M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
Uzi huu ni swali. Tuelimishane kwa tunaojua jibu la swali.
Viongozi wakuu SMZ wanaomaliza muda wao mwaka huu 2020 na wapya waliotangazwa kushinda kwenye uchaguzi uliomalizika visiwani Zanzibar yawapasa warudi nyuma kidogo, watafakari kwa kina na kujifunza kutokana na historia ya chaguzi za Zanzibar huko nyuma ambazo ziliambatana na umwagaji damu.
Kama kuna ukweli katika kinachoripotiwa na mitandao ya jamii, viongozi wa vyama vya upinzani na vyombo vya habari vya kimataifa kuhusu mauaji ya raia yaliyotokea/yanatokea huko visiwani then viongozi wanaomaliza muda wao na wapya wote yawapasa warejee mauaji yaliyotokea January 2001 baada ya uchaguzi ambao Amani Karume alitangazwa kuwa mshindi dhidi ya Maalim Seif.
Chama kikuu cha upinzani visiwani humo wakati huo (CUF) kiliyapinga matokeo hayo kwa nguvu zote ikiwemo kuitishwa kwa maandamano ya amani ambayo yalishambuliwa na vyombo vya dola na kusababisha maafa makubwa.
Lilikuwa ni doa kubwa jeusi kwa nchi ya Tanzania, na haishangazi kuona Benjamin Mkapa (apumzike anapostahili) akikiri kukereka na tukio hili miaka takribani 20 baada ya kutokea.
Amani Karume alikuwa rais zao la umwagaji damu huo. Komandoo Salmini Amour alikuwa ndiye rais aliyempa kijiti Karume katikati ya umwagaji damu huo. Mkapa alikuwa ndiye amiri jeshi mkuu.
Baada ya miaka kadhaa ya kutafakari haya yote, Amani Karume alikuja kujirudi na kuomba poo na Maalim Seif na kupelekea uundwaji wa serekali ya mseto iliyojumuisha CCM na CUF.
Hadi kufikia leo, Amani Karume ametokea kuwa ni mmoja wa marais wastaafu wa Zanzibar waliojijengea heshima kubwa si kwa Wazanzibari pekee bali kwa jamii yote ya Watanzania.
Hatutamwongelea Mkapa kwani hatunaye tena.
Komandoo Salmini yupo lakini sina uhakika Watanzania wengi wanajua haswa yuko wapi, anafanya nini na ana hali gani maana hata kwenye hadhara zinazojumuisha viongozi wastaafu wa kitaifa haonekani (au ni nadra kumuona).
Je, Komandoo Salmin Amour yu wapi? Nini kimemsibu? Kulikoni Komandoo? Ya January 2001 yanahusu?
Tutafakari.
Viongozi wakuu SMZ wanaomaliza muda wao mwaka huu 2020 na wapya waliotangazwa kushinda kwenye uchaguzi uliomalizika visiwani Zanzibar yawapasa warudi nyuma kidogo, watafakari kwa kina na kujifunza kutokana na historia ya chaguzi za Zanzibar huko nyuma ambazo ziliambatana na umwagaji damu.
Kama kuna ukweli katika kinachoripotiwa na mitandao ya jamii, viongozi wa vyama vya upinzani na vyombo vya habari vya kimataifa kuhusu mauaji ya raia yaliyotokea/yanatokea huko visiwani then viongozi wanaomaliza muda wao na wapya wote yawapasa warejee mauaji yaliyotokea January 2001 baada ya uchaguzi ambao Amani Karume alitangazwa kuwa mshindi dhidi ya Maalim Seif.
Chama kikuu cha upinzani visiwani humo wakati huo (CUF) kiliyapinga matokeo hayo kwa nguvu zote ikiwemo kuitishwa kwa maandamano ya amani ambayo yalishambuliwa na vyombo vya dola na kusababisha maafa makubwa.
Lilikuwa ni doa kubwa jeusi kwa nchi ya Tanzania, na haishangazi kuona Benjamin Mkapa (apumzike anapostahili) akikiri kukereka na tukio hili miaka takribani 20 baada ya kutokea.
Amani Karume alikuwa rais zao la umwagaji damu huo. Komandoo Salmini Amour alikuwa ndiye rais aliyempa kijiti Karume katikati ya umwagaji damu huo. Mkapa alikuwa ndiye amiri jeshi mkuu.
Baada ya miaka kadhaa ya kutafakari haya yote, Amani Karume alikuja kujirudi na kuomba poo na Maalim Seif na kupelekea uundwaji wa serekali ya mseto iliyojumuisha CCM na CUF.
Hadi kufikia leo, Amani Karume ametokea kuwa ni mmoja wa marais wastaafu wa Zanzibar waliojijengea heshima kubwa si kwa Wazanzibari pekee bali kwa jamii yote ya Watanzania.
Hatutamwongelea Mkapa kwani hatunaye tena.
Komandoo Salmini yupo lakini sina uhakika Watanzania wengi wanajua haswa yuko wapi, anafanya nini na ana hali gani maana hata kwenye hadhara zinazojumuisha viongozi wastaafu wa kitaifa haonekani (au ni nadra kumuona).
Je, Komandoo Salmin Amour yu wapi? Nini kimemsibu? Kulikoni Komandoo? Ya January 2001 yanahusu?
Tutafakari.