Anayejua dalili za limbwata, ashushe elimu

Anayejua dalili za limbwata, ashushe elimu

Omary - Msamalia

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2020
Posts
2,077
Reaction score
4,523
Aisee wanajamvi nashindwa kuelewa kama ni upendo pekee au kuna kichochezi..

Huyu mwanamke Mama watoto wangu kila kitu anachotaka kutoka kwangu ninampatia kwa gharama yoyote ile.

Akinikwaza kidogo tu nikimwambia akijibu tu ninatulia, kila akisema jambo namsikiliza.

Yaani napoteza sauti yangu taratibu juu yake. Ndugu zangu hebu niambieni mtu aliyepewa limbwata anakuwaje?
 
Ungekuwa mnywaji wa pombe ningekushsuri anza kurudi saa nane usiku uone
Kwa wanawake tuliokomaa kiakili hatutishiki na mume anaerudi usiku wa manane kwa maana inatafsiri yafuatayo; kwamba kurudi saa nane Ni wazi huko ulikokuwa haukuwa na mwanamke na Kama ulikuwa nae Basi hamjakutana kimwili, ama la mmekutana ila hamjachoshana, Ni ngumu sana kumuacha mwanamke/kimada wako kitandani saa tisa usiku eti unarudi kwa mkeo obviously utaona heri urudi asubuhi tu,

Kama ikiwa kinyume chake yani unae kimada na ukamuacha usiku mkubwa hivyo kuwahi kwa mkeo trust me unamuheshimu sana na kumuogopa mke wako, naamini mwanaume wa kurudi usiku mnene Ni ama iwe tabia yake au kapata dharula ila siaminigi kuwa eti katokea kwa kimada, kuliko wanaorudi ndani saa mbili mpaka saa tatu usiku hao wengi wanakuwaga na vimada Tena wamevipangia na nyumba kabisa km mke

Kurudi usiku mnene natafsiri Kama heshima kwa mke, kuliko kurudi asbh
 
Kwa wanawake tuliokomaa kiakili hatutishiki na mume anaerudi usiku wa manane kwa maana inatafsiri yafuatayo; kwamba kurudi saa nane Ni wazi huko ulikokuwa haukuwa na mwanamke na Kama ulikuwa nae Basi hamjakutana kimwili, ama la mmekutana ila hamjachoshana, Ni ngumu sana kumuacha mwanamke/kimada wako kitandani saa tisa usiku eti unarudi kwa mkeo obviously utaona heri urudi asubuhi tu,

Kama ikiwa kinyume chake yani unae kimada na ukamuacha usiku mkubwa hivyo kuwahi kwa mkeo trust me unamuheshimu sana na kumuogopa mke wako, naamini mwanaume wa kurudi usiku mnene Ni ama iwe tabia yake au kapata dharula ila siaminigi kuwa eti katokea kwa kimada, kuliko wanaorudi ndani saa mbili mpaka saa tatu usiku hao wengi wanakuwaga na vimada Tena wamevipangia na nyumba kabisa km mke

Kurudi usiku mnene natafsiri Kama heshima kwa mke, kuliko kurudi asbh
Duh! Kweli umekomaa kimahusiano , hebu nyie wengine mumtumie huyu mwenzenu vizuri kwa ustawi wa ndoa zenu.
 
Wewe ulitaka uishi na mkeo kwa kupigana mangumi na mateke kila siku?

Kama Mkeo nae pia anakuheshimu na kukusikiliza basi hilo ni jambo jema,
Mimi naona hizo ni dalili za wewe kukomaa kiakili na kutambua jinsi ya kuyaishi maisha ya ndoa kwa amani na kuepusha ugomvi usio na ulazima,

Achana na mambo ya kufikirika kwenye ulimwengu huu wa leo wa science na technologies,hakuna cha limbwata wala uchawi,hayo hua ni mawazo ya watu masikini.
 
Ukipewa limbwata huwezi kujigundua mwenyewe...

Hapo ni wewe tu umekaliwa kichwani na mkeo...
 
Hapo tayari😆, wanaume cc n wabishi, ww hupo hivyo bc amechengua akili yako kidg🤣🤣🤣 true joke!

Huo ni upendo mkuu,
 
Mungu alipotuumba akampa kila mtu akili na nafsi hakukosea hata kidogo. Hii customization tunayotamani kuifanya kamwe haiwezi kutuacha salama..... Yaani kuwa na mtu huku unajua kabisa kwamba sio akili yake kwangu mimi najionea maumivu tuu😎😎😎

Mara paap unajikuta unaishi na robot badala ya kuishi na mtu mwenye maamuzi yake binafsi
 
Hakuna limbwata hayo ni mahaba tu kama ya Lowasa, kugombea urais 2015.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom