Aliyekuwa katibu wa CHADEMA Mara ajiunga CCM

du kumbe na wewe ni mjinga kiasi hiki,jana alikuepo kiwiziwiz akitegemea atapata malupulupu ya kifisadi,ya kule ccm kila kikao wanaongeza saiz za suruali zao,amegundu hakuna ujinga huo karudi kwao,huu ndo muda muafaka wa kumjaji baada ya mambo kumshinda,hata wewe njo ujiunge lakini theory ya Darwan itajidhiilisha weak species zitajiondo zenyewe kwenye system.
ulikuwa unakimbizwa wakati unaandika ?
 
Mkutano umekwisha Licha ya kupitiza muda kama kawiada sijaona rabsha kama zile za Singida hivi majuzi. Walahi hii nchi!!!!sikia hii sasa ya kufungia mkutano....anakwambia ubunge wa Vincent Kiboko Nyerere ni sawa na umekuatana na gari la kulipa mshahara wakati wewe hukufanya kazi na unapewa pesa, lazima utachukua ndio kilichotokea kwa Musoma Mjini. Sasa hapa hii kidogo inatia mashaka na ukomavu wa kisiasa wa ndg sibitari na ilikuwaje akakwaa mamlaka ya juu kiasi hiki katika Mkoa???????
kama unakuwa na mashaka na jinsi gani alivyokuwa na wazifa wa juu ndani ya cdm mimi nao ni mzigo wa misumari 2mewatwisha nyie sisiem.kazi kwenuuu vijana bado tupo mapambano yanaendelea,kufa kwa mkwez si mwisho wa kugema .
 
Kijana anawaza vyeo! Jamaa kajitathmini na kujikuta hana mwelekeo cdm hvo ikabidi ajifungulie mlango kwa kujipendekeza ccm! Namhurumia sana jamaa kwani naona kaingia choo cha kike mwenyewe!
 
Hongera mkuu kwa kujikita ndani ya CDM, chama kikuu cha upinzani.Kama ni kuandamana andamana kwa sana tuKama ni kuvinjari na FFU basi we ndo mwenyeweMatusi na kutotumia akili sana ni kwako wewe kwa kwenda mbeleMwisho wa siku utaishia kuwa korokoroni wa ofisi ya CDM, maana CDM hiyo ina wenyeweSisi wa Chama tawala tunawaachia kazi ya kututolea mafisadi ndani ya chama chetu, so far mmefanya kazi nzuri.Siye wa magamba tumekaa mikono kifuani wakati you do the donkey work for usI will never leave CCM mkuu wakati wewe upoSasa mjanja nani?
nilisema , huwezi kuwa member wa ccm ukawa timamu ! Haiwezekani,kielelezo cha fikra lojo.Kwani kazi za serikali wanauliza kadi za chama ! Ni juha anaeweza kufikiri sawa na wewe.Kazi zenye kuhitaji kadi ni zile za chama chenu .Kazi za umma , hazina vyama. Punguza ujuha kidngo uwe timamu.
 
Huyu sio katibu wa chadema,alishasimamishwa ukatibu kwa kuuza jimbo la musoma vijijini,akishirikiana na katibu wa wilaya aliyepewa pikipiki na mbunge wa sasa wa musoma vijijini,huyu Nyanza alihongwa sh milion moja,kwa milioni moja tu akasaliti harakati za ukombozi wa wanamusoma,vijijini.Baada ya kuhojiwa na kamati kuu ya chadema aliyekuwa mgombe Mike alikiri kushawishiwa na huyo Nyanza Sibiriti...
 
Hapo ndo ninapokumbuka ule usemi kuwa ACHA NGANO NA MAGUGU YAKUE PAMOJA MWISHOWE MAGUGU YATAJITENGA KUTOKA NGANO. kwa hiyo sintastajabu haya maana walikuja wakiwa na interest tofauti ndo maana wanaponeshewa 'mlunguru' wanaotoka kwani hawajafikia level ya 'self realization' ambapo unaweza kusismama kuwatetea wanyonge ila walijiunga upinzani ili watafute njia ya kujitajirisha. Hongera umefanikiwa kupewa pesa lkn kumbuka roho za wanamara walifariki wakitetea haki ya wanyonge.
 
Kumbe jitu lenyewe lilisimamishwa kwa tuhuma za rushwa. Ndio maana kaenda kujiunga na wenzie ccm !
Mchukueni mla rushwa huyo na mkitaka mpeni na ukatibu mkuu .
 
CDM hatutaki watu wenye utapia elimu huku, aende akungane na wenzake wenye kwashiokor za elimu huko magambani. kwa CDM yule ni makapi tu, akafie mbali kama shitambala kwani hana jipya

Mbona mlimpa ukatibu wa mkoa???? nyau waahid
 
Huyu sio katibu wa chadema,alishasimamishwa ukatibu kwa kuuza jimbo la musoma vijijini,akishirikiana na katibu wa wilaya aliyepewa pikipiki na mbunge wa sasa wa musoma vijijini,huyu Nyanza alihongwa sh milion moja,kwa milioni moja tu akasaliti harakati za ukombozi wa wanamusoma,vijijini.Baada ya kuhojiwa na kamati kuu ya chadema aliyekuwa mgombe Mike alikiri kushawishiwa na huyo Nyanza Sibiriti...

Tutajie huyo Katibu unayemjua wewe
 
Breaking News: PIGO CHADEMA MARA

Katibu wa CHADEMA wa Mara Nyanza Sibitari amerejesha kadi rasmi jioni hii katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na aliyekuwa mbunge wa Musoma Mjini Vedasto Manyinyi.

Sibitari aliyeongozana na vijana wengine 126 na bendera na Kadi za CHADEMA anadai kuwa kajiengua CHADEMA kwa sababu zifuatazo:

  • CHADEMA Kuendeshwa kama Taasisi na si chama
  • Kushamiri kwa makundi ndani ya Chama hicho
  • Mgogoro ulioanza toka nyakati za uteuzi wa viti maalumu hadi Ubunge

Anadai alipotea na sasa karudi nyumbani

More UP DATE to follow
Hapo kwenye Blue ukweli mtupu
 
mkono_203.jpg



MBUNGE mteule wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono ameingia katika kashfa ya rushwa ya uchaguzi na huenda akapoteza ubunge, MwanaHALISI limeezwa.

Mkono ametajwa kutoa mlungula kwa mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika jimbo hilo, Michael Makanja ili ampe nafasi ya kupita bila kupingwa.

Taarifa zinasema Makanja amewaeleza viongozi wa Kurugenzi ya Ulinzi na Usalama ya CHADEMA, kwamba alishawishiwa na Mkono kupokea kiasi cha Euro 1,000 ( karibu Sh. 2 milioni) ili kujitoa katika kinyang'anyiro cha ubunge.

Fedha hizo ni sehemu ya mamilioni ya shilingi ambayo Mkono inasemekana aliahidi kumlipa mgombea huyo wa Chadema.
Mara baada ya kupokea kiasi hicho cha fedha, Makanja alitimiza kile alichoita, "makubaliano yake na Mkono."

Katika kufanikisha mkakati huo, Mkono inadaiwa kuwa alisaidiwa na kiongozi mmoja wa ngazi ya juu katika chama hicho (jina tunalo) ili kumshawishi Makanja kujitoa.

"Baada ya Makanja kufika hapa, wanachama walimvamia wakitaka kujua nini kimemsibu. Hapo ndipo mchezo ulipobumburuka," alisema afisa mwandamizi wa ulinzi na usalama wa Chadema, Hemed Sabula.

Alisema Makanja aliwasili katika ofisi za makao makuu ya chama hicho kwa lengo la kukutana na viongozi wakuu wa chama, lakini kabla hajaingia ndani alikutana na kundi la wanachama waliombana aeleze ukweli wa kilichotokea hata akajitoa.

Makanja alijitoa kugombea ubunge katika jimbo hilo, siku mbili baada ya kuteuliwa kuwa mgombea kwa kumuandikia barua msimamizi wa uchaguzi wa jimbo.

"Wanachama wale hawakuridhika na hatua ya kujitoa kwake. Wakataka kumpa kibano, lakini aliokolewa na vijana wangu," alisema Sabula.

Haikuweza kufahamika mara moja, ni kiasi gani cha fedha alichoahidiwa kulipwa na Mkono. Lakini taarifa zinasema, ameahidiwa "donge nono."

Akieleza hatua kwa hatua, Sabula alisema Makanja aliwekwa chini ya ulinzi kwa usalama wake na baadaye kuhojiwa na maofisa wa idara ya ulinzi na usalama ya chama, kabla ya kumkabidhi kwa maofisa wa TAKUKURU.

Katika maelezo yake kwa maofisa hao wa chama, Makanja alikiri kupokea kiasi hicho cha fedha na kuongeza kwamba fedha zilizobaki alikuwa akabidhiwe na kigogo wa chama chake ambaye alikuwa nyuma ya mpango huo.

Aidha, Makanja aliwataja viongozi wawili – katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Sibitari Nyanza na mwenyekiti wa vijana wa mkoa, David Katikiro – kwamba ni wabia katika mpango huo.


Mahojiano kati ya maofisa wa Chadema na Makanja yamerekodiwa kwa njia ya video na kwa andishi lake binafsi; gazeti hili limefanikiwa kupata nakala yake.

Katika andishi lake hilo, Makanja anasema alishawishiwa na viongozi wake hao wawili na kigogo mmoja kuachia jimbo kwa Mkono kwa kile alichodai, "walimtisha kuwa angefukuzwa kazi."

Makanja ni mwalimu kitaaluma, lakini kwa sasa anasoma katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Juhudi za gazeti hili kumpata Mkono ambaye ni mwanasheria, ili kuzungumzia suala hilo zimeshindikana. Simu zake za kiganjani Na. 0774-333333 na 0787-763355 zilikuwa hazipatikani kwa muda mrefu hadi tunakwenda mitamboni.

Hata hivyo, mawasiliano kati ya Makanja na kigogo huyo wa Chadema yanaonyesha kulikuwa na aina fulani ya makubaliano kati ya Mkono na kigogo.

Kwa mfano, ujumbe wa simu ya mkononi uliotumwa kwa kigogo huyo kutoka kwa simu ya Makanja (namba tunaihifadhi) unasema, "Mzee ameshanikatia tiketi ya kwenda Dar. Sasa mhimize amalize kiasi kilichobaki, maana hali yangu kiuchumi si nzuri…."

Mwingine ulisema, "Tumeshamaliza kama tulivyokubaliana." Ujumbe huo ulitumwa tarehe 21 saa 8:21 mchana.

Ujumbe mwingine uliotumwa juzi Jumatatu, mara baada ya Makanja kuingia "mtegoni" ulisema, "Niko makao makuu ya chama. Nimewekwa chini ya ulinzi...."

Akijibu katika namna ya kushtuka, kigogo huyo alijibu, "Wewe nani kakwambia uende huko… Watakuua. Siwezi kuja huko kukutetea...."

Makanja alikuwa miongoni mwa wagombea saba wa upinzani waliojitosa jimboni Musoma Vijijini kushindana na Mkono, lakini katika hali iliyoshtua wengi, wote walijitoa na kumuacha Mkono kupita bila kupingwa.

Mbali na Makanja, mwingine ambaye ameshtua uongozi wa Chadema kwa kuamua kutorudisha fomu, ni Dk. Ben Kapwani, ambaye alikuwa mwenyekiti wa Chadema wa Mkoa wa Iringa.

Kamati Kuu (CC) ya Chadema ilimteua Dk. Kapwani kugombea ubunge katika jimbo la Ismani, mkoani Iringa. Hatua yake ya kutorudisha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi, imesababisha William Lukuvi wa CCM kupita bila kupingwa.

Dk. Kapwani alijiuzulu wadhifa wake siku moja baada ya kuvuja kwa taarifa kuwa sekretarieti ya Chadema ilipanga kumsimamisha uongozi.

Kwa mujibu wa sheria mpya ya gharama za uchaguzi, matendo ya rushwa yanaweza kunyima nafasi ya kugombea mgombea aliyeteuliwa ikiwa mpinzani wake au chama cha siasa watawasilisha malalamiko kwa Msajili wa vyama vya siasa dhidi ya vitendo hivyo.

Taarifa zilizofikia MwanaHALISI zinathibitisha kuwa tayari Chadema kinaandaa malalamiko rasmi kwa Msajili wa vyama vya siasa dhidi ya hatua hiyo ya Mkono.

Sheria mpya ya gharama za uchaguzi inataka Msajili mara atakaporidhika kuhusu malalamiko kumfahamisha Tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) ambayo itamfahamisha katibu mkuu wa chama husika kuwa mgombea wake amepoteza sifa
 
Ball young nimesema huyu Nyanza sio katibu wa chadema tena,alishasimamishwa kwa kula rushwa na kumshawishi mgombea ajitoe,na alifanikiwa kumshawishi mgombe,huo ndio ukweli,,,kama wewe unataka kuamini kuwa Nyanza bado ni katibu wa chadema shauri yako..
 
Breaking News: PIGO CHADEMA MARA

Katibu wa CHADEMA wa Mara Nyanza Sibitari amerejesha kadi rasmi jioni hii katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na aliyekuwa mbunge wa Musoma Mjini Vedasto Manyinyi.

Sibitari aliyeongozana na vijana wengine 126 na bendera na Kadi za CHADEMA anadai kuwa kajiengua CHADEMA kwa sababu zifuatazo:
  • CHADEMA Kuendeshwa kama Taasisi na si chama
  • Kushamiri kwa makundi ndani ya Chama hicho
  • Mgogoro ulioanza toka nyakati za uteuzi wa viti maalumu hadi Ubunge
Anadai alipotea na sasa karudi nyumbani

More UP DATE to follow


MBUNGE mteule wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono ameingia katika kashfa ya rushwa ya uchaguzi na huenda akapoteza ubunge, MwanaHALISI limeezwa.
Mkono ametajwa kutoa mlungula kwa mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika jimbo hilo, Michael Makanja ili ampe nafasi ya kupita bila kupingwa.

Taarifa zinasema Makanja amewaeleza viongozi wa Kurugenzi ya Ulinzi na Usalama ya CHADEMA, kwamba alishawishiwa na Mkono kupokea kiasi cha Euro 1,000 ( karibu Sh. 2 milioni) ili kujitoa katika kinyang'anyiro cha ubunge.
Fedha hizo ni sehemu ya mamilioni ya shilingi ambayo Mkono inasemekana aliahidi kumlipa mgombea huyo wa Chadema.
Mara baada ya kupokea kiasi hicho cha fedha, Makanja alitimiza kile alichoita, "makubaliano yake na Mkono."
Katika kufanikisha mkakati huo, Mkono inadaiwa kuwa alisaidiwa na kiongozi mmoja wa ngazi ya juu katika chama hicho (jina tunalo) ili kumshawishi Makanja kujitoa.

"Baada ya Makanja kufika hapa, wanachama walimvamia wakitaka kujua nini kimemsibu. Hapo ndipo mchezo ulipobumburuka," alisema afisa mwandamizi wa ulinzi na usalama wa Chadema, Hemed Sabula.
Alisema Makanja aliwasili katika ofisi za makao makuu ya chama hicho kwa lengo la kukutana na viongozi wakuu wa chama, lakini kabla hajaingia ndani alikutana na kundi la wanachama waliombana aeleze ukweli wa kilichotokea hata akajitoa.
Makanja alijitoa kugombea ubunge katika jimbo hilo, siku mbili baada ya kuteuliwa kuwa mgombea kwa kumuandikia barua msimamizi wa uchaguzi wa jimbo.
"Wanachama wale hawakuridhika na hatua ya kujitoa kwake. Wakataka kumpa kibano, lakini aliokolewa na vijana wangu," alisema Sabula.
Haikuweza kufahamika mara moja, ni kiasi gani cha fedha alichoahidiwa kulipwa na Mkono. Lakini taarifa zinasema, ameahidiwa "donge nono."
Akieleza hatua kwa hatua, Sabula alisema Makanja aliwekwa chini ya ulinzi kwa usalama wake na baadaye kuhojiwa na maofisa wa idara ya ulinzi na usalama ya chama, kabla ya kumkabidhi kwa maofisa wa TAKUKURU.
Katika maelezo yake kwa maofisa hao wa chama, Makanja alikiri kupokea kiasi hicho cha fedha na kuongeza kwamba fedha zilizobaki alikuwa akabidhiwe na kigogo wa chama chake ambaye alikuwa nyuma ya mpango huo.
Aidha, Makanja aliwataja viongozi wawili – katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Sibitari Nyanza na mwenyekiti wa vijana wa mkoa, David Katikiro – kwamba ni wabia katika mpango huo.

Mahojiano kati ya maofisa wa Chadema na Makanja yamerekodiwa kwa njia ya video na kwa andishi lake binafsi; gazeti hili limefanikiwa kupata nakala yake.
Katika andishi lake hilo, Makanja anasema alishawishiwa na viongozi wake hao wawili na kigogo mmoja kuachia jimbo kwa Mkono kwa kile alichodai, "walimtisha kuwa angefukuzwa kazi."
Makanja ni mwalimu kitaaluma, lakini kwa sasa anasoma katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Juhudi za gazeti hili kumpata Mkono ambaye ni mwanasheria, ili kuzungumzia suala hilo zimeshindikana. Simu zake za kiganjani Na. 0774-333333 na 0787-763355 zilikuwa hazipatikani kwa muda mrefu hadi tunakwenda mitamboni.
Hata hivyo, mawasiliano kati ya Makanja na kigogo huyo wa Chadema yanaonyesha kulikuwa na aina fulani ya makubaliano kati ya Mkono na kigogo.

Kwa mfano, ujumbe wa simu ya mkononi uliotumwa kwa kigogo huyo kutoka kwa simu ya Makanja (namba tunaihifadhi) unasema, "Mzee ameshanikatia tiketi ya kwenda Dar. Sasa mhimize amalize kiasi kilichobaki, maana hali yangu kiuchumi si nzuri…."
Mwingine ulisema, "Tumeshamaliza kama tulivyokubaliana." Ujumbe huo ulitumwa tarehe 21 saa 8:21 mchana.
Ujumbe mwingine uliotumwa juzi Jumatatu, mara baada ya Makanja kuingia "mtegoni" ulisema, "Niko makao makuu ya chama. Nimewekwa chini ya ulinzi...."
Akijibu katika namna ya kushtuka, kigogo huyo alijibu, "Wewe nani kakwambia uende huko… Watakuua. Siwezi kuja huko kukutetea...."
Makanja alikuwa miongoni mwa wagombea saba wa upinzani waliojitosa jimboni Musoma Vijijini kushindana na Mkono, lakini katika hali iliyoshtua wengi, wote walijitoa na kumuacha Mkono kupita bila kupingwa.
Mbali na Makanja, mwingine ambaye ameshtua uongozi wa Chadema kwa kuamua kutorudisha fomu, ni Dk. Ben Kapwani, ambaye alikuwa mwenyekiti wa Chadema wa Mkoa wa Iringa.
Kamati Kuu (CC) ya Chadema ilimteua Dk. Kapwani kugombea ubunge katika jimbo la Ismani, mkoani Iringa. Hatua yake ya kutorudisha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi, imesababisha William Lukuvi wa CCM kupita bila kupingwa.
Dk. Kapwani alijiuzulu wadhifa wake siku moja baada ya kuvuja kwa taarifa kuwa sekretarieti ya Chadema ilipanga kumsimamisha uongozi.
Kwa mujibu wa sheria mpya ya gharama za uchaguzi, matendo ya rushwa yanaweza kunyima nafasi ya kugombea mgombea aliyeteuliwa ikiwa mpinzani wake au chama cha siasa watawasilisha malalamiko kwa Msajili wa vyama vya siasa dhidi ya vitendo hivyo.
Taarifa zilizofikia MwanaHALISI zinathibitisha kuwa tayari Chadema kinaandaa malalamiko rasmi kwa Msajili wa vyama vya siasa dhidi ya hatua hiyo ya Mkono.
Sheria mpya ya gharama za uchaguzi inataka Msajili mara atakaporidhika kuhusu malalamiko kumfahamisha Tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) ambayo itamfahamisha katibu mkuu wa chama husika kuwa mgombea wake amepoteza sifa
 
Na Chadema walingoja nini mpaka uchaguzi uishe ndio walete hii habari au hao kina makanja washahama Chadema?
 
Back
Top Bottom