Anaitwa Roma: Wimbo mpya wa Roma Mkatoliki

Kundi kubwa la hadhira hawataki kusikia vitu kama hivi wanapenda anasa musik tu
 
Roma Mkatoliki ni ameamua kujilipua ama? Binafsi sijamuelewa au labda amepewa go ahead na system.

Wimbo mzima ukiusikiliza kwa umakini ni kama ameamua kumnanga "prince".

Pale anaposema "mjibuni mmemzaa Mpare ila siwachukii Wasukuma."

Naendelea kuamini, aidha Roma ameamua potelea mbali liwalo na liwe ama amepewa kinga na wasiojulikana.
"Anitwa Roma nani wakumnyamazisha"
 
Missile of the Nation,
Imefika wakati sasa watambue kuwa vitisho na maguvu yanayokandamiza uhuru wa kujieleza na free press yanauongezea nguvu sana kuliko kuunyamazisha.

Watambue kabisa kwamba huu wimbo wa Roma ni kielelezo cha mtu aliyenyimwa uhuru wa kujieleza ndiyo maana kwa leo una trend sana. Kila aliyekandamizwa anaona wimbo wa Roma kama ni ukombozi kwake.

Wao wanapoteza muda kuwanunua akina Harmonize na Nandy kupiga manyimbo ya kuwasaidia kwa kuwapa hela au kuwaahidi kugombea ubunge. Hiyo ni kazi bure kwa kuwa sanaa huja automatically, hainunuliwi.

Meko aambiwe kuwa kadri anavyozuia uhuru wa kujieleza na vyombo vya habari kwa kuogopa kukosolewa ndiyo anazidi kujenga nyongo ya chuki kwa Watanzania. Bora uwaache watu wajisemee, wakukosoe ili ujue unakosea wapi na ujisahihishe kuliko kulazimisha vyombo vya habari kukusifia kuanzia asubuhi hadi usiku.

Anayosema Roma ndiyo ukweli na anawakikisha maoni ya watu wengi, tunahitaji afya, elimu, maji safi kuliko huko kwenye mabombadier alikojielekeza
 
Nyimbo za ukombozi zinahitajika sana kwa nchi zinazoendelea kama TZ. Ukombozi huu ni wa kisiasa, kiuchumi, na kijamii.

Nchi zinazoendelea zinakabiliwa na matatizo kibao, na sanaa ni zana mojawapo ya kuibadilisha jamii, lakini wasanii wa sasa wao ni kuimba mapenzi na raha raha tu, wakati matatizo kibao!
 
Huyo mtu ni nani? Mbona kama kokoto la Lucas Mkenda
Hili hapa sasa kokoto lenyewe
IMG_20191115_143429.jpeg
 
Roma asema kimafumbo




Hakika nimeshindwa kujizuia usiku huu kuwaletea wimbo huu wa Roma Mkatoliki ambao kwa maoni yangu hakuna kwa sasa wimbo uliojaa hamasa za Kisiasa katika wakati huu mgumu wa siasa za kishamba.
Ndani ya mashairi yake amefunguka kisanii kumtaja mtekaji wake na mambo mengi ya hovyo ya utawala huu.
Tuusikilize na kuuchambua mstari baada ya mstari.
Natamani colabo ya Roma,Stamina na Sugu na Prof J siku moja.
Itapendeza sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom