Aibu ya mwaka kwa Mwigulu

Aibu ya mwaka kwa Mwigulu

Status
Not open for further replies.
Mwigulu ni mtu wa ajabu sana.Lakini ngoja kwanza tupate uhuru
 
Mwisho wa ubaya aibu. Wahenga noma

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Tunasubiri CCM wamakonde huku watuletee Real Madrid na Wacheze na kariakoo ya lindi iliyoshuka daraja ligi kuu,

Kweli mfa maji haachi kutapa tapa,

Na haya madawa wanayojishughulisha nayo KWELI YANAWALEVY SANA,2015 HII HAPA KWENYE KONA,VIJANA WA MJINI WANASEMA ''MWACHE MWACHE''
 
Nao simba nawalaumu kwa kukubali mwaliko wa kijinga kama huo.

Simba wapo njiani kuelekea Tabora kucheza na Rhino mechi ya ufunguzi wa ligi kuu so kama walialikwa kupitia hapa si mbaya wamepata pesa na mazoezi pia!
 
Tunasubiri CCM wamakonde huku watuletee Real Madrid na Wacheze na kariakoo ya lindi iliyoshuka daraja ligi kuu,

Kweli mfa maji haachi kutapa tapa,

Na haya madawa wanayojishughulisha nayo KWELI YANAWALEVY SANA,2015 HII HAPA KWENYE KONA,VIJANA WA MJINI WANASEMA ''MWACHE MWACHE''

Mkuu BIG SHOW, gesi inatoka haitoki?
 
Wangekataa hela kamanda; wapo kikazi zaidi. Siasa za kishamba kabisa. Ni vigumu kuwaghilibi wananchi wa leo ambao njia za kupata taarifa zipo kibao.

Kwa muda mdogo niliojipa ili kujua tatizo la Mwigulu, nimegundua kuwa tatizo lake ni shule aliyosoma, ndiyo imemharibu, maana ndiyo imemfanya awe juu ya wajinga wenzake na hivo kumkabidhi majukumu yanayomlazimu kufanya afanyao.
Naamini kuwa, laiti kama asiingeenda shule, jamaa agekuwa na akili sana.
 
Kiukweli na naomba niliseme hili Wanairamba walielewe Mwigulu hafai hata kuachwa aiongoze familia yake! ni mtu wa ajabu sana! anafanya mambo ya kishenzi na ya aibu! mbona hajifunzi? Nimeichukia club ya simba kwa kutumika kijinga namna hiyo na "Natangaza rasmi kujivua ushabiki wa simba" Kama timu inaweza kutumiwa kipuuzi namna hiyo siwezi kuendelea nayo! Wanairamba ni lazima wachoshwe na mwenendo wa mbunge wao na wamuwajibishe kwa vitendo na ghadhabu kuu!
 
Masikini Simba...wameponzwa na Mwigulu bila kujua !
 
haha..eti nasikia anasema uliwanunu watu aliowanunu ulitoa kitu gani cha ghali ambacho pesa ya CCM imeshindwa....sasa mikutano 170,wakati lumumba hakuna tena mtu mwenye afya wala nguvu si mnataka muua kabisa mwigulu na Nape?


wapo busy wanafikiria hii plan, nadhani thisi time wanajua kiingereza ila kiingereza hakitokuwa issue ila uhalali:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...siwe-km-walivyoomba-meno-ya-tembo-yauzwe.html
Haya mawazo ni yale ya kwako au mengine umechukua ya watu ambao wanamatatizo sijaona unachoongea zaidi ya kujikanyaga na kujipinga mwenywe kweli bavicha kuna manyago ndiyo maana kila bavicha yeye ni matusi tu kumbe vichwa havina kitu.
 
Tangu jana nilipopata taarifa hii nilijivua rasmi uanachama wa simba, na pia nimejivua rasmi ujumbe wa kamati ya ufundi , huyu Rage asidhani simba anaweza kuitumia kisiasa . SHAME ON HIM !

Kumbe mkuu ulikuwa kwenye ile kamati ya ufundi? Asee...kimbia haraka
 
Kiukweli na naomba niliseme hili Wanairamba walielewe Mwigulu hafai hata kuachwa aiongoze familia yake! ni mtu wa ajabu sana! anafanya mambo ya kishenzi na ya aibu! mbona hajifunzi? Nimeichukia club ya simba kwa kutumika kijinga namna hiyo na "Natangaza rasmi kujivua ushabiki wa simba" Kama timu inaweza kutumiwa kipuuzi namna hiyo siwezi kuendelea nayo! Wanairamba ni lazima wachoshwe na mwenendo wa mbunge wao na wamuwajibishe kwa vitendo na ghadhabu kuu!
Mkuu jitahidi uanze kushabikia bavicha club ndiyo inakufaa,

kwani slaa akienda sehemu kazi zingine za pale hazifanyiki basi mwambieni aanzishe bendi ili aanze kufanya makongamano kama anataka kuangaliwa.
 
simba wameonyesha umbulula kwa kweli. Yaani hao waliocheza nao wanauwezo gani wa kuwachalenji simba...??? Yaani jina mlilolijenga hapa TZ, ndo mnaishia kucheza na hiyo timu..?? Mmejidhalilisha
 
Mkuu jitahidi uanze kushabikia bavicha club ndiyo inakufaa,

kwani slaa akienda sehemu kazi zingine za pale hazifanyiki basi mwambieni aanzishe bendi ili aanze kufanya makongamano kama anataka kuangaliwa.
Sasa mtu mmoja atajigawa vipi mara mbili?? Yaani huyo huyo awepo kwenye mkutano halafu wakati huo huo awepo kwenye kazi zake nyingine...???? Hebu jitahidini kufikiri kwa kutumia kichwa bana, hayo ma------ shughuri yake ni nyingine
 
Ndugu zangu wana JF,
Kama ilivoelekezwa hapo awali, Katibu mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Dr. Wilbroad Slaa anaendelea na ziara yake nchini. Leo hii, Dr. Wilbroad Slaa akiambatana na ujumbe wake wameanza ziara ya kichama Mkoani Singida. Awali, Dr. Slaa alipanga kufanya mkutano Kiomboi leo jioni. Hata hivyo, katika hali isiyo ya kawaida, Mbunge wa Iramba magharibi, Mwigulu Nchema aliialika timu ya Simba kucheza na timu ya Kiomboi bila kiingilio. Hii ilikuwa ni strategy ya makusudi ya kupunguza mahudhurio katika mkutano wa CHADEMA. Lakini pamoja na mbinu hiyo mufilisi, mkutano wa CHADEMA ulioanza majira ya saa nane Mchana ulifurika kupita kawaida, na wananchi walibaki katika hali ya utulivu mpaka pale Dr. Slaa alipomaliza kuhutubia na kupanda Helikopta kuelekea Singida Mjini kwenye mkutano mwingine. Katika mechi hiyo ambayo ilichelewa sana kuanza kutokana na gari waliyokuwa wamepanda timu ya Simba kupata matatizo ya kiufundi njiani ambayo imemalizika hivi punde, Simba S.C ilifanikiwa kuwakung'uta mahasimu wao kwa mabao matatu pasipo majibu.

Ndugu yangu Mwigulu, siku baada ya siku mambo yanazidi kukuendea vibaya. Huoni umuhimu wa kujirekebisha na kutimiza majukumu yako ya kibunge? Hizi gharama za kuwaleta Simba S.C hapa Kiomboi zingeweza kuwaleta Kindai Shooters au Magic F.C kutoka pale Singida Mjini na bado zikatosha kuwasaidia wananchi wa Urughu pale wanaojifungulia majumbani mpaka leo kwa kukosa kituo cha afya.. Badala yake, ulijitafutia utukufu kwa kuileta Simba yenye jina na uwezo mkubwa, sio ili kuwaburudisha wananchi au ili kujipima kimchezo, bali ili uizuie CHADEMA.
Sina shaka mfululizo wa kushindwa kwako kutakufundisha jambo.
"Akili ndogo vs. Akili kubwa"..
Naomba kuwasilisha.

Angekuwa binadamu wa kawaida, mwenye moyo wa kawaida na labda utashi wa binadamu, ningesema message sent..atasoma..ataelewa! But how mtu wa aina ya Mwigulu, mwenye roho mbaya, asiye na huruma hata kwa ndugu zake na aliyetukuka kwa matendo ya kishetani anavyoweza kuelewa lugha nyepesi kama hiyo? Naamini lugha pekee anayoweza kuielewa ni ile inayozungumzwa kuzimu na jehanum, ingawa anatakiwa kutubu kabla ya kufikia mwisho wa maisha yake hapa duniani ili asiende huko!
 
Mtakodisha sana Simba na itabidi muwalete hata Manchester kwa sababu mikutano itakuwa zaidi ya 170 (angalau 10 kila kata) kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani. Itabidi mkubali siasa za kistaraabu na za akili. Siasa za kijinga na fitina hazina nafasi katika karne ya leo. Poleni sana.

damu ya kijana uliyemuua kule ndago itakutafuna mpaka mwisho wa maisha yako. Ona sasa unavyoweweseka. Muuaji weee
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom