Wandugu Masanja
JF-Expert Member
- Apr 26, 2008
- 1,584
- 553
wadanganyika wanapenda masimulizi kwa mchezo huu bado nyavu hazionekani
Hivi Hosea ni mtumiaji wa Pombe? na kama ndiyo anapendelea kunywa pombe gani? anakunywa wakati gani wa siku? na je alisema maneno hayo kanywa? hata hivyo kama hakunywa siamini kuwa msukuma anaweza kumchunguza msukuma kwani wasukuma ni watu wanaukabila sana wa chinichini ukitaka kujua nenda Mwanza
Hivi kumbe huyu bwana bado hajafukuzwa kazi!!
Hivi Hosea ni mtumiaji wa Pombe? na kama ndiyo anapendelea kunywa pombe gani? anakunywa wakati gani wa siku? na je alisema maneno hayo kanywa? hata hivyo kama hakunywa siamini kuwa msukuma anaweza kumchunguza msukuma kwani wasukuma ni watu wanaukabila sana wa chinichini ukitaka kujua nenda Mwanza
Tafadhali ndugu, kuwa lump watu wote pamoja siyo vizuri.Ulifanya research gani? Una data gani ku support hichi ki sweeping statement? Nikienda Mwanza nikaangalie nini?
Unapoongea kuhusu reputation ya mtu au watu ni lazima uwe mwangalifu sana.Wsukuma wana "camaraderie" sana miongoni mwao na kwa kila mtu, lakini pia wanajua ku-change vizuri sana inapokuwa appropriate.
Kama una argument ya ukabila wa wasukuma ilete vingine, hiyop hapo juu ni collossal failure.
Tafadhali ndugu, kuwa lump watu wote pamoja siyo vizuri.Ulifanya research gani? Una data gani ku support hichi ki sweeping statement? Nikienda Mwanza nikaangalie nini?
Unapoongea kuhusu reputation ya mtu au watu ni lazima uwe mwangalifu sana.Wsukuma wana "camaraderie" sana miongoni mwao na kwa kila mtu, lakini pia wanajua ku-change vizuri sana inapokuwa appropriate.
Kama una argument ya ukabila wa wasukuma ilete vingine, hiyop hapo juu ni collossal failure.
Huyu Hosea ninyi hamjui mimi namfahamu... akiwa msaidizi wa jaji hapo dar alikuwa anaomba rushwa waziwazi mimi nafikiri wasaidizi wa rais hawajamshauri vizuri katika hili
Kikwete sasa mfukuze Hosea
Tahariri
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
MKUTANO wa Nane wa Taasisi ya Leon Sullivan uliokuwa ukifanyika Arusha umemalizika juzi (Ijumaa), huku ukiacha ujumbe mzito uliotolewa na Rais mstaafu wa Nigeria, Olesegun Obasanjo, kwa Watanzania.
Katika hotuba yake aliyoitoa katika mkutano huo, Obasanjo alisema nchi za Afrika zinakabiliwa na tatizo la rushwa na kuwataka viongozi wakuu wa nchi hizo kuwawajibisha viongozi wote walio chini yao wanaotuhumiwa kwa rushwa na ufisadi.
Sisi tumeuchukulia kwa uzito wa kipekee ujumbe wa Obasanjo, kutokana na vita inayoendelea sasa hapa nchini ya kupambana na ufisadi na rushwa, vita inayoongozwa na Rais Kikwete mwenyewe.
Kwa kutambua uzito wa ujumbe na vita ya rushwa tunayopigana sasa, tunapenda kumkumbusha Rais Kikwete kuwa kama alivyosema Obasanjo, ana kila sababu ya kuanza kuwachukulia hatua viongozi waliokwishatajwa kuhusika na kashfa za rushwa na ufisadi.
Kiongozi wa kwanza anayepaswa kuanza naye ili kuhakikisha mapambano ya sasa yanafanikiwa, ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hosea. Yeye ni miongoni mwa viongozi waliotuhumiwa kuisafisha kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond dhidi ya tuhuma za kupata zabuni hiyo kwa njia zisizostahili.
Hosea ni mmoja wa viongozi wanaoongoza taasisi nyeti, aliyetajwa na katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, iliyoundwa kuchunguza uhalali wa upatikanaji wa zabuni hiyo, inayoligharimu taifa hasara ya mamilioni ya shilingi kila siku, kuwa anapaswa kuachia ngazi kwa kulindanganya taifa katika ripoti yake ya uchunguzi wa upatikanaji wa zabuni hiyo.
Ripoti ya kamati hiyo inabainisha kuwa Hosea alitoa ripoti ya uongo kwa umma wa Watanzania, iliyokuwa ikieleza kutokuwapo kwa aina yoyote ya rushwa au ufisadi katika mchakato wa upatikaji wa zabuni hiyo kwa Kampuni ya Richmond.
Mbali ya Hosea, viongozi wengine waliotajwa kuhusika katika kashfa hiyo ambao wamekwishaachia nyadhifa zao, ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.
Wengine walioachia ngazi sambamba na Lowassa, ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, na aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha.
Kuachia madaraka kwa viongozi hao kulionyesha dhana ya uwajibikaji ilivyoanza kushika kasi hapa nchini, baada ya kipindi kirefu cha viongozi kugoma kuwajibika, hata wanapobainika kufanya makosa ya wazi katika utendaji kazi wao.
Kwa hao waliokwisha kuachia madaraka, tunarudia kusema kuwa wamefanya jambo jema kwa sababu wametimiza wajibu wao na wamefungua milango kwa wengine kufuata nyayo zao, wakibainika kuwa katika mazingira kama hayo yaliyowakuta mawaziri hawa watatu.
Kinachotushangaza ni kitendo cha Hosea tunayeamini kuwa - licha ya kutajwa katika kashfa hii - ni mtu mwenye hekima na anayeheshimu misingi ya uongozi bora, kukataa kuachia ngazi.
Tunapenda kueleza msimamo wetu wazi kuhusu suala hili kuwa Rais Kikwete ana kila sababu ya kumfukuza kazi Hosea, kutokana na kashfa zilizoelekezwa kwake na Kamati Teule ya Bunge, ambazo ushahidi wa mazingira unaonyesha kuwa zina kila chembe ya ukweli.
Tunajua kwamba Hosea hakutarajia kukutana na hali hii, lakini tunamtaka azingatie kauli ya awali ya Rais Kikwete wakati akielezea mazingira yaliyolazimisha kungatuka kwa Edward Lowassa, kuwa kilichotokea kwake (Lowassa) ni ajali ya kisiasa, na ya hivi karibuni ya Obasanjo ya kuwataka viongozi wakuu wa Afrika kuwawajibisha viongozi wanaotuhumiwa kwa rushwa na ufisadi.
Hosea tunasubiri umauzi wa Waziri mkuu, kwenye kushughulikia ripoti ya Mwakyembe, maana alisema ataifanyia kazi in 3 months sijui imebaki muda gani maana kamati ilitkaka na huyu naye afukuzwe kazi mara moja!