Ana 400,000 mfuko wa shati. Anahitaji ushauri

Ana 400,000 mfuko wa shati. Anahitaji ushauri

Atafute mtu wa sokoni kwenye soko la matunda awe anampelekea machungwa halafu Aje Muheza Tanga huu ni msimu wa machungwa , kwa hela yake hiyo hatakosa kununua machungwa 5000 na ajitahidi chungwa lifike sokoni kwa bei ya Tsh 50 au 60 hata akiuza kwa bei ya jumla ya Tsh 80 hatakosa Tsh 20 ya Faida kwa kila chungwa kwa hiyo kwa machungwa 5000 hatakosa Faida ya TSH 100000 kumbuka Mzunguuko huo unaweza kuchukua wiki moja
 
Kuna mshkaji wangu kaamua kuachana na utumwa wa kuajiriwa. Amekusanya kiasi cha Tsh. 400k na kuniomba ushauri wa kipi afanye ili asije kujuta

Nimemwambia anipe muda nimuangalizie. Na muda huo nalileta suala hili mbele ya JF, where we dare to talk openly.

Anaishi Manzese Dar es salaam. Amekataa kata kata biashara ya kubet ama Folex

Ushauri wenu ndugu katika Bwana...
cha muhimu ni NIA unaweza kuanza na chochote
 
Biashara mpya kama una uvumilivu unafunga mapema.
Pesa hiyo ni kutafuta mwenzake mwenye pesa kama yeye wakashirikiana biashara yoyote itakayokuwa fursa kwao
 
Kuna mshkaji wangu kaamua kuachana na utumwa wa kuajiriwa. Amekusanya kiasi cha Tsh. 400k na kuniomba ushauri wa kipi afanye ili asije kujuta

Nimemwambia anipe muda nimuangalizie. Na muda huo nalileta suala hili mbele ya JF, where we dare to talk openly.

Anaishi Manzese Dar es salaam. Amekataa kata kata biashara ya kubet ama Folex

Ushauri wenu ndugu katika Bwana...
Uyo jamaa ako ndo wewe
 
Nimekuc
Ok karibu sana

👉 Kuna hizi biashara japo mtaji ni mdg akikomaa anatoka, kikubwa ajitahidi apate backup maake Kuna wakati mtaji unazingua ko backup ni muhimu biashara hizi hapa 👇

👉 Genge la matunda namaanisha maembe, parachichi, azingatie matunda fresh, usafi, na eneo.

👉 Anaweza Kuchoma kuku tu, Tena kwa uswahilini huko ni vzr zaidi anaanza na kidogo kusoma eneo.

👉 Kuna kuuza mitumba masoko kama ya manzese, mwenge na sehemu zenye minada ikiwa yupo tyr!

👉 Akikubali kufanya baba lishe napo kwa kuanzia sio mbaya hapa anatafuta kijiwe kizuri anakitengeneza kinakaa anaanza kutoa huduma.

👉Kuna biashara ya kupika chapati na maharage na supu hii ni unatafuta eneo lolote hata sio lzm fremu!

👉 Kuna kuchemsha supu, miguu, kichwa, ndizi na mtori tuu inakuwa ni supu center uswahilini zinatoka sana

👉 Kwa upande wangu biashara zipo hizo though zipo nyingi sana.
Nimekucheki DM mkuu
 
Biashara ukishauriwa kwa maneno unaweza kuona umekuwa tajiri tayari.... Ipeleke kwenye vitendo sasa..

Niliwahi kushauriwa biashara fulani ambayo kwa siku nitaingiza tsh elf 10..

Mwisho wa cku hata elf 3 nilikuwa sipati..

NB: Sikatish tamaa ila ukipewa idea fulani usijipe mategemeo makubwa.. biashara ni risk
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom