Ameondoka nyumbani

Ameondoka nyumbani

Hapo ndio unapokosea, kumuachia aje anavyotaka. Shut him off jumla ili mfanye maamuzi haraka na maisha yaendelee. Mapenzi ya kubipu bipu hayana maana. Alijijua ana mtoto, kilimuondoa nini? Mkubalianevisitation, la sivyo uanze process za divorce
. every after few days anakuja kwa kigezo cha kumsalimu baby. namuangalia tu.
 
Usiwaze sana,wakati huponya maumivu yote.

Tulia,tazama mbele na endelea kupambana kwani kuondoka kwake si mwisho wa dunia.

Pole sana.
 
Mtu kama huyo unahangaika nae ili iweje!!! huyo anataka attention yako tu, mwambie kama vipi ahame hata nchi...
 
Reason ya nane to hate you for thinking like me! Zikifika 10 nakuchukulia hatua.
Kwa kweli zombie ana hasara, siwezi ng'ang'aniza ndoa kabisa. SIjui kwenda kwa mchungaji au baraza la usuluhishi? Ataenda yeye not me.

Akihama tu, nabadili na vitasa, mlinzi na mbwa wapya!
 
Mwanaume wa ukweli na jasiri hawezi kuhama nyumba yake. No matter what. Huyu mwanaume ana hawara au kwao wana laana. Unamkimbia mke na mtoto?? Halafu mwanao alelewe na nani? Huu ni upimbi na ulimbukeni. Dada nakushauri piga moyo konde lea mwanao kwa furaha. Sali sana Mungu akupe faraja maana ndiye kitulizo cha kweli. Maisha ni lazima yawepo tena jitahidi kama una kazi yako kazana na maisha. Tafuta mali zako na andika majina yako. Kwa muda huu omba Mungu asikuletee mpenzi kabisa ili upate muda wa kutafakari maisha yako. Pole sana. Jiamini kuwa you can stand out without him. Mwanaume nyambafu huyu.
 
muombe Mungu akupe ujasiri, akituma msg mjibu ili ujue ulimkosea nini,hamna mtu anaehama kwake bila sababu nzito,jishushe yaishe
 
Watu wanahama vyumba na vitanda ila siyo nyumba...huyu mwanaume ana maisha ya kifilipino..
 
Hii hali imeanza kukua sasa ya wanaume kuacha nyumba zao na kwenda kupanga lakini inawezekana wewe ni sababu ya yeye kuwa kama alivyo eidha kwa malalamiko yasiyoisha , kutaka kumcontroll na kucontroll kila analofanya, kumchagulia marafiki na labda kumkataza kunywa pombe!kilazima kila kitu kinafanyika taratibu.
Hivi kila mwanaume akiwehuka akaanza kutoa maamuzi yasioeleweka lawama ni lazima abebeshwe mkewe?
Mwehu tu huyo,kama kweli kuna alilokerwa na mkewe ameshindwaje kulisema akakimbilia kuhama?
 
muombe Mungu akupe ujasiri, akituma msg mjibu ili ujue ulimkosea nini,hamna mtu anaehama kwake bila sababu nzito,jishushe yaishe
Ajishushe ili nini? Hana alichokosewa huyo mume,labda amekosa yeye kiasi hawezi tena mtazama mkewe usoni akaamua kuhama!
Dawa ni bint kukaza tu,am block kabisa ikibidi.
Kwa nini anamuweka in suspense msichana wa Watu? Kama ameamua kusonga basi wahitimishe yaliyokuwa maisha yao pamoja kila mtu ashike njia!
 
Mume ameniacha, kaenda kupanga nyumba sehemu nyingine, ananiambia tuachane sababu hatufanani.

Mbaya ananitumia meseji kila siku usiku akiniambia jinsi gani ananimiss na kuwa ni jinsi gani moyo wake unamuuma kwa kuniacha ila inambidi aniache tu.

simjibu. Anaamini baada ya muda haya maumivu yatatuisha na tutaanza upya.

Ananiombea nipate mume mwingine and it is a strong christian marriage.

Nimeumia sana ila sasa naona moyo umeanza kuchukulia kwamba ndiyo hali halisi, ila nimefedheheka sana kujua I married a person mwenye akili za aina yake.

Nilikuwa naamini ana akili njema sana.

Sijui nani kamloga baba mtoto.

Tatizo nyie wanawake sio wa kweli kuelezea tatizo ni nini, mnachofanya ni kutafuta kuonewa huruma hata kama mmekosea
 
muombe Mungu akupe ujasiri, akituma msg mjibu ili ujue ulimkosea nini,hamna mtu anaehama kwake bila sababu nzito,jishushe yaishe

Wanawake waongeaji sana hata wakikosa wao kusa huamishia kwa mwanaume. Mwanaume hana ujasiri wa kumuacha mwanamke, bali mwanamke anao. Afanyacho mwanaume ni kuweka mazingira mwanamke asepe, inapofikia hatua kama iyo ujue huyo mwanamke ni hatari. Hatuwezi jua undani wanajua wao
 
Hivi kila mwanaume akiwehuka akaanza kutoa maamuzi yasioeleweka lawama ni lazima abebeshwe mkewe?
Mwehu tu huyo,kama kweli kuna alilokerwa na mkewe ameshindwaje kulisema akakimbilia kuhama?

Onga nao awo umbuje...! Sema naoo
 
^^
Katika mapenzi, kuna wapenzi wanaitwa rebels! Hawa hawapendi kunyimwa uhuru wao, hawapendi kurudia mambo yale yale nyakati zote, ni wavumilivu wa tabia zinazobadilika. Inapotokea hawaoni mabadiliko kwa wenza wao, huamua kuasi. Huondoka. Huutafuta uhuru wao uliopotea, na huaga! Hilo ndilo lililokupata mleta mada. Kifupi, kwa hulka na silika zao, si rahisi kurudiana. Tafuta mwingine.
^^

uko sahihi
 
Jamani tusimlaumu mtoa mada labda kuna kosa amemfanyia mumewe. .hawa viumbe wa kiume sometime ni maji ya moto kweli
Nilishudia kesi ya baba yangu mkubwa kuama nyumba mnzuri tu tegeta na kuacha mpk watoto wake na kwenda kupanga buguruni chumba sebule na mwanamke mwingine hiyo nyumba alioyopanga choo passport size yaani ni aibu.
 
Jamani tusimlaumu mtoa mada labda kuna kosa amemfanyia mumewe. .hawa viumbe wa kiume sometime ni maji ya moto kweli
Nilishudia kesi ya baba yangu mkubwa kuama nyumba mnzuri tu tegeta na kuacha mpk watoto wake na kwenda kupanga buguruni chumba sebule na mwanamke mwingine hiyo nyumba alioyopanga choo passport size yaani ni aibu.

Mapenzi ni kitu cha ajabu kabisa na chenye vital power kubwa mno
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom