Robidinyo
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 3,736
- 7,677
Jana kupitia Insta Live, King wa muziki wa Bongo Fleva AliKiba amefunguka namna ambavyo Dully Sykes alishiriki katika kumsaidia kutengeneza wimbo wake wa kwanza mwaka 2003.
.
Dully Sykes alimsikia Alikiba anaimba kwa Mjomba wake, akapenda sauti, akamchukua na kwenda studio kwa Enrico na wakarekodi wimbo wa Kuteseka Nimechoka. Baada ya hapo Dully Sykes akamtambulisha Alikiba kwa G Lover na kuanzia hapo Alikiba akaanza kufahamika.
Hata hivyo Kiba amewashukuru wale wote waliomshika mkono katika safari yake ya maisha wakiwemo, Mully B, Prof Jay, Sugu, Dj Venture, pamoja na Dj Majey aliyekuwa Dj wa kwanza kuchukua CD yake na kumpambania wimbo wake kupigwa.
King Kiba pia awamewataka mashabiki wake kuendelea kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona kwa kufuata maagizo ya mamlaka husika huku akiwataka kukaa mkao wa kula kwasababu Alhamis wiki hii anadodosha wimbo mpya.
Jana mida ya Saa mbili nilipandisha nyuzi hapa kuwapa taarifa wapenzi wa muziki wa bongo fleva kuchat na King wa muziki huu na pia nilitegemea tupeane update kupitia ule uzi kuhusu alichokisema King kwa mashabiki, NIMESIKITIKA BAADA YA KUKUTA UZI UMEFUTWA sijui shida nini kwa Mods kuendelea kufuta nyuzi nazoleta zinazowahusu kiba na Harmonize
Hata huu uzi sitoshangaa baada ya dk kadhaa ukafutwa
.
Dully Sykes alimsikia Alikiba anaimba kwa Mjomba wake, akapenda sauti, akamchukua na kwenda studio kwa Enrico na wakarekodi wimbo wa Kuteseka Nimechoka. Baada ya hapo Dully Sykes akamtambulisha Alikiba kwa G Lover na kuanzia hapo Alikiba akaanza kufahamika.
Hata hivyo Kiba amewashukuru wale wote waliomshika mkono katika safari yake ya maisha wakiwemo, Mully B, Prof Jay, Sugu, Dj Venture, pamoja na Dj Majey aliyekuwa Dj wa kwanza kuchukua CD yake na kumpambania wimbo wake kupigwa.
King Kiba pia awamewataka mashabiki wake kuendelea kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona kwa kufuata maagizo ya mamlaka husika huku akiwataka kukaa mkao wa kula kwasababu Alhamis wiki hii anadodosha wimbo mpya.
Jana mida ya Saa mbili nilipandisha nyuzi hapa kuwapa taarifa wapenzi wa muziki wa bongo fleva kuchat na King wa muziki huu na pia nilitegemea tupeane update kupitia ule uzi kuhusu alichokisema King kwa mashabiki, NIMESIKITIKA BAADA YA KUKUTA UZI UMEFUTWA sijui shida nini kwa Mods kuendelea kufuta nyuzi nazoleta zinazowahusu kiba na Harmonize
Hata huu uzi sitoshangaa baada ya dk kadhaa ukafutwa