Mtu mmoja mwenye hekima aliwahi kusema hivi : " UKIONA WATU USIO FAHAMIANA NAO WANAKUCHUKIA, BASI JUA WANAKUKUBALI SANA, ILA WANACHUKIA KWANINI WANAKUKUBALI "
Kwa muda mrefu sasa tangu aanze kujihusisha na masuala ya Social Network, Lemutuz amekuwa muhanga wa lugha za dharau, kejeli na matusi kutoka kwa watu mbalimbali wanao tumia mitandao hiyo.
Kila mara jina la LEMUTUZ linapotajwa hapa JF au kule Tanuru la Fikra basi kinacho fuatia huwa ni lugha za matusi, kejeli na kashfa. Watu wengine wanatoa lugha komenti zao katika namna inayo onyesha kuwa wana uchungu sana mioyoni mwao....
Nilijaribu kufanya uchunguzi wangu kujua ni kitu gani kinacho wafanya watu wamchukie Lemutuz kwa kiwango hicho? Sikupata sababu yoyote ya msingi, isipokuwa nilicho kiona ni hicho hapo juu nilicho kisema. Watu wanamkumbali Lemutuz but wanachukia kwanini wanamkubali Lemutuz, mwisho wa siku wanaishia kuexpress their feelings kwa kuandika lugha zisizo faa dhidi ya brother huyu.....
Kwa sisi watu tunao tazama mambo kwa jicho la INRI huwa hatupendi kuona mtu anaonewa bila sababu ya msingi. Tunaamini hakuna mtu aliye mkamilifu...