Alshabab walifanikiwa kuondoka

Alshabab walifanikiwa kuondoka

Status
Not open for further replies.
UDHAIFU WA JESHI LA KENYA.
1.Hawakua na mawasiliano, na mtu wa kuongoza operesheni.

Walibeba silaha kubwa hawakuzingatia uwepesi wa silaha na ufanisi wake wakati wa kazi, ni ngumu komando kujipinda kuruka sarakasi akiwa kajitwisha mbunduki mkuubwaaa.

Wengine hawakua na sare, alievaa traksuti sawa, mwenye shati na suruali haya, mwenye kaunda suti na mokasini pia. Hii imepelekea ndani ya jengo kupigana wao kwa wao mana kwa tukio kama hili mtu akijitokrza tu mbele yako kashika silaha basi hujiulizi mara mbili ni kumuwahi tu kwa kiwewe.

Nje ya jengo walijipanga hovyo hovyo tu na wengi milio ya risasi ikisikika wanakimbilia mitaroni kujificha, hii imeonyesha ni waoga.

Ndani ya jengo wanajeshi wameonekana wakitupa mabomu ya kurusha kwa mkono kulipua vyumba bila kujali pengine ndani kulikua na mateka walio hai waliojificha.

Iliwachukua siku nne kumaliza tatizo huku effort kubwa ya serikali ni kitaka kuiaminisha dunia kuwa kenya bado ni salama hvyo watalii wasiache kuja,

Je hii ndio sababu walilipua vyumba kwa mabomu??

Je walitaka kumaliza mchezo haraka baada kuonekana kukata tamaa kwa siku nne??

Inasemekana mateka walikua zaidi ya 200 na walio onekana wakiokolewa hawazidi 50 je wengine wako wapi??

Jambo kubwa na la ajabu ni kupeleka vifaru nje wa jengo.

Magaidi kumi tu tena wasiozidi miaka 29 kuwapelekea vifaru??

Hivi vifaru na magaidi tena waliopo mjini ndani ya jengo tena wakiwa na mateka walio hai inakuja kweli??

Wakenya tambueni ulinzi ni technique na mafunzo imara na sio kujua kingereza kama mnavyoonekana kutunanga watanzania humu mitandaoni mitandaoni.

Naamini kabisa kwa vijana wetu ingehitaji makomandoo 10 walioiva sawa sawa kumaliza ile operesheni.

Poleni sana ndugu zetu na nawaambia badala ya kututenga Eac basi ombeni vijana wetu wamipatie mafunzi angalau muwe stable kukabiliana na magaidi ambao tayari wameahidi kuendelea kufanya ugaidi kila watakapo amua.
 
sijateta chochote hapa ila mie nimesema tu sio uungwana wala ustaarabu kutumia neno "wajinga wa kiislamu"ni neno linaloonekana linalochochea na kuleta matabaka hili huwezi kuiona kama ukiwa hujakaa muda mrefu darasani

na ni kweli sikatai kitu walichokifanya ni cha kijinga lakini huwezi kuweka dini yao mbele kwani kila mtu duniani anafanya maovu wao sio watu wa kwanza kuua
wangapi wanaua watu wasio na hatia? polisi hawauwi watu wasio na hatia tukianzia hapa Tanzania?

tena polisi wa kikristo je tuwaaite Wajinga wa Kikristo?

hakuna majambazi yanayovamia watu na kuua ovyo wakiwa ni wakristo

je tuwaite "wapumbavu wa kikristo?"

tukinzingatia Tunu zetu saba sie watanzania hatuwezi kufika kugawanyika hivyo

so nasisitiza kusema sio uungwana, sio uustarabu, sio hekima, kuwaita wenzako "wajinga wa kiislamu"

unless wewe uwe una matatizo upstairs

Usiwe muoga hao ni wajinga waache tu kwani hata kuua Hutumia udini wao kwanza kabla ya kuua sasa dini na jambo wanalolitenda huwezi litofautisha kamwe.... hata ukiwauliza wao hawajitenganishi ila wale wasio na misimamo mikali huwakana na kuwakataa na kuwaita si waislam na uislam hautaki hivyo.... Hata Muislam hawezi mswahilina hawezi kukataa kama Magaidi ni wajinga. Kuwaita wajinga neno wajinga haliwezi leta mtafaruku wowote wala matabaka kwa sababu lina ukweli ndani yake......

Ukisema Wapumbavu wakristo hilo lipo tofauti jamaa kazungumzia Ujinga nadhani neno hilo linatofautiana... Au na wewe unamatatizo kwenye Medula yako... Uoga hata mbinguni hautofika.
 
Wale jamaa walikuwa na Automatic Guns na zilikua na mikanda ya risasi za kutosha tu si unajua tec ya sasa? Watu wanaset tu na mabomu yanayolipuka kwa muda unaotaka kama vile unavyo set arlam ikuamshe muda gani.

Hizi propaganda za mijitu isiyo na chembe ya huruma baada ya kuua watu wakiwemo watoto wasio na hatia.
Useless'
 
Hizi propaganda za mijitu isiyo na chembe ya huruma baada ya kuua watu wakiwemo watoto wasio na hatia.
Useless'

Kipi kinachokufanya ulie namna hiyo? Tunachotaka hapa ni uthibitisho kama kweli Magaidi wote waliuawa "Picha" vinginevyo ni kweli walitoroka na wewe inabidi ufute haya machozi.
 
[UOTE=Mkoroshokigoli;7436912]propaganda ni nini????[/QUOTE]

Ndo hapo sasa hivi kifo nacho kinahitaji propaganda?
 
Lakini hata Al-shabaab wanakiri kenya walitumia sumu kuingia ndani ..kwa maana hiyo wameuawa ..
 
Lkn acheni utani Alshab ni noma
Lkn vile vile na jesh la kenya ni
Dhaifu tena dhaifu hii ni aibu walioiyoiyonesha ktk nchi ya kenya
 
Hakuna asiyepinga ugaidi na wala sifikirii kama kuna binaadamu mwenye akili timamu aliyefurahia yaliyotokea Westgate. Ila kichwa chako kimejaa mavi na chuki dhidi ya Uislam.

umet6a ushauri kizuzu sana wewe.nenda shule ujue kutulia na kuacha papala
 
porojo baada ya Mauaji, wale wajahedeen waliuwawa wote, hakuna mjinga wa Al Shaabab aliyetoka kule!

We ndo unaandika porojo,,,kuna hata Mwili wa Al-Shabaab ulionekana kama waliwaua kweli? Na kwanini wafukuze waandishi wa habari? Askari wa Kenya ndo ma gaidi ilibidi walipue na wawaue raia wao!
 
labda magaidi waliishikisha bunduki midoli ya ndani ya mall ikawa inapambana na askari wa kenya. hahahahaha..............

hakuna mapambano hapo.wale wakenya walitupa risasi hovyo tu bila plan..wakurupukaji.hovyo sana
 
Mkuu humu watu wengi hawafikiri kabisa na kama wanafikiri sina uhakika kama wanatumia ubongo,kwani kulikuwa na majibizano ya risasi na mateka walikuwa wakishikiliwa ndani,sasa mtu unawezaji kufikiri tu eti walitoka wote?Baadhi wangeweza kutoka na raia lakini si wote.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

mkuu bila shaka ww ndo ubongo wako una limit ya kufikiri.hawa watu walitega mabomu na ndo maana hata baada ya president kusema the mall is under their controll still jion milipuko iliendelea kusikika lakin ushikiriwaji wa mateka wale walikuwa kwenye kutake cover ndo maana wengi walikutwa wamejifungia maofifiin na kujificha sio kwamba walikusanywa sehemu moja hapana na ndo maana wanasema kenya waliwauwa raia wao pasipokujua wapo wapi mm naanimini kwa jinsi wakenya wanavyopenda sifa na majigambo hata wangeua mmoja wangeonesha tu maiti kwaiyo yawezekana pia walisepa maana mmoja wao aliwatoka wanajeshi kwa stlye na kuokoa mateka
 
Ndio habari inayowaumiza vichwa wana usalama wa Kenya wakisaidiwa na wale wa kutoka Nje ni kwamba baada ya kufanya lile tukio la Westgate jamaa walifanikiwa kuondoka salama salmin kwa kupitia mtaro wa maji taka ambao umeambaa mita kadhaa kutoka lilipo jengo walimofanya tukio la kufuru

Source"tbc habari sa2

HAPA lazima kuna mchezo umechezwa..kuna haja kwa wakenya kuangalia upande wa pili wa shilingi kuna amasuala ya kujiuliza tena kwa utulivu kwani kama wamechezewa na makachero wa kimarekani ...
  • suala zima lime fichwa na hakuna habari ya maana
  • wale jamaa wameuliwa na kwa mujibu ya habari za kipolisi 5 wameuliwa..sasa sura zao zipo wapi? sura ni muhimu sana kwa public kwani mtu akiina picha anaweza kusaidia kama aliwahi kumwona huyo gaidi
  • kwa nini gorofa ziliangushwa? jee hao magaidi wote walikua kajichumba kimoja
  • jee hawa sio US's alqaeda ? yaani jamii ya alqaeda wa syria wanalipwa na kupata support ya US ? sio jamii hio ? kwani hapa kun achanga la macho....
  • kuna twitter fulani zikitoka ambazo zilionesha ni za alshabab.....lakini ukifuatilia twitter hizo utaona kama hao watu wanazungumza ndani ya westgate ? hii inasgangaza kidogo...
hapa kenya waangalie upande mwengine wa shilingi.....vijana wao wanao kwenda kufundishwa kupambana na ugaidi wanaweza kuwa ndio chanzo wana tumikia mabeberu...kwa US kila kitu kinawezekana kwa lengo maaulum...mimi sijui na wewe hujui lakni wao kutoa mhanga watu wao ni jambo la kawaida......na zaidi ikumbukwe Obama ni mkenya kwa asili na amekua akilegeza kamba ya kupambana na magaidi wa kina bush...juzi tumeona alivo lipeleka suala la syria kwa congress ili lipate baraka...na mpaka sasa syria haijashambuliwa....kuna neo cons hawapendi kuona vita yao inarudi nyuma wanataka iendelee
wanataka zile kambi za mateso zirudi...
wanataka kenya lazima wapitishe ile sheria ya ugaidi kuna mambo mengi....
hata kama utaona kuna al shabab wana kubali kuwa hilo wamefanya wao..lakini inawezekana ni kutaka sifa tu baada ya kuona hilo limetokea na kwa fikra zao labda wamefanya vijana wao
kenya fanyeni uchunguzi mpana...

 
Itafahamika, na mimi nashangaa wanadai wamewaua lakini hawaja display sura wala maiti za hao magaidi.
Kuna usiri usioleweka na habari zisizo kamili juu ya hili tukio kwani habari zinazotolewa hazijitoshelezi zina maswali na gaps nyingi
 
Selikali ya Kenya ndio yenye kujua ukweli. Hizi "may have" "inasemekana" haziwezi prove the validity. Kama jamaa walisepa au waliuwawa wao ndio wenye ukweli.
Kama ni kutoroka kupitia mtaro,huo mtaro destination yake ni wapi? Na ni mtaro wa aina gani? Kama walipita forensic inaonyesha vipi? Na waliibukia wapi kwa umbali gani? ukiangalia picha hizo za kusanifu hapo juu utagundua kuwa mtaro ni cylindrical ditch na ni ndefu kwelikweli na hazionyeshi zinaishia wapi? Pia kama walitoka kupitia mtaro huo,mateka wale wa mwisho wa siku ya nne mwishoni walikuwa wanangoja nini kukimbia,coz walikuwa huru watekaji hawakuwepo!!
Pia kama walitoka kama mateka,watuambie walitoka muda gani,kama walitoka ile siku ya kwanza ndani ya dakika zile 30 naweza kubali coz tukio lilionekana kama ni ujambazi wa kawaida,lakini kama walitoka kuanzia siku ya pili kuendelea sitaamini kwani mateka wote walikuwa wanadakwa ima na wanajeshi wenyewe na majeruhi walikuwa wakipewa huduma ya kwanza na Red Cross,sifikirii kama mateka baada ya siku ya pili walikuwa wakiachwa kutawanyika hivi hivi.
Tusubiri,uchunguzi ukamilike na selikali iseme inawashikiria kina nani na waliouwawa ni kina nani. Uchunguzi wa tukio hili hauwezi toka kama matokeo ya uchaguzi.
 
HAPA lazima kuna mchezo umechezwa..kuna haja kwa wakenya kuangalia upande wa pili wa shilingi kuna amasuala ya kujiuliza tena kwa utulivu kwani kama wamechezewa na makachero wa kimarekani ...
  • suala zima lime fichwa na hakuna habari ya maana
  • wale jamaa wameuliwa na kwa mujibu ya habari za kipolisi 5 wameuliwa..sasa sura zao zipo wapi? sura ni muhimu sana kwa public kwani mtu akiina picha anaweza kusaidia kama aliwahi kumwona huyo gaidi
  • kwa nini gorofa ziliangushwa? jee hao magaidi wote walikua kajichumba kimoja
  • jee hawa sio US's alqaeda ? yaani jamii ya alqaeda wa syria wanalipwa na kupata support ya US ? sio jamii hio ? kwani hapa kun achanga la macho....
  • kuna twitter fulani zikitoka ambazo zilionesha ni za alshabab.....lakini ukifuatilia twitter hizo utaona kama hao watu wanazungumza ndani ya westgate ? hii inasgangaza kidogo...
hapa kenya waangalie upande mwengine wa shilingi.....vijana wao wanao kwenda kufundishwa kupambana na ugaidi wanaweza kuwa ndio chanzo wana tumikia mabeberu...kwa US kila kitu kinawezekana kwa lengo maaulum...mimi sijui na wewe hujui lakni wao kutoa mhanga watu wao ni jambo la kawaida......na zaidi ikumbukwe Obama ni mkenya kwa asili na amekua akilegeza kamba ya kupambana na magaidi wa kina bush...juzi tumeona alivo lipeleka suala la syria kwa congress ili lipate baraka...na mpaka sasa syria haijashambuliwa....kuna neo cons hawapendi kuona vita yao inarudi nyuma wanataka iendelee
wanataka zile kambi za mateso zirudi...
wanataka kenya lazima wapitishe ile sheria ya ugaidi kuna mambo mengi....
hata kama utaona kuna al shabab wana kubali kuwa hilo wamefanya wao..lakini inawezekana ni kutaka sifa tu baada ya kuona hilo limetokea na kwa fikra zao labda wamefanya vijana wao
kenya fanyeni uchunguzi mpana...


Na ndio maana hapa tunataka tujadili kama ulivyogusia hapo lakini kuna watu sijui wamepakwa ----- gani yani wao na dini dini na wao kifupi hawatoi hata mawazo mapya yote wana copy kutoka ktk vitabuMAJANGA.COM
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom