Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Aliyetupa Macho asiweze kuona?

I wouldn't argue more...Ni kweli unachosema, unaonekana uko smart sana tu. Mnaopenda kusifiwa kwa kila kitu dawa yenu ni kuwasifia tu.

Unafanya hivyo moyoni ukweli umekuingia na umeamua kuukimbia. Kuikimbia ukweli ni kama kulificha jua lisionekane. Kitu kimoja kaa ufahamu kuwa nafsi zetu hutuambia ukweli muda wote kuliko mtu mwingine yeyote. Usihangaike kujificha wala kukimbia, nhuwezi kuikimbia nafsi yako, ukitulia peke yako itaanza kukuambia ukweli ule akili yako isiyopenda kuusikia
 
Tatizo hamtaki kukubali, yaani mnakuwa kama kazi yenu nyinyi ni kubisha tuuuu....
maana hatuoni jitihada za kuleta maendeleo mliyohaidi zaid ya kushinda mkilalama
na kutoa matamko lukuki kama "devonshire white paper"
 
Viongozi wa vyama vya upinzani muda umefika sasa wa kupanga mikakati na kuimarisha upinzani.
Chama tawala kinawaaribia mikakati kidiplomasia .
msipostuka mtakuta uchaguzi huo na nyie hamjajipanga.
Nafikiria sasa ni wakati muafaka wakuanza kupanga mikakati ya chaguzi zijazo.
Mfano mzuri wa chaguzi zilizopita chama tawala wameshinda vizuri kwasababu ya vyama vya upinzani kujikita kwenye kushughulikia matatizo.
Wananchi wanaopiga kura sio wote wanaweza kuona mnayolalamikia yana impact gani kwa sasa au kwa baadae.
Rudini kimkakati zaidi mrudishe imani zenu kwa wananchi kwa makosa yanayotokea sasa kwenye serikali.
Wawepo wa kuangaika na kesi pia mikakati ya kidplomasia iwepo ili walau msihue upinzani.
Wengine hatuna vyama lakini tunapenda kuona Demokrasia ya kweli inatawala Tz.
Mnyika,Zitto,Lema na wengineo tunakosa mengi mazuri kutoka kwenu badilikeni kutokana na mazingira muokoe jahazi la upinzani.
Mmefanya mengi kipindi cha Comredi Slaa njooni na mikakati ya kidplomasia wakati ndio huu.

Kweli wasihue upinzani, nimeipenda hii
 
sasa nimemuelewa "mtakatifu" yaani kila akikosolewa anaona ni adui kwa utawala wake,hapo ni sawa na kukimbia kivuli chake kwani watanzania wanaelewa kinachoendelea
 
Mfungulie basi thread. Mimi hanihusu na wala simjui. Ni nani kwanza?
Kama humjui Mbowe Aka DJ, aka Shem Mukya, aka Bashitte wa Ihungo basi, mbona unataka afunguliwe thread kwani wewe MA bashite wako wooote huko kwenu umewaanzishia thread ?
 
Hahhahahahahhaahhaha Pole kaka.Mwenye nguvu mpishe.Binadamu anaweakness yake.Nina eneo ambalo hata Lema anaweza kuwish kuwa nusu yangu.

Kwa jinsi alivyo bold enough kutetea anachoamini,I wish ningekuwa na guts kama zake.Sijajishusha,bali nimepa sifa anayostahili.

Kwa upande wa wazazi wangu naomba uwaachie wenyewe,wamenielea katika mazingira mazuri ya kutokubali kuonewa na kiumbe yeyote duniani hapa.Na wamenifundisha mwiko kuabudu mtu,bali sifia panapo hitajika.

Kaka ninajielewa kwa kupitiliza pole sana
hahaha,,,wewe bendera fuata upepo ndio unajielewa? maajabu haya
 
Lema...Wakati mwingne mkiwa mnaandika UZI humu muwe mnafikiria mara mbili mbili kabla ya KUANDIKA especially kwa nyie ambao ni VIONGOZI....Mnatakiwa wakati mwingne muwe wa KWELI hili la LISSU kukamtwa leo KAJITENGENEZEA mwenyewe makusudi kuelekea huu UCHAGUZI wa TLS ili ionekane hili la yeye kukamtwa leo lina uhusiano na TLS......hamtaki kabsa kuangalia upande wa pili wa yeye kuvunja SHERIA.....
Unaweza kuweka ushahidi hapa,au na wewe unahisi tu,ukimsoma vizuri Kibatala utaelewa kwa nini unachosema hakina uwezekano,tahadhari uliyowapa kina Lema mi nzuri lakini kwa hii ishu ya Lissu sio applicable
 
Mkuu alichoandika Lema hakuna faida kwako?
Anadhani yeye anatengwa na madhila yanayotokana na kinachoendelea. Ni aina ya watu wabinafsi wanaodhani wanaweza kudondokewa na makombo ya watawala wanaosigina mfumo wa sheria na usimamizi wa haki. Ni aina ya watu wa kupuuzwa kwa kuwa wako tayari kushangilia maumivu hata ya wazazi wao ili mradi wao wanatarajia makombo. Ni aina ya watu wepesi ambao tayari wameishaambukizwa chuki, sasa wanashangilia pale wenzao wanapokuwa katika mateso. Asichokijua, mwisho wa siku hataepuka mapigo yatakayotokana na dhambi ya roho mbaya na chuki dhidi ya binadamu wenzao. Kwa sasa mpuuze!
 
hahaha,,,wewe bendera fuata upepo ndio unajielewa? maajabu haya

Bendera fuata UPEPO wako Lumumba Umoja wa VIWAVI wa Chama Cha Mauaji.Huko ndiko utakapo wakuta hao unaowafikiria.

Ambao wanadhani Mwenyekiti akinya Barabarani basi sababu ni Mwenyekiti na kwao ZIDUMU fikra za Mwenyekiti basi lazima wapige makofi.
 
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)

Wengine watadhihaki kwa vile tu aliyetoa ujumbe ni Godbless Lema, hivyo kujitia upofu na uziwi kwa ujumbe huo wenye ncha kali ya ukweli!

United we stand, divided we fall. Tanzania yenye neema na usawa kwa wote inawezekana.....lakini ni nje ya CCM tu.
 
Bendera fuata UPEPO wako Lumumba Umoja wa VIWAVI wa Chama Cha Mauaji.Huko ndiko utakapo wakuta hao unaowafikiria.

Ambao wanadhani Mwenyekiti akinya Barabarani basi sababu ni Mwenyekiti na kwao ZIDUMU fikra za Mwenyekiti basi lazima wapige makofi.
nakuonea huruma kwa sababu hujui ulitendalo unahitaji maombi
 
Bendera fuata UPEPO wako Lumumba Umoja wa VIWAVI wa Chama Cha Mauaji.Huko ndiko utakapo wakuta hao unaowafikiria.

Ambao wanadhani Mwenyekiti akinya Barabarani basi sababu ni Mwenyekiti na kwao ZIDUMU fikra za Mwenyekiti basi lazima wapige makofi.
nakuonea huruma kwa sababu hujui ulitendalo unahitaji maombi
 
Kama humjui Mbowe Aka DJ, aka Shem Mukya, aka Bashitte wa Ihungo basi, mbona unataka afunguliwe thread kwani wewe MA bashite wako wooote huko kwenu umewaanzishia thread ?
Usipotoshe kwa lengo la kijifariji: Mbowe ambaye ni Freeman Aikael Mbowe alihitimu kidato cha sita Ihungo kama ulivyoandika, na akapata divisheni zero (ambayo umeibatiza kuwa "Bashite"). Na baada ya hapo aliendelea na masomo yake kwa kusafisha hiyo divisheni zero na baadaye kufanya shahada na yuko vizuri kielimu. Na uelewe kupata divisheni zero sio tatizo kwa kuwa hiyo wakati mwingine huwa haimaanishi kuwa mhusika hana uwezo wa kiakili, bali pengine hutokana na sababu mbalimbali. hata hivyo, wapo watu ambao wanapata zero kwa sababu ya uelewa wao kuwa mdogo.

Ndugu yako unayetaka kumfariji hapa, yaani Bashite: Yeye hajagusa kidato cha tano wala cha sita. Alipata divisheni zero kidato cha nne baada ya kuwa anafeli mitihani akiwa shule ya msingi. Darasa la saba alifeli na hata hapo Pamba sekondari alisoma "evening class", hakujiunga kwa kufaulu. Kwa hiyo alipomaliza kidato cha nne hakuwa na cheti kwa kuwa alizungusha. Hadi hapo kama nilivyotangulia kusema hakuna tatizo kwa kuwa angeweza pengine ku resit akafaulu. Alichofanya, ni kutumia njia ya mkato lakini ambayo ni uhalifu (criminal offence), akatumia cheti cha mtu mwingine ambaye ni Paul kujiunga na chuo cha uvuvi Nyegezi kwa masomo ya kiwango cha cheti na kuendelea hivyo hivyo mpaka alipokuja "kuzawadiwa" ukuu wa wilaya.

Kwa hiyo unapofanya reference, usijaribu kumwonyesha Bashite kuwa tatizo lake ni kupata divisheni zero. Fanya reference kwake kama mtu mtuhumiwa wa uhalifu ambaye muda huu unapojaribu kufifisha makali ya "tuhuma dhidi yake" kwa kumfananisha na Mbowe, anastahili kuwa mahabusu ya Keko kama ilivyo kwa watuhumiwa wengine!
 
Usipotoshe kwa lengo la kijifariji: Mbowe ambaye ni Freeman Aikael Mbowe alihitimu kidato cha sita Ihungo kama ulivyoandika, na akapata divisheni zero (ambayo umeibatiza kuwa "Bashite"). Na baada ya hapo aliendelea na masomo yake kwa kusafisha hiyo divisheni zero na baadaye kufanya shahada na yuko vizuri kielimu. Na uelewe kupata divisheni zero sio tatizo kwa kuwa hiyo wakati mwingine huwa haimaanishi kuwa mhusika hana uwezo wa kiakili, bali pengine hutokana na sababu mbalimbali. hata hivyo, wapo watu ambao wanapata zero kwa sababu ya uelewa wao kuwa mdogo.

Ndugu yako unayetaka kumfariji hapa, yaani Bashite: Yeye hajagusa kidato cha tano wala cha sita. Alipata divisheni zero kidato cha nne baada ya kuwa anafeli mitihani akiwa shule ya msingi. Darasa la saba alifeli na hata hapo Pamba sekondari alisoma "evening class", hakujiunga kwa kufaulu. Kwa hiyo alipomaliza kidato cha nne hakuwa na cheti kwa kuwa alizungusha. Hadi hapo kama nilivyotangulia kusema hakuna tatizo kwa kuwa angeweza pengine ku resit akafaulu. Alichofanya, ni kutumia njia ya mkato lakini ambayo ni uhalifu (criminal offence), akatumia cheti cha mtu mwingine ambaye ni Paul kujiunga na chuo cha uvuvi Nyegezi kwa masomo ya kiwango cha cheti na kuendelea hivyo hivyo mpaka alipokuja "kuzawadiwa" ukuu wa wilaya.

Kwa hiyo unapofanya reference, usijaribu kumwonyesha Bashite kuwa tatizo lake ni kupata divisheni zero. Fanya reference kwake kama mtu mtuhumiwa wa uhalifu ambaye muda huu unapojaribu kufifisha makali ya "tuhuma dhidi yake" kwa kumfananisha na Mbowe, anastahili kuwa mahabusu ya Keko kama ilivyo kwa watuhumiwa wengine!

Unaielewesha mijitu yenye akili kama BASHITE,haielewi,sijui ikoje hii mijitu
 
Unayehitaji Maombi ni wewe kila baya unapigia makofi,huoni tofauti ya utumbo na uongozi
mimi sijaona baya lolote hakuna vita watu wanafanya shughuli zao kama kawaida tatizo CHADEMA mnapenda umbea sana si mtafute kazi halali ya kufanya kuliko hii ya umbea umbea?
 
Back
Top Bottom