Mwanzo nilikua naamini Ali kiba hapendi kabisa kujihusisha na maswala ya diamond lakini naanza kuamini sio kweli.
tukiachilia mbali swala la hamisa mobeto kuwa mwanamitindo wa video wanawaita “video vixen” , they way Ali kiba alikuwa anaji-portray kutokutaka kuhusishwa na chochote kuhusu diamond aliwaaminisha wengi kuwa yeye huwa hana time na attentions zisizozuwa na msingi kwake.
lakini huenda upepo unavyoenda inaonekana ameshindwa na inabidi ili abaki kwenye game walau kwa miaka kadhaa ijayo ni lazima asake attentions.
Wapo wataosema hamisa ni video vixen Kama wengine lakini kwa Ali kiba alivyotuaminisha alikuwa sio wa kumtumia hamisa kwenye hii video , anahitaji Ipate promotion ya kutosha, Je ali kiba ameamua kufanya janja janja (opportunist) sawa na diamond anavyofanyaga?