Ajali Kibaha yaua Mhadhiri wa SUA

Ajali Kibaha yaua Mhadhiri wa SUA

Kwa mara ingine tena bara bara zetu zimeendelea kuwa kimeo na janga la Taifa. Mhadhiri kijana ; SUMA MWAITULO wa Crop Science and Production Department kapoteza maisha yake leo asubuhi. Alikuwa anaendesha gari akiwa na watoto wake pamoja na mtumishi wa ndani (House girl). Wote waliokuwemo kwenye gari wamefariki. Barabara zetu kwa kweli ni janga lingine ambalo linatakiwa liingizwe kwenye KATIBA mpya ili kudhibitiwa

Mbona wenzenu tunapita humo miaka nenda rudi hatufi? Alikuwa lena huyo mnasingizia barabara!
Mhaziri mzima unaacha kuajiri dereva proffesional kazi zote unataka kufanya wewe.
We unadhani udereva mchezo.
 
Kwanini umeruhusu, ee mungu mwenyezi..yatusononeshe moyoni ...Pole sana wafiwa na Wapumzike kwa amani marehemu wote.
 
Magufuli ndio anaetengeneza bara bara zisizo na viwango, malori yapo dunia nzima mbona kwingine hawalalamiki..

Mfano lori likitoka na mzigo bandari ya Dar mpaka Lusaka linapita barabara za tanzania mpaka border then linapita bara bara za zambia kuanzia boarder mpaka lusaka na mzigo uzito huo huo, mbona wenzetu hawalalamiki?

Magufuli mwizi tu, anajua kabisa bara bara zake hazina viwango ndio maana hajiamini, mbona rwanda, burundi, congo hawalalamiki wakati hayo malori yanaenda nchi zao na yanatembea kwenye bara bara zao na mizigo uzito huo huo waliotoka nao bandarini

mnamkata ngebe kwa kila hali,makampun ndio hayo hayo yakwenu mnatumia kila njia mpate tender za kutengeneza barabara feki,Magufuli peke yake hawezi mko wengi na mna nguvu kubwa,magogoni mnaenda hata na ndala,na haitusaidii sana,anyway vyanzo ajali za mara kwa mara kwa sasa tz inaweza kuwa..

uchakavu wa vyombo hivi vya moto

ujuzi hafifu wa kuvitumia

ulevi

miundombinu mibovu

vifaa feki i.e matairi

uzembe
 
Mhhhh!!! Msiba mkubwa sana huu kwa wafiwa. Poleni sana.

Kwa mara ingine tena bara bara zetu zimeendelea kuwa kimeo na janga la Taifa. Mhadhiri kijana ; SUMA MWAITULO wa Crop Science and Production Department kapoteza maisha yake leo asubuhi. Alikuwa anaendesha gari akiwa na watoto wake pamoja na mtumishi wa ndani (House girl). Wote waliokuwemo kwenye gari wamefariki. Barabara zetu kwa kweli ni janga lingine ambalo linatakiwa liingizwe kwenye KATIBA mpya ili kudhibitiwa
 
tena tangia viroba vimekuwepo sokoni ndo imekuwa balaa kabisa

hivi kikosi cha usalama barabarani si juzikati walinunua vifaa vya kupimia ulevi kwa madereva?.
Hakika ulevi unachangia sana hizi ajali.
Wiki iliopita nlikuwa nimekaa bar nikamwona dereva wa basi la mwanza to dar akinywa pombe hadi saa8 usiku. Saa12 asubuhi ilikuwa anatakiwa kuanza safari ya kwenda dar. Jiulize kama kuna umakini hapo kwenye uendeshaji katika hali ya ulevi.
Madereva wa fuso na malori ndio usiseme. Wengine wameweka hadi maboksi ya viroba ndani ya gari kwa ajili ya kunywa ili eti kukata usingizi.
 
Mhhhh!!! Msiba mkubwa sana huu kwa wafiwa. Poleni sana.
Ni kweli Baki, jumla wamekufa watu saba. Wawili kwenye Fuso na watano kwenye saloon. Watano familia moja. That woman was very confident and active. Kama movie vile
 
Dah... Leo kweli balaa!!! Kuna mtu alipost asubuhi kuwa leo ni siku ya mabalaa na kweli ndicho kimetokea!

"Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe"
 
Mwenyezi Mungu utusamehe kwa madhambi tunayotenda sisi wanadamu,nina uhakika ndo chanzo cha majanga yote haya..
 
kwanza natoa pole kwa ndugu wa mhadhiri,waswahili tunasema ajari haina kinga ingawa wenzetu wanapinga na mimi naona wapo right,inawezekana mhadhiri labda hakuwa na uzoefu wa kuendesha gari kwa long journey au tatizo la gari,anyway kwa barabara ya dsm moro angalau ipo katika viwango,kwa matumizi ya gari ndogo,sijui kwa malori,namuunga mchangiaji mmoja maana ni ajabu haya malori yanayosemekana yana beba mzigo mkubwa lakini huko yaendako hakuna tatizo,ilitakiwa barabara zetu ziwe bora maana kumbuka kuna nchi zaidi ya tano zinategemea kupitisha mizigo yao through our roads,sasa ukijenga barabara iliyo chini ya kiwango sijui unategemea nini,tena barabara yenyewe ya kawaida,zingekuwa za juu ingekuwaje,inabidi tanzania tuwe serious kwa kweli.
 
Back
Top Bottom