All about Edward Hosea, Mwanyika

All about Edward Hosea, Mwanyika

JK hawezi kumfukuza HOSEA kama ameshindwa ku-deal ma MAFISADI wengine walioko CCM. Hosea anajua kila kitu kuanzia EPA, RADA, JET ya RAIS na uchafu mwingine tusioujua. Jk kumfukuza Hosea ni kama vile atakuwa anatangaza vita within their CHAMA. Kweli JK ameshika pabaya kama hayuko makini maana hata Urais wake unahusishwa na huo UCHAFU. Unless amuombe aandike barua ya kujiuzuru kabla huo UPUPU haujamwagwa huko Bungeni. Wenyewe si wanaweza kuambizana kabla ya SOO halijaibuka kama alivyofanya Sitta kwa Lowassa. Kazi iko.
 
Ila twende mbele kurudi Nyuma, Hosea TAKUKURU ni kama JOKA LA KIBISA YAANI HALING'ATI ILA LINALAMBALAMBA.

Kuntakinte umeniua, unakumbushia "Kibisa Dancing Troupe" back in the dayz, youngunz hawajui hayo mambo.

Ila Joka la Kibisa linaweza kuliwajibisha Joka lingine la Kibisa?
 
Pinda alisema anahitaji miezi mitatu, ustaarabu ni kumpa nafikiri bado haijaisha ikiisha then ndio tutamkoma nyani na yeye anajua hilo vizuri sana!
 
Kuntakinte umeniua, unakumbushia "Kibisa Dancing Troupe" back in the dayz, youngunz hawajui hayo mambo.

Ila Joka la Kibisa linaweza kuliwajibisha Joka lingine la Kibisa?

100% True Mkuuu
 
Kikwete sasa mfukuze Hosea


Sisi tumeuchukulia kwa uzito wa kipekee ujumbe wa Obasanjo, kutokana na vita inayoendelea sasa hapa nchini ya kupambana na ufisadi na rushwa, vita inayoongozwa na Rais Kikwete mwenyewe.


Labda mimi sijui ni vita gani hiyo ya kupambana na mafisadi inayoongozwa na JK. kuna kitu kingine anachofanya zaidi ya kuwabembeleza na kuwamwagia masifa pale wanapopata shutuma na kujiuzulu.
 
Mbona wako kimya kama vile hawakutajwa na Ripoti ya Mtu makini Mwakyembe? Waseme Neno au tutawasemea kwa niaba yao wasitufanye sisi Hamnazo!!
 
Hoseah alonga

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah, ameamua kueleza kile kinachousononesha moyo wake.

Akizungumza wiki hii jijini Dar es Salaam, Dk. Hoseah alisema anaumia sana moyoni kutokana na watu wengi kumhusisha na kashfa za ufisadi.

Alibainisha kuwa, kinachouumiza sana moyo wake ni jamii kutompa sifa stahiki kutokana na juhudi anazotumia kupambana na rushwa nchini.

“Mimi nitafaidika nini na ufisadi?” alihoji Dk. Hoseah wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl mapema wiki hii.

“Nasikitika kuwa watu wanaonekana kukata tamaa mapema… lakini wanapaswa kufahamu kuwa kazi hii (ya kupambana na rushwa kubwa) ni ngumu na TAKUKURU ni chombo kinachojijenga hivi sasa,” aliongeza.

Dk. Hoseah alieleza masikitiko yake hayo baada ya kurushiwa swali na Mwenyekiti wa wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), Reginald Mengi, aliyemtaka kueleza taasisi anayoiongoza imefanya nini hadi hivi sasa kukabiliana na rushwa nchini.

Katika maelezo aliyoyatoa kabla hajauliza swali hilo, Mengi alibainisha kuwa wananchi wengi wamepungukiwa na imani na chombo hicho kutokana na masuala mawili.

Kwanza, alisema, wananchi wengi wana shauku kubwa ya kufahamu au kuona kilichofanyika dhidi ya watu wanaotajwa kuhujumu nchi na mafisadi.

Pia, Mengi alisema wananchi wengi hawajui kwa uhakika muda unaotakiwa kwa taasisi kama TAKUKURU, kuchunguza tuhuma za rushwa kubwa na kuchukua hatua.

Kauli hii ya Mengi, bila shaka ni mwendelezo wa malalamiko kutoka katika jamii, ambayo inaonekana kukatishwa tamaa na kasi ndogo ya kuwashughulikia wala rushwa wakubwa na mafisadi nchini.

“Dk. Hoseah, tumekupa imani kwa miaka miwili, tunaamini kuwa sasa ni wakati wa kuona matunda. Tukiona mwaka wa tatu unakatika, utakuwa umetuangusha na kifo chetu kitakuwa cha mende,” alisema Mengi.

Mengi alisema kutokana na shauku hiyo, Watanzania hivi sasa wanatarajia kumuona Dk. Hoseah mpya na akaahidi kuwa MOAT na vyombo vya habari vitampatia ushirikiano wa kumwezesha kuyatekeleza majukumu yake vema.

“Huko nyuma tulikuandika vibaya kwa sababu zile mbili. Sasa tunakupa muda wa kupumua tukisubiri kazi yako,” alisema Mengi na kumuonya kuwa iwapo watu hawataona matunda ya kazi hizo, wanaweza kuanza kumwandika tena vibaya.

Akijibu hayo, Dk. Hoseah alifafanua kuwa kazi ya kupambana na rushwa kubwa, si rahisi kama watu wengi wanavyofikiria.

Aidha, alisema kuwa ni vema kwa taasisi kama TAKUKURU, kuwa na uhakika wa kile inachokifanya, hasa kufikia maamuzi ya kumfikisha mtu mahakamani kwa tuhuma za rushwa kubwa.

Alisema ni aibu kwa TAKUKURU kukurupuka na kumfungulia mtu mashitaka, lakini mahakama ikamwachia kutokana na kutokuwepo kwa ushahidi wa kutosha kumtia hatiani mtu huyo.

Dk. Hoseah alisema utaratibu wa uchunguzi unaondeshwa na taasisi yake unahusisha pia taasisi nyingine, kama vile Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kabla uamuzi wa kuifikisha kesi mahakamani haujafikiwa.

Aidha, Dk. Hoseah alibainisha kuwa sheria inamzuia kutangaza kesi ambazo TAKUKURU inazishughulikia, na hii inaweza kuwa sababu moja ya wananchi kudhani kuwa taasisi hiyo haifanyi lolote kushughulikia rushwa kubwa.

“Lakini sisi TAKUKURU tumejiwekea malengo na kutokana na utendaji tunakamilisha malengo yetu. Kwa mfano, tumejiwekea malengo ya kukamilisha upelelezi wa kesi kumi za rushwa kubwa kila mwaka.

“Ilipofika katikati ya mwaka huu tayari tulikuwa tumekamilisha uchunguzi wa kesi tano na majalada yake tuliyafikisha kwa DPP.

“Baada ya kuyapitia, DPP ameturudishia majalada mawili kwa ajili ya kuyafanyia marekebisho… lengo letu ni kuhakikisha kuwa hadi mwisho wa mwaka tunakamilisha kesi kumi tulizojipangia,” alisema.

Alibainisha kuwa urasimu huu, pamoja na ugumu wa kufuatilia masuala ya rushwa kubwa, ambayo mara nyingi yanahusisha pia tasisi za nje ya nchi, ndivyo vikwazo vinavyowafanya Watanzania wasijue kinachoendelea ndani ya taasisi hiyo.

Lakini aliwataka Watanzania kuwa wavumilivu na kuipatia TAKUKURU ushirikiano kwani kazi inayofanyika ni kubwa na itazaa matunda mazuri.
 
Ukiwa fisadi unakosa mwelekeo kabisa.Unashindwa kujua mema na mabaya.Ndipo alipofikia Hosea.Tanzania sasa tunahitaji Mungu aingilie kati,hali ni mbaya sana na wakuondoka sio yeye tu ni wote!
 
Fisadi hawezi kujichunguza...Nimemwelewa R.Mengi kwasababu ametaja mambo mawili very constructive..Kwamba hakuna kilichofanyika na muda umepita mrefu na hivyo tunataka kuona matunda/matokeo.

Hosea huyo huyo bado amedai aongezewe muda....Hapo unaweza kuona kuwa hakujibu kutokana na maelezo ya mwenyekiti na wasiwasi wa wanajamii.

Yuko out of touch na pia nadhani hawezi kufanya chochote zaidi ya kutaka kuendelea kula jasho la walipa kodi masikini.

Kazi ake yeye ni kukusanya ushahidi..Sasa hata kama ni makampuni ya nje kwenye dunia hii ya utandawazi kweli ni kigezo cha kutuletea?

Kama ni ushahidi hata kaguzi zote za makampuni ya kimataifa si zinatosha?
Si kuna taasisi zenye kuwa finaced na zenye kushirikiana inapokuja kwenye rushwa iliyovuka mipaka?

Hosea anadahni tunaishi kwenye ujamaa bado?

Kama kuna watu waliojitolea kwasababu ya kupambana na rushwa kama wanahabari hao..Na kukabidhi habari zote na ushahidi wa yale wanayoyaandika..Then whats going on?

Huyu Hosea alivyoona kina Kubenea wanashambauliwa alifanya nini?

Ama bado anaona hakuna umuhimu wa kuwafikisha watuhumiwa wote kunakohusika?

Kazi yake yeye si kuona kama ushahidi huo unatosha kuwafungulia mashtaka...Kazi yake yeye ni kuuwasilisha ushaidi huo ambao wengi wetu tunaona unatosha na DPP atafanya kazi yake.

Asijilimbikizie majukumu mengine na kuendelea kuvuta muda huku akila kote kote kutoka kwa wananchi na mafisadi..Anataka kutumia muda huo ili siasa zimfanye asahaulike.
 
Tatizo la ufisadi linaanzia kwenye chama cha mapinduzi. hakiko tayari kuwaadabisha mafisadi eti kinaogopa chama kitachafuka na kitaachwa kupendwa, kwakuwa wanaotajwa katika ufisadi ni makada nguli wa chama hicho.

waige mfano wa chama cha anc cha afrika ya kusini ambacho kinaachia mambo ya ufisadi kwenye vyombo vya sheria! sheria/mahakama ikikuacha huru, cofidence ya jamii inaongezeka. Ufisadi hautakoma nchini kama chama cha mapinduzi kitaendelea na sera yake ya kulindana na kutumia vikao vya chama kumaliza/kufuta tuhuma hizo. waache watuhumiwa wakajisafishe mahakamani.
 
Dr. Hoseah ni Mtu safi..

kwa maana ya kwamba alikuwa amechafuka amejisafisha; kwamba hajawahi kuguswa na uchafu? au kwamba ameuona uchafu lakini hakutaka kuugusa? Au aliushughulikia uchafu pasipo yeye mwenyewe kuchafuka? Nakumbuka mtu mwingine aliwahi kuwa Rais tuliambiwa ni "Msafi" kumbe ni kwa sababu hakuwahi kuwekwa mahali akachafuka!
 
Mtu haitaji degree kuchunguza ni vipi watoto wa vigogo serikalini wanaweza kupelekwa kusoma nje ya nchi wakati mishahara yao inafahamika. Wala huitaji diploma kujua wanaofanya kazi TRA wameweza vipi kujenga majumba au kuwa na magari baada ya kufanya kazi kwa muda mfupi. Huko nyuma anticorruption unit ilikuwa na nguvu sana, ilikuwa ni impossible kwa mtumishi wa serikali kununua hata baiskeli. Siku hizi ni kitu cha kawaida kwa mtumishi wa uma kuwa na nyumba mbili, tatu na magari ya kifahali. Wasitubabaishe hao TOOTHLESS TAKUKURU @#$s
 
He! Hosea anasema kazi ya kupambana na rushwa kubwa ni ngumu, sasa hiyo si ndiyo kazi aliyopewa na yeye kukubali kuifanya? Kama ameshindwa si aseme awekwe mtu mwingine
 
Mimi nadhani watu kama Hosea ni wengi katika mfumo wa serikali. Tunahitaji Watanzania kama wananchi wa Tarime, ili wakatae kuburuzwa hadi vyombo vya dola vikatae kutumika na wanasiasa kama ambayo imeanza kuonekana Tarime, maana ukitumika kisiasa maafa yanatokea.

Mimi naamini pia angalao Hosea ni safi kwa viwango vya Tanzania lakini ili kuonyesha ushujaa na kwa kuwa ana nafasi finyu ya kuendelea kuwapo pale, aamue KUJIUZULU kwa kishindo.

Kabla ya kujiuzulu abebe majalada na nyaraka zote muhimu azihamishe mbali kabisa na ikibidi anitafute na kunikabidhi ndipo atangaze KUJIUZULU na kusema wazi jinsi alivyoshinikizwa kuandika taarifa ya Richmond na baadaye asema alivyoshindwa kuwafikisha mahakamani kina Mkapa, Yona, Mramba, Manji, Mlaki (TIB) na mafisadi wa EPA na amtaje aliyemwambia asipeleke mahakamani.

Hosea pia atuambie ni nani mmiliki wa Kagoda ambaye PCB (si PCCB) walichukua nyaraka zake katika benki kadhaa kabla hata ya wakaguzi kubaini udhaifu wa EPA.

Hosea pia katika Press Conf ya KUJIUZULU atuambie jinsi alivyotaka kumkamata Jeetu Patel mwaka 1997 akakatazwa na Mkapa na badala yake wakaishia kumkamata Baghadad kwa kuwa tu alionekana alitofautiana nao kisiasa wakati wa uchaguzi wa mwaka 1995. Atueleze pia jinsi Baghadad alivyokuja kushinda rufaa baada ya kuingia kwa utawala mpya.

Pia atueleze ni kwanini mpaka sasa hawana ubavu wa kuwashitaki wahusika wa ununuzi wa rada na badala yake wanasubiri SFO ndio wawaamulie.

Hapo Hosea atakuwa shujaa na ataendelea na kazi zake za uwakili kwa amani na pengine anaweza kupata ajira hata nje ya nchi na pengine anaweza kufanya Press Conf kwa waandishi maalumu ambao wataitoa wakati yeye akiwa hewani ndani ya KLM kuelekea apendapo
 
jamani huyu baba anatia huruma!!! anaogopa mpaka macho ya watu. kwa nini asiache kazi? na anajua imenshinda
 
jamani huyu baba anatia huruma!!! anaogopa mpaka macho ya watu. kwa nini asiache kazi? na anajua imenshinda


Anza kujiuzuru wewe,Dr. Hoseah hawezi kujiuzuru kwasababu ya chuki za watu ambao hawana hoja hata kidogo,yeye anaongoza PCCB kwa sheria iliyopo.

Mie nashauri afuatilie Ufisadi uliofanywa viongozi wa CHADEMA katika Ruzuku ya Chama
 

Mie nashauri afuatilie Ufisadi uliofanywa viongozi wa CHADEMA katika Ruzuku ya Chama


Kwa hili la ruzuku nakuunga mkono Mkuu gembe. lakini fukunyua yake aipanue asiangalie Chadema tu, aangalie matumizi ya ruzuku kwenye vyama vyote vha sdiasa. nadhani watanzania tunaliwa sana fedha zetu kupitia ruzuku kwenye vyama. Mimi Nadhani hakuna haja ya kutoa ruzuku kwa ajili ya vyama vya siasa, wanasiasa wanaopenda kuwatumikia wananchi hawahitaji kulipwa
 
Back
Top Bottom