Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Lema...Wakati mwingne mkiwa mnaandika UZI humu muwe mnafikiria mara mbili mbili kabla ya KUANDIKA especially kwa nyie ambao ni VIONGOZI....Mnatakiwa wakati mwingne muwe wa KWELI hili la LISSU kukamtwa leo KAJITENGENEZEA mwenyewe makusudi kuelekea huu UCHAGUZI wa TLS ili ionekane hili la yeye kukamtwa leo lina uhusiano na TLS......hamtaki kabsa kuangalia upande wa pili wa yeye kuvunja SHERIA.....


Mkuu kukamatwa kwa TL kulishapangwa tangu Muda, Nia yao asiwepo kwenye ule Uchaguzi.

Rejea pale alipokamatwa alipokuwa Mahakamani.
 
Matamko koko na kushinda mahakamani haviwasaidii wapiga kura wenu

Mngemwambia Mwenyekiti wako kwanza kwamba kwa kupeleka wapinzani mahakamani kila siku hakuongezi viwanda
 
Ndo kaz iliyobaki kwa sasa
Kukamata,kuingilia mihimili ya mahakama, wakuu wa mikoa kujifanya miungu watu, na wenye nchi waliopewa dhamana ya kuongoza nchi wanafuatilia SHILAWADU
 
Mikwara mbuzi tu mnamhusisha Mungu kwenye upuuzi wenu mkiwa majukwaani mnatukana wenzenu Mungu anapenda? Awamu hii ni jino kwa jino fanya upuuzi wenzio wafanye upumbavu
Jino kwa jino ndo unavyopenda iwe? Ukweli hauna maficho ya kudumu na ukiufahamu utakuweka huru: Hili nalo kitapita. Hatimaye siku moja haki itatamalaki. Aliyopitia Lema, Lijualikali na udhalimu anaofanyiwa TAL, ndiyo garama ya amani ya kweli (ambayo ni tunda la haki) inayotafutwa usiku na mchana.

Pole Mh Lema, Mh Lijualikali. Mh Lisu tumuombee sana na kwa imani Mungu ataingilia kati na haki itatamalaki.

Udhalimu una mwisho na mwisho wake uko karibu kuliko ilivykuwa jana!
 
Lema Machinga Complex uliotuahidi kipindi cha uchaguzi hapa Arusha iko wapi?
Nakushauri fungua thread yako ukiwa na hoja zilizokwenda shule na ushahidi wa mkutani wa lini alifanya na kuahidi hayo na maneno hasa gan alisema ikiwezekana unukuu na maneno aliyosema na faida ambazo zitapatikana kujenga hio machinga complex.
Ukishafanya hivo naamin ujumbe utafika sawia. Ukiona kimya basi nenda ofisini kwake kaombe appointment nae namin atakusikiliza.
 
Mikwara mbuzi tu mnamhusisha Mungu kwenye upuuzi wenu mkiwa majukwaani mnatukana wenzenu Mungu anapenda? Awamu hii ni jino kwa jino fanya upuuzi wenzio wafanye upumbavu
Komoa adui yako ili kuangamiza mawazo mbadala ili uishi kwa raha milele
 
Hivi mh.Mbowe kwaninj huyu hukumpa ukatibu mkuu wa chama?

Nani? Lema?
Hapana! na sababu kubwa ni kaskazini
Wapo wengi kanda zingine wenye uwezo mkubwa tu
Yupo Wenje ama Lwakatare ziwa
Yupo Msigwa kanda ya Nyanda za juu kusini
Yupo Lissu Kanda ya Kati
Wapo wengi tu na sio kujazana kaskazini tupu kwenye nafasi nyeti za chama.
 
Lema Machinga Complex uliotuahidi kipindi cha uchaguzi hapa Arusha iko wapi?
Weye ni chinga? Sasa hivi serikali imeruhusu biashara kufanyika kila mahali Kwa chingas bila usumbufu unataka gorofa ili liwe gofu?
 
Asante sana kwa ujumbe Godbless J Lema
Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.
 
Mikwara mbuzi tu mnamhusisha Mungu kwenye upuuzi wenu mkiwa majukwaani mnatukana wenzenu Mungu anapenda? Awamu hii ni jino kwa jino fanya upuuzi wenzio wafanye upumbavu
Majivuni yote haya, eti kwa sababu una mapolisi nyuma yako. Hata Iran wakati wa shaha ilikuwa hivyo hivyo lakini mapinduzi yakafanyika pamoja na kutuma vifaru katikati ya waandamaji. Nyooooooo, ptuuuu.
 
Swali la Msingi La Kujiuliza Ni Hilo .

Huu ni Uchaguzi wa TLS , Figisu Kibao , Vip Uchaguzi Mkuu Ujao. ?

Wabunge na Viongozi Wa Upinzani , mnapaswa kukataa haya katika atua Za Awali .Vuoni uoga na Ingieni Front Kuzikata Dhuluma zinazoendelea , Other wise Impact yake Mtakuja Kuiona Chaguzi ijayo.
 
kamanda Godbless lema mmebaki mtu Mbili ....
1; lema
3; Lissu....

ndio real opposition members
 
Mkuu Lema wakati upo jela MKATA umeme amechukua pesa zetu kaenda kujenga kwao....likiwanja la midege likuuubwa wakati hakuna hata chiriku anayeenda huko kwao...

Braza Lema....wakati upo Jela wenzako uliowaacha walishindwa hata kuusema huo ufisadi...Lema braza,tunakuomba hili pia uliangalie

Halina tofauti na lile likiwanja la dictator Mobutu

President Mobutu's ruined jungle paradise, Gbadolite - in pictures
 
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)
Mh Lema anzisha michango ya tuweze kuwawezesha mawakili watende kazi ya Mungu. Weka mpesa, togo pesa etc. Work on that!
 
Hivi mh.Mbowe kwaninj huyu hukumpa ukatibu mkuu wa chama?
Mkuu unakipenda chadema kweli, yaani mwenyekiti alipata zero form 6 unataka na katibu wake awe mtu wa elimu ya hapa na pale??
nani atakayemuongoza mwenzake......umewahi kipofu anamuongoza kipofu mwenzie?!
 
Back
Top Bottom