Mikataba ya ujenzi wa vipande vya Dodoma- Tabora na ameanzisha ujenzi wa Mwanza - Isaka.

5. Hospitali
Kama ilivyo kwenye elimu hapa napo Mama Samia hajalala. Ameendeleza na kuanzisha ujenzi wa vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali nyingi sana. Amenunua vifaa na magari mengi kwa ajiri ya hospitali mbalimbali. Huku amefanya kwa kutumia fedha za tozo pamoja na fedha za mkopo wa covid. Amefanya vizuri na hongera kwake

6. Miradi mipya
Pamoja na kufanya na kuendeleza vizuri bila kupoa. Samia ameanzisha miradi mipya. Mradi wa LNG ambao ameanzisha mazungumzo pamoja na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ambao pia ameanzisha mazungumzo. Kwa wachumi miradi hii miwili ndo inatarajiwa kuwa breakthrough ya Tanzania kiuchumi. Anafanya vizuri na ana malengo mazuri!

7. Ubunifu mpya kwenye Utalii
Baada ya malalamiko ya miaka mingi juu ya Taifa la Tanzania na serikali zake kutotumia vizuri fursa za kiutalii ambacho ni moja ya vyanzo vizuri na vikubwa vya mapato kwa Mataifa mengi Duniani, Samia ametumia ubunifu wake kwa kufanya kipindi cha The Royal Tour. Kipindi hiki kinatarajiwa kuiweka vizuri zaidi Tanzania katika ramani ya utalii duniani na kikishaznduliwa kinatarajiwa kuvutia watalii zaidi ya Mil 5 katika nchi hii kwenye miaka ya hivi Karibuni. Kwa hili pia amefanya vizuri sana

8. Ajira
Baada ya kukwama kwa ajira kwa karibu miaka 5 , serikali ya Awamu ya sita kwa miezi hii 9 tu wametoa ajira zisizopungua elfu 15 kwa serikalini tu. Ajira hizi zimetolewa jwtz, magereza, polisi, uhamiaji, zimamoto, pccb na Tra. Pia ametoa ajira za walimu na madaktari. Kwa hili hongera Sana Rais Samia

Changamoto

1. Hujuma kutoka kwa watu wasiomkubali


Hapa amekuwa akipata hujuma kutoka kwa kundi linalojulikana Kama Sukuma Gang ambao hawa hawakutaka awe Rais. Wamekuwa wakimuhujumu kupitia sekta mbalimbali Kama nishati kama kukata umeme hovyo ili kumchonganisha na wananchi wake. Kwenye umeme kundi hili kutokana na kuwa na uhusiano na watu fulani wamekuwa wakuhujumu Tanesko na kusababisha kukatika kwa umeme katika maeneo kadhaa hapa Tanzania. Inasemwa hata katika mikoa ya Rukwa na Katavi ambako umeme ni wa kununua kutoka Zambia nako umeme umekuwa Uko katika kutokana na hujuma tu za kundi hili.

Ni vizuri waziri wake Makamba na watendaji wapya wa Tanesco wakachukulia kuwa hii ni vita na sio vile wanavyoona na wakachukua hatua kali ili kudhibiti hili. Ni vizuri na vyombo vya ulinzi na Usalama vikahusika katika kushughulikia hizi hujuma

2. Kupanda kwa bei za bidhaa

Ingawa hii inaweza kuwa imechangiwa na janga la Corona Ila kwa sehemu fulani Kuna kauzembe kwa watendaji wake katika kuzuia uholela kwenye hili hasa katika Bei za mafuta ya kula, sukari, sabuni na vifaa vya ujenzi.
Hapa akiwabana vizuri Mawaziri wake wa viwanda na biashara anaweza pata suluhisho kwenye hili maana wanaoneka wamerelax sana katika kuzuia hili

Mwisho napenda kuipongeza Awamu ya sita. Si kazi ndogo kuongoza Tanzania lakini mmeonesha mnaweza. Sijagusia kwenye ulinzi na Usalama ambako nako mbao Beka aso dar mko vizuri Ila kiukweli keep it up. So far mko vizuri
 
Hujuma gani amekuwa akizipata kutoka kwa hao so called Sukuma gang? Hivi hao Wasukuma wanao muhujumu ni wana CCM au chadema?

Watu mnao imba mapambio ya Rais kuhujumiwa ndio wapambe nuksi kabisa na chawa wa kiwango cha juu, hivi kweli unaweza kusema ni wapi hao wamemkwamisha na kumuhujumu?

Hivi vijana mbona nmnajipendekeza sana bila sababu?

Mfumuko wa bei wa huduma na bidhaa nao ni sukuma gang?

Umeme nao ni sukuma gang?
 
Unasemaaa?

Halafuuu, Mimi naona kama mnalazimisha" mnachokiandika mnatumia nguvu ya kushinikizwa kuulazimisha uongo uwe kweli

Mitaani, pesa hakuna, bidhaa zinapanda Kila uchwao, soda nazo kwa Mara ya kwanza hazipatikani, maji nayo yameanza kusuasua, maana yake inatafutwa namna hizi bidhaa zipande

Mambo hovyoo tuuu

Maendeleo ni nini?

Ni kuwa na maisha magumu?

Acheni kupamba tusemeni ukweli na ukweli utuweke huru!

Kwani kuboreka kwa mahusiano na mataifa mengine ndo kuifanya sembe iuzwe, 800?

Mtanunua sembe 2000 soon

Endekezeni upuuzi
 
Blah blah kama kawaida ye praise and worship ukweli ni kuwa BADO masha ya wat wengi ni duni hali ya umasikini imeongezeka

We endelea kujifurahisha na mbandiko yako ya kipuuzi wakati nduguzo wanakula mlo mmoja
 
Sukuma gang wamefanyejeee?

Ndio wamefanya bidhaa zipande?

Mdiyo wanasababisha umeme ukatikekatike Kila wakati?

Ndio wamefanya mradi wa umeme Rufiji use uwanja wa siasa?

Soon hao sukuma gang hamtapiga kampeni bila kutaja uwepo wao ili mpewe kura!

Mnatufanya hatuna akili na macho hatuna ya kuuona mnavyokwenda kwenda eeh,
 
kupost matangazo ya ajira na kuajiri ni vitu 2 tofauti, labda ungesema umpongeze kwa kupost matangazo
 
Beauty is in the eye of the beholder, hakuna umeme, hakuna maji, tunakopa kujenga madarasa na madawati ya watoto wetu, kila kitu kimepanda bei lakini “so far so good“ !
 
Unasemaaa?

Halafuuu, Mimi naona kama mnalazimisha" mnachokiandika mnatumia nguvu ya kushinikizwa kuulazimisha uongo uwe kweli

Mitaani, pesa hakuna, bidhaa zinapanda Kila uchwao, soda nazo kwa Mara ya kwanza hazipatikani, maji nayo yameanza kusuasua, maana yake inatafutwa namna hizi bidhaa zipande

Mambo hovyoo tuuu

Maendeleo ni nini?

Ni kuwa na maisha magumu?

Acheni kupamba tusemeni ukweli na ukweli utuweke huru!

Kwani kuboreka kwa mahusiano na mataifa mengine ndo kuifanya sembe iuzwe, 800?

Mtanunua sembe 2000 soon

Endekezeni upuuzi
Kumbe vyuma vimekaza kilikuwa ni kipindi cha awamu ya 6 asante kwa kunifahamisha lakini UKWELI daima hujitenga na unafiki.
 
Beauty is in the eye of the beholder, hakuna umeme, hakuna maji, tunakopa kujenga madarasa na madawati ya watoto wetu, kila kitu kimepanda bei lakini “so far so good“ !
Kipindi haukopi ulijenga madaraka gani?
 
Utawala wa Awamu ya sita ulianza rasmi tarehe 17 mwezi machi mwaka 2021, Rais Samia alichukua kiti cha Uongozi baada ya kifo cha JPM.
Katika miezi hii 9 na ushee Mama huyu alipochukua kiti cha Uongozi napenda kusema nimeridhika kwa namna ambayo analiongoza Taifa letu pendwa la Tanzania. Amepata mafanikio mengi pamoja na kuwepo kwa changamoto za hapa na pale

Mafanikio
1. Kiuchumi

Baada ya mkwamo wa miaka kadhaa kutokana na magomvi baina ya Tanzania na majirani zake. Rais Samia alipoingia madarakani jambo la kwanza alilofanya lilikuwa ni kuboresha mahusiano baina ya Tanzania na majirani zake. Kuboreshwa kwa mahusiano haya kumeenda kusababisha Tanzania kuongoza Kwa kuuza bidhaa kwenye Mataifa ya Uganda na Kenya kwa Mara ya kwanza kwenye historia za mataifa haya. Ripoti za Benji kuu za Uganda na Kenya katika mwezi July na Agosti zilisema haya. Haya ni mafanikio

Katika kipindi cha miezi michache aliyokaa madarakani fedha ya Tanzania imepata nguvu zaidi dhidi ya Sarafu ya marekani jambo ambalo Kwa wabashiri wa masuala ya kiuchumi wanasema ni taa ya kijani kwake katika kuipa Tanzania Uchumi mkubwa na kuongoza kiuchumi katika kanda hii ya Afrika Mashariki na Kati katika siku zijazo!

Kwa upande wa hifadhi yetu ya fedha za kigeni chini ya Utawala wake ameomgeza zaidi hifadhi yetu na kutufanya tuongoze kwa Mataifa ya Afrika Mashariki kwa sasa!

2. Kiutalii
Kutokana na kufuata taratibu mbalimbali za kuepukana na corona Tanzania ilishuhudia kupokea watalii wengi zaidi katika kipindi hiki kuliko ilivyokuwa mwaka jana kipindi hiki. Taarifa zinasema mapato ya italii kwa kipindi hiki tu yamepanda kwa zaidi ya Trilioni 1 baada ya Tanzania kupokea watalii laki Saba na ushee ikiipiku kenya katika kipindi cha mwisho cha mwaka huu!

3. Elimu!
Kwenye Elimu katika kipindi hiki kifupi cha Awamu ya sita , Taifa limeshuhudia ujengwaji wa madarasa Bora kabisa Kwa ajiri ya kusomeshea watoto wetu! Ilionekana Kama masikhara ila kwenye kipindi kifupi sana, Taifa letu limeshihudia madarasa mazuri yenye mazingira mazuri sana yakijengwa Kwa ajiri ya watoto wetu. Ingawa watu wanasema pesa hizi ni za mkopo ila ukweli lazima usemwe! Haya ni matumizi safi na Bora zaidi katika kuboresha mazingira ya elimu yetu . Amefanya vizuri sana kwenye hili

4. Miundombinu!
Katika miundombinu amerudi kufanya vizuri sana! Hakuna mradi hata mmoja aliorithi kutoka kwa mtangulizi wake ambao umesimama. Amekamilisha ujenzi wa daraja la Tanzanite, Ujenzi wa Barabara ya Morroco - Mwenye, ujenzi wa Barabara za mji wa Serikali Mtumba ambazo Mtangulizi wake alifariki akiziacha sehemu kubwa zikiwa za vumbi. Ameendeleza ujenzi wa Awamu wa pili wa mji wa serikali na sasa ukiwa Mtumba kila sehemu utakuta ni mabati ujenzi ukiwa unaendelea.

Kwenye Bwawa la Nyerere nako hakujasimama, mafundi wako site wanaendelea na kazi, SGR nako hakujapoa kipande cha Dar - Moro amekikamilisha na sasa kinatarajiwa kufunguliwa muda si mrefu. Amesaini Mikataba ya ujenzi wa vipande vya Dodoma- Tabora na ameanzisha ujenzi wa Mwanza - Isaka.

5. Hospitali
Kama ilivyo kwenye elimu hapa napo Mama Samia hajalala. Ameendeleza na kuanzisha ujenzi wa vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali nyingi sana. Amenunua vifaa na magari mengi kwa ajiri ya hospitali mbalimbali. Huku amefanya kwa kutumia fedha za tozo pamoja na fedha za mkopo wa covid. Amefanya vizuri na hongera kwake

6. Miradi mipya
Pamoja na kufanya na kuendeleza vizuri bila kupoa. Samia ameanzisha miradi mipya. Mradi wa LNG ambao ameanzisha mazungumzo pamoja na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ambao pia ameanzisha mazungumzo. Kwa wachumi miradi hii miwili ndo inatarajiwa kuwa breakthrough ya Tanzania kiuchumi. Anafanya vizuri na ana malengo mazuri!

7. Ubunifu mpya kwenye Utalii
Baada ya malalamiko ya miaka mingi juu ya Taifa la Tanzania na serikali zake kutotumia vizuri fursa za kiutalii ambacho ni moja ya vyanzo vizuri na vikubwa vya mapato kwa Mataifa mengi Duniani, Samia ametumia ubunifu wake kwa kufanya kipindi cha The Royal Tour. Kipindi hiki kinatarajiwa kuiweka vizuri zaidi Tanzania katika ramani ya utalii duniani na kikishaznduliwa kinatarajiwa kuvutia watalii zaidi ya Mil 5 katika nchi hii kwenye miaka ya hivi Karibuni. Kwa hili pia amefanya vizuri sana

8. Ajira
Baada ya kukwama kwa ajira kwa karibu miaka 5 , serikali ya Awamu ya sita kwa miezi hii 9 tu wametoa ajira zisizopungua elfu 15 kwa serikalini tu. Ajira hizi zimetolewa jwtz, magereza, polisi, uhamiaji, zimamoto, pccb na Tra. Pia ametoa ajira za walimu na madaktari. Kwa hili hongera Sana Rais Samia

Changamoto

1. Hujuma kutoka kwa watu wasiomkubali


Hapa amekuwa akipata hujuma kutoka kwa kundi linalojulikana Kama Sukuma Gang ambao hawa hawakutaka awe Rais. Wamekuwa wakimuhujumu kupitia sekta mbalimbali Kama nishati kama kukata umeme hovyo ili kumchonganisha na wananchi wake. Kwenye umeme kundi hili kutokana na kuwa na uhusiano na watu fulani wamekuwa wakuhujumu Tanesko na kusababisha kukatika kwa umeme katika maeneo kadhaa hapa Tanzania. Inasemwa hata katika mikoa ya Rukwa na Katavi ambako umeme ni wa kununua kutoka Zambia nako umeme umekuwa Uko katika kutokana na hujuma tu za kundi hili.

Ni vizuri waziri wake Makamba na watendaji wapya wa Tanesco wakachukulia kuwa hii ni vita na sio vile wanavyoona na wakachukua hatua kali ili kudhibiti hili. Ni vizuri na vyombo vya ulinzi na Usalama vikahusika katika kushughulikia hizi hujuma

2. Kupanda kwa bei za bidhaa

Ingawa hii inaweza kuwa imechangiwa na janga la Corona Ila kwa sehemu fulani Kuna kauzembe kwa watendaji wake katika kuzuia uholela kwenye hili hasa katika Bei za mafuta ya kula, sukari, sabuni na vifaa vya ujenzi.
Hapa akiwabana vizuri Mawaziri wake wa viwanda na biashara anaweza pata suluhisho kwenye hili maana wanaoneka wamerelax sana katika kuzuia hili

Mwisho napenda kuipongeza Awamu ya sita. Si kazi ndogo kuongoza Tanzania lakini mmeonesha mnaweza. Sijagusia kwenye ulinzi na Usalama ambako nako mbao Beka aso dar mko vizuri Ila kiukweli keep it up. So far mko vizuri
HII NI AWAMU YA TANO KIPINDI CHA PILI

Hili tu limenifanya niishie kusoma kichwa cha habari ambacho "MBOJI" au Shudu au Kinyesi chepesi.

Nime kudis grade kwa kitendo chako cha kusema ni awamu ya 6.

Ni awamu ya 6 hewa

Kiongoz tuambie "WEWE NI PRAISE SINGER WA MAMA

Hivi unaimbia SAUTI YA NGAPI?😃🤣🤣🙄🙄
 
Siasa hazifai kuwepo kwenye kila kitu .

Factor gan za kiuchumi umezitumia kuthibitisha huyo Mama kuinua uchumi kwa miezi 9 tu?

Hapo hujazungumzia ongezeko la uzalishaji kwenye sekta mbalimbali hasa viwanda uchumi unakua vipi wakati kuna mahali wanashinda siku nzima hakuna umeme wala maji?

Tuangizie uhitaji na ongezeko la ajira hasa sekta binafsi ambayo mtangulizi wake kwa ushamba wake aliamini serikali inaweza kufanya kila kitu hata kuuza nyanya shame ! aliua sekta binafsi kabisa .

Tukiangalia ubora wa maisha naona bado uko chini sana hiyo nguvu ya sarafu unayosema imekua sioni kabisa ni ngonjera tu.

Nimehitimisha kwa kuona bandiko hili ni siasa tupu..
 
Back
Top Bottom