Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Mkuu unakipenda chadema kweli, yaani mwenyekiti alipata zero form 6 unataka na katibu wake awe mtu wa elimu ya hapa na pale??
nani atakayemuongoza mwenzake......umewahi kipofu anamuongoza kipofu mwenzie?!

Kama wewe ni msomi kuliko Lema na Mbowe basi ni majanga kabisa kama siyo ubashite, maana hotuba za Mbowe na hata jinsi ambavyo Lema amawasilisha mada yake, havilingani kabisa na uwasilishaji wako.

Bila shaka wewe hutofautianai na Daudi Albert Bashite.
 
ok...na ya CHADEMA ni ipi? Viwanda si umeona cha dangote na bahresa vinavyopiga kazi? na dangote anajenga kingine cha makaa ya mawe

Wale Chadema umeshamaliza wewe hapo juu kwamba hawana dira na hawajitambui, sasa unataka nini zaidi tena Mkuu???
 
Basi kama huyo Rais wako alikuwa anategemea wananchi ndio tutajenga viwanda atasubiri sana.na wewe endelea kusubiri sisi wananchi tujenge viwanda.kenge wewe huna akili hata moja
Mh mkuu wa nchi yeye kuandaa "paratable & favourable conditions interms of socio,political, economocal dvp for the proper dvp of our industries" wala si vinginevyo mkuu.
 
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)

Mhe. Godbless Lema, kwanza nikupe pole sana kwa kifungo cha miezi 4 bila hatia wala mashtaka. Pole sana.
Hii ndiyo Tanzania ya Magufuli, ni vurugu, ni unyama, ni udikteta, ni uhuni na ubabe uliopitiliza. Haya matukio ni mageni sana masikioni mwa watu wa Tanzania. Sielewi huyu Rais wa CCM A5 anataka Watanzania wafanye nini kwa haya mambo ya ajabu ajabu anayowafanyia Watanzania wenzake kana kwamba ni Makaburu!!

Nelson Mandela(RIP) pamoja na kufungwa na MAKABURU miaka 27 gerezani bado alikuja kuwa Rais wa SA na AKAWASAMEHE MAKABURU WOTE!!. Bado Nelson Mandela alipoanza kutawala nchi ya Afrika Kusini ALIWEZA KUWAACHIA IKULU CHAMA CHA UPINZANI KUKAIMU AKIWA ZIARANI NCHI ZA NJE!!! Je, Magufuli anaweza kufika hata 0.00001% ya UTU na UUNGWANA aliokuwa nao Marehemu Mandela???

Tanzania inapitia kipindi kigumu sana katika Historia tangu kuundwa kwake. Bahati ni kwamba Watz hawakupitia misukosuko ya vita vya kupigania Uhuru ndiyo maana hawana fujo za kijinga kutaka kujibu mapigo. Lakini Rais Magufuli lazima ajue kuwa ameshaanza kubadilisha mwelekeo na upepo kwa Watanzania. Asifikiri Watanzania ni Malaika walioshushwa kutoka Mbinguni. Watz nao ni wanadamu kama wanadamu wengine kama wa nchi za Rwanda, Burundi, Algeria, Misri, Libya, Yugoslavia n.k.
Kuna kitu Rais Magufuli anachokitafuta kwa Watanzania na iko siku inakuja atakipata. Naomba JPM ayakumbuke maneno ya Baba wa Taifa aliyoyatumia wakti wa kumng'oa mkolone bila kutumia bunduki yanayosema,'' TUMEONEWA KIASI CHA KUTOSHA, TUMEPUUZWA KIASI CHA KUTOSHA,TUMENYONYWA KIASI CHA KUTOSHA. UNYONGE WETU NDIO ULIOTUFANYA TUONEWE, TUNYONYWE NA TUPUUZWE, SASA TUNASEMA BASI ''

Magufuli ameamua kuchezea HAKI, UTU na HESHIMA za Watanzania kwa kuamua KUWAONEA, KUWAPUUZA, KUWANYONYA na KUWANYANYASA kisa tu eti wapinzani. Kwanini Magufuli ameamua kuwafanya WATANZANIA WAISHI KAMA WAKIMBIZI NDANI YA NCHI YAO????Hii ni akili ya ajabu sana kuwahi kufanywa na mtu anayejiita Rais wa JMT. Sijajua kwa akili ya Magufuli kama Wapinzani ni maadui,wahaini au magaidi wanaotaka kupindua nchi!! Nchi hii ni ya Watanzania wote bila kujali wako chama gani, wana itikadi gani, wana dini gani, wana Elimu gani au wanatoka kabila gani. Lakini kwa Utawala huu rangi zote za Ubaguzi na Ukabila zimeanza kuonekana waziwazi. Ubaguzi wa kiitikadi/kichama uko wazi(rejea speech zake kwenye Mkutano Mkuu wa CCM juzi na alipoongea na Wabunge wa CCM.Ukija kwenye Ukabila usiseme, kwa sasa kila akitumbua mtu anayemteua ni Msukuma mwenzie. Angalia swala la RC Makonda, pamoja na USHAHIDI WA WATU WA MUNGU KUWA HUYU ALIGHUSHI VYETI MAGUFULI YUKO KIMYA anajifanya kama vile haoni au hayupo. This is double standard. Inasikitisha sana. Nimalize kwa kusema tu kwamba haya yote anayotufanyia Watanzania wawe Wapinzani, wawe Wanachuo waliokosa mikopo, Wafanyakazi ambao hawajapata madai yao kama WAALIMU na MADAKTARI, Watani zangu WAHAYA na TETEMEKO LA ARDHI, Mungu wa Mbinguni anaona huu UTAWALA MWOVU NA IKO SIKU ATAUPATILIZA KATIKA JINA LA YESU KRISTO.

Mwisho ni kuwa Wana CCM tunashauri mwambieni Mwenyekiti wenu na Rais wenu kuwa VISASI HAVIJENGI VIWANDA wala UMOJA WA KITAIFA. Anachofanya kwa sasa ni KUBOMOA NCHI NA KUSAMBARATISHA UMOJA,AMANI, MSHIKAMANO NA UPENDO TULIACHIWA NA WAASISI WA TAIFA HILI. Shame on him!!!
 
Lema...Wakati mwingne mkiwa mnaandika UZI humu muwe mnafikiria mara mbili mbili kabla ya KUANDIKA especially kwa nyie ambao ni VIONGOZI....Mnatakiwa wakati mwingne muwe wa KWELI hili la LISSU kukamtwa leo KAJITENGENEZEA mwenyewe makusudi kuelekea huu UCHAGUZI wa TLS ili ionekane hili la yeye kukamtwa leo lina uhusiano na TLS......hamtaki kabsa kuangalia upande wa pili wa yeye kuvunja SHERIA.....
Siku ukibaki peke yako ndio utaelewa maana kwa sasa bado unajifariji...
 
Kamanda hongera, busara kama hizi ulizonazo ni hazina kwa taifa.
Kamanda hata mimi sipendi kushuhudia udhalimu wa watawala nataka nifungue kesi ya kikatiba mahakamani siku moja ila sijapata mawakili tu.
Godbless J Lema
 
Kamanda nitafurahi siku moja nikikusikia ukiongea kwa undani kilichompata kamanda Ben Saanane..Tafadhali Lema fuatilia hili tumebaki kwenye giza nene,watu hatujui huyu kamanda yupo wapi..tusaidie katika hili kamanda..
 
Wakati mwingine unaweza kumsoma mtu ukashangaa mwenyewe. Mbunge ambaye ndiye mtungaji wa Sheria anaandika vitu kiushabiki kiasi hiki?

Mtu anatengeneza mazingira ili kupata huruma za watu.. huu ni Ujinga kufanywa na Mtu mfano wa Lissu. Kampeni za kipuuzi mfano huu zinakushusha. (Ingawa siuoni huo uimara wako).

HAKUNA DHAMBI MBAYA KAMA KUMSHIRIKISHA MUNGU KWENYE UONGO
 
Zoezi la kutumbukiza karatasi likifanyika kwa haki 2020 matokeo ni aibu kwa fulani! Hata huko kwenye nyumba ndogo hata ikipigwa ndiyo na hapana bado ni aibu!
Kuficha aibu kwenye nyumba ndogo ni kufanya figisu ili asipingwe, hilo limefanyika, Ikitegemewa kuwa kwenye nyumba kubwa rafu za February Zitaokoa jahazi!
 
Lema...Wakati mwingne mkiwa mnaandika UZI humu muwe mnafikiria mara mbili mbili kabla ya KUANDIKA especially kwa nyie ambao ni VIONGOZI....Mnatakiwa wakati mwingne muwe wa KWELI hili la LISSU kukamtwa leo KAJITENGENEZEA mwenyewe makusudi kuelekea huu UCHAGUZI wa TLS ili ionekane hili la yeye kukamtwa leo lina uhusiano na TLS......hamtaki kabsa kuangalia upande wa pili wa yeye kuvunja SHERIA.....
Amevunja sheria ipi tuambie wengine hatujui mkuu
 
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)
Wewe akili yako bado haijakaa sawa. Tuliza kichwa kwanza bwana mdogo.
 
sasa hoja gani unayoizungumzia? kama ni suala la Tundu Lisu kukamatwa ni ujinga wake alipaswa leo awe mahakani kwenye kesi yake mkuu.....Tundu lisu anafanya makusudi ili kutafuta huruma ya wapiga kura kesho kutwa.....kesi yake iko dar anahangaika na kesi ya Dodoma ambayo wakina masha wapo na wanao uwezo wa kuishughulikia
Which is which?-TL ni mjinga au anafanya makusudi? Nafasi yake katika kesi ya Dodoma ni ipi na nafasi ya wakili wake kwenye kesi yake Dar ni ipi? Nauliza haya maswali kwa kuwa umemega kipande kidogo cha hoja nzima ya Lema ukaona alichokiandika hakina maana kwa kuwa TL ni mjinga au anafanya makusudi......Hoja niliyokuwa nazungumzia ni mantiki ya kilichoandikwa na Lema.
 
Back
Top Bottom