Kinyungu
JF-Expert Member
- Apr 6, 2008
- 17,365
- 33,004
JK alikuwa mwanasiasa haswa pamoja na mapungufu yake. Alichokosea ni kutokuona hatari ya huyu aliyemwachia.Muasisi wa Serikali ya Mseto Znz ni Jakaya Mrisho Kikwete
Serikali ya Karume ilikuwa inapinga wazo hilo na hata kwa kejeli Waziri wake maarufu Ali Juma Shamhuna akawa anakebehi anasema anajua Mseto wa Chakula sio wa Serikali
Jakaya akaitisha kikao cha NEC kikafanyika Butiama 2009 akaingiza na kuipitisha kibabe hoja ya Serikali ya Mseto Znz kina Karume wakatoka vichwa chini na kwa kuwakomesha mahafidhina akampitisha Mpemba kwa mara ya kwanza
BTW Pohamba ningependa kusikia commen yako kuhusu utawala uliopita wa Shein? Alikuwa at peace na Wazanzibar wote kweli au naye wanamchukulia kama Komandoo Salmin?