Aliyemdanganya Rais kwamba kuna waliofungwa kwenye kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe akamatwe haraka

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,746
218,335

Ni dhahiri sasa kwamba Mh Rais alidanganywa na kuambiwa mambo ya uongo , kwamba kabla ya kukamatwa Mbowe alikimbilia nje ya Nchi baada ya kupata taarifa kuwa miongoni mwa watuhumiwa kwenye kesi hii wamekwishahukumiwa kifungo jela baada ya kukiri makosa yao ya Ugaidi .

Mh Rais alitoa kauli hii hadharani tena kwa kujiamini kabisa , Alipokuwa anahojiwa na BBC ambalo ni shirika la Utangazaji la kimataifa, maana yake ni kwamba habari yake hiyo ilisikika Duniani mote .

Bali sasa ni dhahiri shahili kwamba kauli ile haikuwa ya kweli baada ya Mpelelezi Mkuu na nguli wa kesi hii mwenye uzoefu wa miaka zaidi ya 20 kwenye kitengo hicho , aliyesomea Botswana , Inspector Tumaini Swilla kukanusha jambo hilo Mahakamani mbele ya Mtukufu Jaji Tiganga , Swilla akijibu swali la Wakili wa Utetezi Kibatala , ameiambia mahakama kwamba Watuhumiwa wa Ugaidi wako wanne na ni ambao wameshitakiwa Mahakamani na wala hakuna mwingine yoyote aliyefungwa miongoni mwao .

Kwa kufupisha : Ni nani alimdanganya Mh Rais kuhusu jambo hili kiasi cha kumdhalilisha mbele ya jamii ? je anastahili kuendelea kubaki ofisini , na kwanini asikamatwe na kushitakiwa kwa kumdanganya Rais?


1644919783993.png


Pia, soma: Rais Samia: Mashtaka dhidi ya Mbowe sidhani kama yamechochewa kisiasa
 
Basi tu lakini hizi nchi za kiafrika raia huwa wanaonekana hamnazo inasikitisha sana, tuliambiwa kuna ushahidi mzito mara Mbowe alikimbilia dubai mara kuan watu washahukumiwa tayari, dah jamani

View attachment 2120086
Kwa nchi za wenzetu yangeandaliwa maandamano ya kumg'oa kwa kutoa taarifa za uongo na kuingilia uhuru wa mahakama, hii ilikuwa kashifa kubwa sn kwa mhimili moja
 
Kosa moja la Rais wa nchi ni hatari sana.
Sema Mama atachukulia powa kwa vile ana mgwaya Siro.
Kama alisha agiza kesi za mchongo zifutwe lakini Siro bado hatii amri ya Mh. Rais tusemeje?
Na bila shaka ndie alie mlisha Mh. Rais matango pori. Na bado yupo yupo sana ofisini. Ze Igp Siro
soma post#13
 
Uongo huwa hauna umri wala Cheo, na ni dhahiri sasa kwamba Mh Rais alidanganywa na kuambiwa mambo ya uongo , kwamba kabla ya kukamatwa Mbowe alikimbilia nje ya Nchi baada ya kupata taarifa kuwa miongoni mwa watuhumiwa kwenye kesi hii wamekwishahukumiwa kifungo jela baada ya kukiri makosa yao ya Ugaidi .


Pia, soma: Rais Samia: Mashtaka dhidi ya Mbowe sidhani kama yamechochewa kisiasa. Natamani kukutana na Wapinzani
Tatizo huyo aliedanganywa nae hakufanya uchunguzi aliropoka tu tena kwenye chombo kikubwa cha habari
 
Back
Top Bottom