Ali Kiba - Mwana Dar es Salaam (video)

Ali Kiba - Mwana Dar es Salaam (video)

Hakuna video producer anayetengeza video bila kuelezwa maana ya wimbo. Kuna tatizo la kuamini kwamba kila music video lazima yawepo maigizo ya kilichoimbwa, hii ni dhana potofu.
Kuna nyimbo nyingi mbona hazina maigizo? Kwani Number 1 Remix ya Nassib na Davido si watu wamedance tu mwanzo mwisho? Personally au Alingo za P Square si wamedance tu? Au New Flame ya Chris Brown na Usher Raymond na Ricky Ross kuna maigizo mle ndani?
Ni kawaida Narrative Music Videos huwa hazina maigizo jamani.
Ova

Mkuu you seem to have knowledge ya music videos but unalack morals.
Mkuu usidhani kila kilicho ktk theories lazima kiwe applied na wote.
Nyimbo nyingi unazozitolea mfano hapo juuu,hazipo ktk dhana sawa na wimbo wa mwana wa alikiba.
Ukisema maigizo sio lazima unakua unakosea wakati video nzima mule kuna maigizo(sema ni maigizo ambayo ni out of content ya wimbo)

Si kila anaesema kukisekana kwa maigizo ya huyoo.mwana basi anamchukia alikiba..na ndio maana wengi hawalalamiki kuhusu kuvaa wala quality ya video,bali wanalalamikia kukosekana kwa hicho kitu(maigizo kdg juu ya kilichoimbwa) na trust me kina matter sana,usikidharau ukaishia kusema watu wana mponda au hatujui aina za music videos no,utakua unakosea...we want something good zaidi coz kafanya something good but kakosea mahali.
Ukitazama maoni ya wadau kwa kichwa kisicho na kiburi cha kutopokea mawazo tofauti na unavyoamini utaona tu watu wanahate kumbe sivyo.
 
Wewe ndio umenifumbua macho sasa, hili linaweza kuwa tatizo la wengi, nashangaa watu wanaoikataa video nzuri kama ile, haina kabisa matukio ya kuboa.
Ukiwa msanii ni lazima usikae mahali ambako wengi walitegemea, ulete fikra tofauti na waliokuwa walitegemea mashabiki wako.
Ova

Kaka kuleta kitu tofauti haimaanishi utoke kwenye skeleton ya maudhui yako,especially kwa nyimbo yenye message Kama yake.
 
Katoa maana ya darisalam sio dar ila ni mji mkubwa wowote labda asingetumia jina darisalam angesema mwana wa mjinini nadhani mgeona video imeenda sawa ila kuna vitu vimemiss jumejitahidi dogo mwanzo mgumu

Kweli...na mm natamani tupate wengine Kama kumi hivii

Mfano hapo wewe ukiambiwa utaje wasanii kumi wakali wa Nigeria utawataja bila kukwama,lakini mtafte mnigeria muulize kuhusu wasanii kumi wa Tanzania akikutajia wengi basi ni watatu..
Tunahitaji kuvuka hili lengo.
Na kweli mwanzo mgumu that's why wadau wanatoa mawazo ya kujenga ktk suala la video...haya mawazo si ya kuyakataa tu eti kwa kigezo watu wamekariri.
 
Naona huyu Godfather atakula sana hela za wasanii wetu. Tangu Dimond atoke na video ya number one ndio kila mtu anaenda kwake

Mimi tatizo langu ni kwenye nyimbo zaidi kuliko video. Nyimbo hii Si kali kama ukilinganisha single boy, so far away Au usiniseme. Alitakiwa aje na ngoma mpya kali kama hizo nilizo taja halafu aitengenezee kichupa
 
Unajua, hapa ww ndio hater.

Ile video kiba kachemsha kutokuweka maigizo, trust me. Yaan video ya kara jeremiah mpya ni nzuri kuitizama kuliko ya kiba.

Huo ni mtizamo wako, ila 4 me the best video in 2014 is mwana, ikifuatiwa kwa mbali sana na pacha wangu ya rich mavoko. Hutaki unaacha.
 
Huo ni mtazamo wako na uheshimiwe, ila kwa jinsi nikuonavyo, unaleta ushabiki hapa. Video imesimama, utake usitake!
 
Safi sana...Hiyo ndo inaitwa kazi ya sanaa...Hapa watu walikuwa na mavideo yao kichwani ya maigizo....Jamaa amewacha waswahili wanashangaa....wanataka kuona maigizo eti binti katoka kijijini....

Big up Kiba....Video bombaaaa sans
 
Kweli Humu Mamburula Wengi Aisee Umeona Wapi Production Kubwa Za Kimataifa Zinafanya Upuuzi Kama Huo Mnaoufikiria Ungekuwa Kwenye Hii Video,labda Video Hiyo Mliyokuwa Mnahitaji Iwe Hivyo Mtakavyo Ingefanyika Kibongo Bongo Lakini Kwa Wenzetu Ni Kisasa Mno Na Director Wa Kimataifa Hawezi Tengeneza Video Za Kilocal.Big Up Kiba ,tusubirie Na Video Ya Ay Ft Seankingstone Itakuaje
 
Hivi wewe unazijua types of music videos? Unajua kama kuna Performance music videos, Narrative music videos na Conceptual music videos? Video ni taaluma jamani msiongee tu kwa kuwa ipo JF inayokupa nafasi ya kuongea.
Kilichofanyika kwenye video ya Mwana ni kitu kilicho kwenye taaluma kabisa, na ndivyo inavyokuwa Narrative music videos na imetendewa haki kama ambavyo imekuwa.
Producer haamui tu kuweka wimbo fulani kwenye video ya aina fulani, ila kutokana na urefu kisa chenyewe pamoja na mambo mengine ya kitaaluma. Kwa unavyofikiri kisa cha wazo la wimbo wa Mwana kinaweza kufanyiwa video na kutosha kwa dakika nne?
Nadhani Bob Marley angekuwa Mtanzania naye ungemshambulia kwa kufanya video ya wimbo No Woman No cry kwa aina ya Performance Music Videos, kwa sababu tu ni kwamba kuna mafunzo.
Unapaswa kuelewa kwamba hakuna wimbo usio na mafunzo duniani, ila kuna wimbo wa mafunzo mabaya na mafunzo mema.
Ova


Ha ha ha haaaa. Sasa unadhan mashabiki wangapi wanayajua haya? Unaongea nn ww? He should deliver what we want na sio kutuletea huu ulimbukeni wa kujifanya unajua aina video... Kazingua. Video ya kawaida... Soon itapotea na kusaulika.


Hivi wewe unazijua types of music videos? Unajua kama kuna Performance music videos, Narrative music videos na Conceptual music videos? Video ni taaluma jamani msiongee tu kwa kuwa ipo JF inayokupa nafasi ya kuongea.
Kilichofanyika kwenye video ya Mwana ni kitu kilicho kwenye taaluma kabisa, na ndivyo inavyokuwa Narrative music videos na imetendewa haki kama ambavyo imekuwa.
Producer haamui tu kuweka wimbo fulani kwenye video ya aina fulani, ila kutokana na urefu kisa chenyewe pamoja na mambo mengine ya kitaaluma. Kwa unavyofikiri kisa cha wazo la wimbo wa Mwana kinaweza kufanyiwa video na kutosha kwa dakika nne?
Nadhani Bob Marley angekuwa Mtanzania naye ungemshambulia kwa kufanya video ya wimbo No Woman No cry kwa aina ya Performance Music Videos, kwa sababu tu ni kwamba kuna mafunzo.
Unapaswa kuelewa kwamba hakuna wimbo usio na mafunzo duniani, ila kuna wimbo wa mafunzo mabaya na mafunzo mema.
Ova
 
Wabongo tunashida sana.. assume wimbo huohuo ingetumika kizulu naamini wabongo wangeipenda hii video.
Tatizo mnajitengezea video zenu kichwani lakini yeye hajelenga soko la ndani tu yupo internationally..
 
Huu wimbo una video mbili au nimeufananisha?

Ile uliyowahi kuiona kabla hii haikua official video ile walitengeneza tu na kuunga vipande vya matukio ya nyimbo za watu wengine...angalia vizuri yale matukio ni ya nyimbo za wasanii wengine tofauti tofauti
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom