Prezidah
JF-Expert Member
- Feb 1, 2013
- 750
- 182
Picha haiendani na stori nadhani anayeongelewa angeigiza hapo: i.e wazazi wakimlilia, kaanza kulewa, mademu, madawa. ....yule jamaa wa kibajaji angenogesha sana hii video
Last edited by a moderator:
Hakuna video producer anayetengeza video bila kuelezwa maana ya wimbo. Kuna tatizo la kuamini kwamba kila music video lazima yawepo maigizo ya kilichoimbwa, hii ni dhana potofu.
Kuna nyimbo nyingi mbona hazina maigizo? Kwani Number 1 Remix ya Nassib na Davido si watu wamedance tu mwanzo mwisho? Personally au Alingo za P Square si wamedance tu? Au New Flame ya Chris Brown na Usher Raymond na Ricky Ross kuna maigizo mle ndani?
Ni kawaida Narrative Music Videos huwa hazina maigizo jamani.
Ova
Wewe ndio umenifumbua macho sasa, hili linaweza kuwa tatizo la wengi, nashangaa watu wanaoikataa video nzuri kama ile, haina kabisa matukio ya kuboa.
Ukiwa msanii ni lazima usikae mahali ambako wengi walitegemea, ulete fikra tofauti na waliokuwa walitegemea mashabiki wako.
Ova
Katoa maana ya darisalam sio dar ila ni mji mkubwa wowote labda asingetumia jina darisalam angesema mwana wa mjinini nadhani mgeona video imeenda sawa ila kuna vitu vimemiss jumejitahidi dogo mwanzo mgumu
Unajua, hapa ww ndio hater.
Ile video kiba kachemsha kutokuweka maigizo, trust me. Yaan video ya kara jeremiah mpya ni nzuri kuitizama kuliko ya kiba.
Hivi wewe unazijua types of music videos? Unajua kama kuna Performance music videos, Narrative music videos na Conceptual music videos? Video ni taaluma jamani msiongee tu kwa kuwa ipo JF inayokupa nafasi ya kuongea.
Kilichofanyika kwenye video ya Mwana ni kitu kilicho kwenye taaluma kabisa, na ndivyo inavyokuwa Narrative music videos na imetendewa haki kama ambavyo imekuwa.
Producer haamui tu kuweka wimbo fulani kwenye video ya aina fulani, ila kutokana na urefu kisa chenyewe pamoja na mambo mengine ya kitaaluma. Kwa unavyofikiri kisa cha wazo la wimbo wa Mwana kinaweza kufanyiwa video na kutosha kwa dakika nne?
Nadhani Bob Marley angekuwa Mtanzania naye ungemshambulia kwa kufanya video ya wimbo No Woman No cry kwa aina ya Performance Music Videos, kwa sababu tu ni kwamba kuna mafunzo.
Unapaswa kuelewa kwamba hakuna wimbo usio na mafunzo duniani, ila kuna wimbo wa mafunzo mabaya na mafunzo mema.
Ova
Hivi wewe unazijua types of music videos? Unajua kama kuna Performance music videos, Narrative music videos na Conceptual music videos? Video ni taaluma jamani msiongee tu kwa kuwa ipo JF inayokupa nafasi ya kuongea.
Kilichofanyika kwenye video ya Mwana ni kitu kilicho kwenye taaluma kabisa, na ndivyo inavyokuwa Narrative music videos na imetendewa haki kama ambavyo imekuwa.
Producer haamui tu kuweka wimbo fulani kwenye video ya aina fulani, ila kutokana na urefu kisa chenyewe pamoja na mambo mengine ya kitaaluma. Kwa unavyofikiri kisa cha wazo la wimbo wa Mwana kinaweza kufanyiwa video na kutosha kwa dakika nne?
Nadhani Bob Marley angekuwa Mtanzania naye ungemshambulia kwa kufanya video ya wimbo No Woman No cry kwa aina ya Performance Music Videos, kwa sababu tu ni kwamba kuna mafunzo.
Unapaswa kuelewa kwamba hakuna wimbo usio na mafunzo duniani, ila kuna wimbo wa mafunzo mabaya na mafunzo mema.
Ova
Huu wimbo una video mbili au nimeufananisha?