Ali Kiba - Lupela

Ali Kiba - Lupela

Habarini JF...
Nianze kwa kusema kuwa kila binadamu ana uhuru wakufanya kile akitakacho bila kuvunja sheria! Uhuru wa kuongea na kutoa maoni ni moja ya haki za binadamu ila tu asivunje sheria!

Na mimi bila kuvunja sheria Naomba niweke wazi kwa kusema kuwa zamani kabla mziki wetu haujavuka nje ya mipaka ya Tanzania, na kabla ya wasanii wa Kibongo kwenda kushoot Video nje ya Nje kwa kutumia Madirector wa nje nilikuwa naangalia Videos alizo kuwa anafanya ADAM JUMA....kwa kiasi chake alikuwa anafanya vizuri kutokana na Mziki wetu ulivyo kuwa zamani....Ingawa nilikuwa naona Makosa mengi ya kiufundi na kitaalamu katika uongozaji wa videos hizo.....Nikikuwa nikiringanisha na wasanii wa nje nikawa ninaona kuwa ADAM JUMA kuna kitu anakosa.....Nilipo Fuatilia kwa ukaribu sana Videos zake nilikuja kugundua kuwa ni kweli Adam Juma kuna makosa yanafanyika.....Nikaanza kususia Videos anazo zifanya Mdogo mdogo baada ya kuona Anakosa Ubunifu!......Siku nilipo anza Kuziona Videos alizo Fanya Nisher nilianza kuamini kile nilicho kuwa nafikiria toka kwa Adam Juma, na baada ya kuangalia Videos za Goodfather nikajua dhahiri kuwa Adam Juma anazingua!

Pamoja na kuwa Adam Juma ni mzoefu wa Kuongoza videos na ni mkongwe katika kazi hiyo leo nimefikia Rasmi Kumdharau na kudharau kazi zake zote anazo zifanya....Nimefikia hatua hiyo baada ya kuona yale aliyo yaandika kuhusu Video ya Alikiba ya Lupela!

Siongelei kishabiki Lakini nimejiuliza maswali Mengi sana kuhusu Post Ya AJ ya kuisifia video ya Alikiba! Asitake kutumia ukongwe wake wa Kazi pamoja na Uzoefu wake kudanganya watu kuwa Video ile ni nzuri mimi Napinga!

Mtu kama AJ sio wa kukaa na kusema Video ile anaipa A,huku Video ikiwa na gizaa,rangi mbaya ya video,background mbaya,video hata haina Mng'ao ya kifupi ni Low quality! haina ushawisha wa mtu kuangalia mara mbili mbili! halafu AJ Anakuja kusema eti Sisi tunao kosoa Hatujui Art hivi kweli mkongwe kama AJ anasema pale tukiangalia kwa umakini tutajua....tutaona nini cha tofauti hata tuangalie kwa makini?, huo mda tunatoa wapi ilihali video inaumiza Macho?

Wasanii wetu wasilewe sifa za Madirector kama hawa kamwe mziki wetu hauto kuja kusonga mbele!, Huwezi kutoka kimziki nje ya Tanzania kwa Video kama Ya Lupela! Ni dhahiri kuwa AJ Kaongea kishabiki na bila kujua anacho kisema! Eti ukiangalia Video ya Lupela utapata Ujumbe.....Ujumbe gani utapata kwenye video kama ile tuwe wawazi,Kwa asie jua kiswahili ni dhahiri kuwa Lupela itampita kushoto kwa kila kitu!

Mwisho kwa quality ya videos za AJ labda kweli kwake hii ni Best Video! Lakini Naona hapa hawa Wakongwe wote wanapelekana wasiko kujua! siku zote Katika Sanaa,UBUNIFU ni kila kitu....Kuisifu video ya Lupela kwa Msanii mkubwa kama Alikiba ni Unafiki na Dharau kubwa sana....Hata underground sahizi hawatoi video kama Za lupela! Ni heri kuitazama Video ya AIYOLA mara 299 kuliko video ya Lupela

“Lupela @officialalikiba , this is art, watanzania
hatujui kuidadavua art. Hatujui thamani ya kitu,
tunachukulia kiurahisi urahisi tu, kila mtu
anajifanya anajua kitu ambacho sio sawa. Hii sio
video tu, tulia basi angalia kwa umakini utapata
ujumbe usipoelewa inawekana tatizo lipo kwenye
level yako ya kuchanganua ujumbe ktk picha, btw
sio fan wa alikiba ni mwana tu. Ningependa
kusema video ni A one, haifanani na kitu
ambacho tumezoe!!! Go kiba….. . ” – Adam Juma
Hii video ina vumbi kibaooo yaani mi nimeiangalia sana jana lkn haivutii kiukweli.....
Au king kiba anatoa pesa kidogo nn mana video ni gharama
 
Eti huyu nae kaongea jamani!Huu uhuru wa kutoa maoni unatufanya tuwe wendawazimu.
Sijaona chochote cha maana katika post yako hii zaidi ya chuki 'A One'.
Adam Juma kaipa sifa zake kitaalamu wewe unaleta story zako za ujuzi wa mitaani....WTF?
 
Eti huyu nae kaongea jamani!Huu uhuru wa kutoa maoni unatufanya tuwe wenzawazimu.
Sijaona chochote cha maana katika post yako hii zaidi ya chuki 'A One'.
Adam Juma kaipa sifa zake kitaalamu wewe unaleta story zako za ujuzi wa mitaani....WTF?
Anajifanya hachangii kishabiki..kajiumbua alipotaja wimbo wa Aiyola tumemjua alichokua anamaanisha.
 
Nakuunga mkono

Nakuunga mkono kabisa ktk hili, nimemuona Alikiba juzi juzi kupitia Tv akihojiwa ktk the sporah show, hajibu maswali anayoulizwa, na kama akijibu lazima atajilinganisha indirectly na diamond, alafu hajachangamka, hana ucheshi.
Ila pia nimewahi muona diamond ktk show hiyo hiyo, jamaa ni mcheshi sana na yuko down to earth kabisa. Nafikiri kwa diamond ule uswahili unamsaidia sana, hajali lolote, yeye anaongea na kucheka kuhusu lolote lililopo ktk ubongo wake.
Kiba aliambiwa aimbe wimbo mmoja wa diamond akakataa. In fact, alisema haimbagi nyimbo za watu, husikiliza tu.


nasubiri siku diamond aitwe aimbe wimbo wowote wa kiba
 
Tuwaache wasanii wafanye kazi Yao, kukosoa kila kitu na kufananisha kila kazi ya kiba na chibu kunaharibu Sanaa ya Tanzania. Wasanii wengine wanashindwa kukua Kisa mkasa Chibu na Kiba, watieni moyo Watanzania wenzetu achana na chuki za kishabiki.
 
Binasfi nilivyoiona kiba hana mshauri mzuri zaidi ya kundidimiza
 
Jamani tuache chuki kwa mtu anaejua mziki ni kwa mba unaendana na hisia.huu wimbo umetulia sema mnasababu zenu binafsi,mimi sio shabiki wa kiba wala baba zai,ila ukweli ndiyo huo.mziki umekaa kama mke na hakuna mke mwenye sura mbaya.mbaya kwako kwa wenzio poa
 
YANI UMEMPOOOOONDA ADAM JUMA NKAJUA SIJUI KAONGEA KITU GANI KIBAYA..
MBONA KAONGEA VIZURI TU NA KISTAARABU MNOO
 
Mkuu video lazima iwe na vipande ambavyo vitakufanya ushike remote mkononi, sasa video ipo kama masanii yupo jukwaani.

Labda niambie wewe ukali wa ile video uko wapi. ?
utofauti wa alikiba na diamondi ni kwamba, diamond anafanya mziki biashara, alikiba anafanya mziki usela.
Diamond huwa anajifunza kila siku, anajifunza jinsi ya kuwa tofauti na kuupeleka mziki wake juu zaidi.

Mameneger wanaomsimamia diamond na washauri wake wanapata mshiko wa maana, sio mbahili kutoa pesa. Hii ndio maana ya biashara, toa pesa upate pesaa
 
Video nzuri sana tu, mimi binafsi nimeipenda...

Ukiona mwanaume kazi yako kubwa kusubiri mwanaume mwenzako afanye kazi then wewe ukae kijiweni ukosoe ujue una matatizo makubwa sana... Ali Kiba kuweka kipande kinachoonyesha Tembo kwenye Video yake imekuwa kesi ila Dimondi alimweka Dr. Mwaka na wala hakuna aliyekosoa wala kusema chochote...

Ambao hamjaiona video hii hapa..


Tatizo hiyo video haiendani na kasi ya soko la sasa, video hiyo utafikiri ni ya miaka mitatu, hakuna ubunifu.
Bora video ya mr bluu ya hii ngoma yake aliyotoa majuzi
 
Eti huyu nae kaongea jamani!Huu uhuru wa kutoa maoni unatufanya tuwe wendawazimu.
Sijaona chochote cha maana katika post yako hii zaidi ya chuki 'A One'.
mmmh...
mamdogo...!!!
wewe si ndo umeanzisha uzi wa kuchunguza makalio ya Zari..?
sasa kinachokufanya umshangae huyu anayechambua video ya LUPELA ni nini..!?
samahani lakini!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom