Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Aliyetupa Macho asiweze kuona?

Mh naomba kutoa maoni yangu...Wakati campaigns za mitandaoni ziliendelea,nilikuwa nashauri watu wajikite vijijini kupiga campaigns,kama issue ni pesa,wananchi tuko tayari kuchangia,ili mradi tu kampeni zifanikiwe (ikiwezekana nyumba kwa nyumba)tukiamsha ari ya watu kukichukia chama tawala,tunaweza kufanikiwa kuleta mabadiliko mbeleni,

Japo kwa muono wangu,2020 Lowassa agombee tena coz mkifanya kosa mkamuweka mtu mwingine tofauti na Lowassa,huyo mtu hata kama ana nguvu kiasi gani akiukosa urais hiyo 2020 atakuwa amekufa kisiasa...nashauri mkae mezani na ZZK muwe kitu kimoja then by 2025 tumtumie kama hazina kwenye uchaguzi mkuu...

My point here ni kuhakikisha angalau mwaka 2020 idadi ya wabunge wa CCM na Upinzani either inakuwa sawa au Upinzani wanakuwa wengi,hii itasaidia kurudisha hadhi ya bunge kwa kulifanya kuwa muhimili wa dola unaojitegemea tofauti na hali ilivyo sasa
Nakubaliana na wewe lakini nafikiri nafasi ya uraisi kwa tume hii na katiba hii ni ngumu nadhani idadi ya wabunge toka upinzani inabidi ipiganiwe kwa nguvu iongozeke halafu ndani ya bunge tunaweza kurekebisha mengi ikiwamo katiba na tume.
 
I wish ningekuwa japo nusu kama wewe.
Wewe ni aibu kwa wazazi wako hapa duniani, tena usije ukakuta ni dume zima unajishusha thamani namna hii
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)
 
Mkuu unakipenda chadema kweli, yaani mwenyekiti alipata zero form 6 unataka na katibu wake awe mtu wa elimu ya hapa na pale??
nani atakayemuongoza mwenzake......umewahi kipofu anamuongoza kipofu mwenzie?!

cheti cha form 4 ndio kipimo cha six hata kama ni ziro poa tu....hivi anacho au anatembelea nyota ya mwingine.....
 
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)
Î
Godbless unaandika mengi unaishia kujichanganya, naamini unafahamu unajichanganya ila kwa vile unawajua wajinga unaowaandikia ambao watakipenda na kukishangilia ulichoandika umeamua uandike hivyo hivyo kwani unawadharau. Kama unasema hiyo hali iliyopo ni mpango wa Mungu kama ilivyokuwa kusulubiwa kwake Yesu kwa nini tena utake watu walaani? Unataka watu walaani mipango ya Mungu? Kama uliandika pasipo kufahamu basi ujinga huo haumithiliki
 
Mikwara mbuzi tu mnamhusisha Mungu kwenye upuuzi wenu mkiwa majukwaani mnatukana wenzenu Mungu anapenda? Awamu hii ni jino kwa jino fanya upuuzi wenzio wafanye upumbavu
Ni nguvu ni kitambo tu, hata yeye atapita. Afanye jino kwa jino au jicho kwa jicho au chuma kwa chuma vyote vinapita tena vinapita haraka kuliko unavyoweza kudhani. Huyo unayemshabikia inamfaidia nini kutweza utu wa watu? Na je wewe unafaidika nini unapoona mwingine anateseka kwa sababu ya kuwa na maoni tofauti na watawala? Je unashangilia kwa sababu hujapatwa na hayo yanayowapata akina Lissu? Je una jihisi uko salama sana kwa kuhisi wewe si kama wao? Hata kama wewe kazi yako ni kusifu tu ipo siku utaumia kwa kuchelewa kutoa sifa kwa unaowasifu. Jifunze kulia na waliao na kufurahi na wanaofurahi.
 
Hakika LEMA wewe ni great thinker,wewe ni mwana-falsafa na wewe pia ni mwandishi mahiri.Kwenye hii vita tunawaunga mkono,mnatusaidia tusio na sauti.Ila wito wangu kwako ni mmoja tu;kamnongoneze MBOWE mwambie katibu mkuu wa Chadema yaani MASHINJI hatufai kwenye safari hii ya kuelekea kwenye ufalme.Chadema ni chama kikubwa sana,kwa sasa tunamtaka katibu mkuu asiyeogopa jela ili aweze kupambana vita ya kutuvusha dhidi ya huyu mtukufu.Kama chadema mtaamua kwenda na huyu katibu mkuu wa sasa hadi 2020 msijisumbue na msije kutafuta mchawi wa kushindwa kwenu kwakuwa ninyi ndiyo mtakuwa mnatusaliti.
 
Yaani Nimepata hasira hadi nimempiga boss kibao na hajanikosea
 
Pole sana mwambie Mwenyekiti wako hatajenga kiwanda hata kimoja kwa njia anayopita.
Angalau ungekuwa basi unavifahamu hivyo viwanda ili usipoviona ujue havipo, sasa hata kuvifahamu hauvifahamu utajuaje kama havipo hata kama Visipokuwepo? Au utamsubiri yule mshamba atoke jela aje akwambie kama vipo au havipo? Ama nchi mbaya lakini kutusomesha kwake ndio kumetuleta mjini wengi
 
Huu ni utawala uliojaa uovu, mwisho wa utawala huu muovu hauko mbali
Utawala uliopita mlikuwa waovu nyie..mkatukana sana tu..mkabeza sana na Bado mkakaribishwa juice..hakuna aliyesema mungu anawaona wala katupa masikio..utawala huu mmebanwa kwa kutotii mamlaka mnaanza kulalamika..mbona wenzenu walitulia tuli???!!jifunzeni kuvumilia ingawa hamna la kufanya na mkileta jeuri mtaumia nawaambia..wabunge wenzenu waliotulia wanahudumia wananchi sasa hivi..
 
siku hizi Lema anajifungia chumbani kwake na kutuma post huku Jf....kiherehere cha maandamano na vurugu chote kwisha

Mkuu, you are being coward. Hata uhuru wa wewe kuja kuandika haya maneno hapa haujaletwa na haulindwi na watu waoga kama wewe. Ni hao unaowaita "viherehere" ndio wanaopigania kuulinda kwa gharama na mateso makubwa. Mifano unayo. Ifike mahali tujitambue.
 
Watanzania hata haki zao hawazijui,watajuaje kuwa zinavunjwa?
Ni pale taifa litakapokuwa na wachache lakini powerful and influential kama Lissu,ndipo wengi watajifunza kupitia hao,ndio sababu watawala wanajitahidi kuwakandamiza hao wachache,ili kuzuia fursa ya wao kuelimisha na kuamsha walio wengi ambao watawala hawataweza kushindana nao.
Hivyo msikate tamaa mlio wachache,hakikisheni taa yenu haizimiki,ipo siku wengi watamiliki taa na kila kitu kitaonekana wazi,siku ambayo we will call a spade, a spade.
 
Wewe ni aibu kwa wazazi wako hapa duniani, tena usije ukakuta ni dume zima unajishusha thamani namna hii

Hahhahahahahhaahhaha Pole kaka.Mwenye nguvu mpishe.Binadamu anaweakness yake.Nina eneo ambalo hata Lema anaweza kuwish kuwa nusu yangu.

Kwa jinsi alivyo bold enough kutetea anachoamini,I wish ningekuwa na guts kama zake.Sijajishusha,bali nimepa sifa anayostahili.

Kwa upande wa wazazi wangu naomba uwaachie wenyewe,wamenielea katika mazingira mazuri ya kutokubali kuonewa na kiumbe yeyote duniani hapa.Na wamenifundisha mwiko kuabudu mtu,bali sifia panapo hitajika.

Kaka ninajielewa kwa kupitiliza pole sana
 
Mh Lissu amekamatwa leo na yuko njiani analetwa Dar es salaam . Hatupaswi kuogopa , kwani aliyetupa masikio asiweze kusikia kilio na maombi yetu na dua kweli ? Aliyetupa macho mnafikiri haoni ? Aliyetupa akili na fikra asiweze kuwaza juu ya mambo haya ? Tunawakati mgumu katika kazi zetu za siasa kwa sasa , lakini ni wakati muhimu kuliko wakati wowote katika historia ya mfumo wa vyama vingi , ni tabu ya kutembea kwa miguu ndiyo iliyosababisha ugunduzi wa gari , ni giza ndio kilikuwa chanzo cha ugunduzi wa umeme duniani , na tabu ya kuvaa magome ya miti ndiyo iliyoleta mapinduzi ya nguo tunazovaa Duniani leo .

Tunahitaji wakati kama huu katika mahitaji yetu ya mabadiliko , wala msiingie hofu , kwa wale wakristo mnaelewa shetani asingempleka Yesu msalabani mpango wa Mungu kwenu usingetimia , tunapita katika mateso na huzuni kwa maana kubwa katika ustawi na historia ya Nchi yetu ,kila mmoja wetu anapaswa kuona kinachoendelea na kuchukua hatua ya kulaani na kulaumu na kuomba , hata hivyo baada ya giza nene asubuhi utokea.
Msiogope Mungu amekusudia mema kwetu na kwenu .

Aluta continua , Uchaguzi mkuu wa Nchi utakuaje kama leo uchaguzi wa TLS huna vikwazo hivi ? Sio Lissu aliyekamatwa na kuanza kuletwa Dar , bali ni haki , utu ndio vimekamatwa , na wewe na mimi ni ndugu wa haki na utu wa karibu , ni sote tumekamatwa . Amkeni , dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga.

Mungu awabariki .

Godbless J Lema ( MB)
Napata shida sana kujua m uwezo wa kujenga hoja kwa wapinzan wa TZ. Nkisema CCM itaendelea kuwa chama pendwa kwa WaTZ walio wengi ntakuwa sijakosea kabisa.
 
Angalau ungekuwa basi unavifahamu hivyo viwanda ili usipoviona ujue havipo, sasa hata kuvifahamu hauvifahamu utajuaje kama havipo hata kama Visipokuwepo? Au utamsubiri yule mshamba atoke jela aje akwambie kama vipo au havipo? Ama nchi mbaya lakini kutusomesha kwake ndio kumetuleta mjini wengi

Kwa sababu hivyo viwanda havipo na usitegemee vitakuwepo.Mnakubali kupiga makofi tu,hao akina Diamond ndiyo wakwepa kodi wakubwa wakishirikiana na Mkuu wa Mkoa aka Bashite na GSM.

Halafu kutwa mko na akina Mbowe
 
Mh naomba kutoa maoni yangu...Wakati campaigns za mitandaoni ziliendelea,nilikuwa nashauri watu wajikite vijijini kupiga campaigns,kama issue ni pesa,wananchi tuko tayari kuchangia,ili mradi tu kampeni zifanikiwe (ikiwezekana nyumba kwa nyumba)tukiamsha ari ya watu kukichukia chama tawala,tunaweza kufanikiwa kuleta mabadiliko mbeleni,

Japo kwa muono wangu,2020 Lowassa agombee tena coz mkifanya kosa mkamuweka mtu mwingine tofauti na Lowassa,huyo mtu hata kama ana nguvu kiasi gani akiukosa urais hiyo 2020 atakuwa amekufa kisiasa...nashauri mkae mezani na ZZK muwe kitu kimoja then by 2025 tumtumie kama hazina kwenye uchaguzi mkuu...

My point here ni kuhakikisha angalau mwaka 2020 idadi ya wabunge wa CCM na Upinzani either inakuwa sawa au Upinzani wanakuwa wengi,hii itasaidia kurudisha hadhi ya bunge kwa kulifanya kuwa muhimili wa dola unaojitegemea tofauti na hali ilivyo sasa
Wajikite vijijini kupiga kampeni kwani tupo katika uchaguzi????

Yaelekea mnafanya haya yote kama mnafanya kampeni....wahimizenu wananchi kulima huu ndio msimu wa mvua msiwavuruge badae mkaanza kuililia Serikali kuwa haitaki kuwapa wananchi wake chakula...
 
Back
Top Bottom