Nakumbuka mwaka 2000 nilibahatika kuona video ya Uswahilini Matola, wimbo wa Kosa la Marehemu Hakuvaa Kondom, ile video jamaa walikuwa mbele ya camera wanacheza kwa kupishana au wanarudi kwa nyuma ili waonekane wote.
In fact location ilikuwa ni moja, mavazi hayakubadilishwa na ni jamaa tu walikuwa wanachana mbele ya camera. Hii video ya Lupela naifananisha na ile video kwa kiasi kikubwa kwa sababu location ilikuwa ni moja, nguo ni zile zile na inaonekana camera zilikuwa stationed sehemu moja tu.
Nilichokipenda kwenye hii video ni ile hali ya Kiba kujidhihirisha kweli yeye ni Balozi wa Wanyama na asingependa kuona wanyama wanauawa kwa sababu za ujangili.