Aibu ya mwaka kwa Mwigulu

Aibu ya mwaka kwa Mwigulu

Status
Not open for further replies.
Wangekataa hela kamanda; wapo kikazi zaidi. Siasa za kishamba kabisa. Ni vigumu kuwaghilibi wananchi wa leo ambao njia za kupata taarifa zipo kibao.

Dr. Kitila,
Nlipata shida sana baada ya kupata taarifa ya ujio wa Simba. Hofu yangu ilitokana na ukaribu kutoka uwanja ambapo mechi imechezwa na pahala ambapo tuliandaa mkutano. Cha ajabu, Mkutano umemalizika hata kabla ya mechi kuanza kutokana na gari ya Simba kupata hitilafu.
Wananchi wa Iramba wamefanya maamuzi sahihi leo, wamechagua Jembe na mfuko wa mbegu badala ya Sinema ya maigizo..
 
Amekula za uso savimbi huo mda na fedha alizotumia angeweza kutengeneza uji wa lishe ili aendelee kumlisha mwanae apate akili za ziada asije akarithi akili za baba yake.
 
Ndugu zangu wana JF,
Kama ilivoelekezwa hapo awali, Katibu mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Dr. Wilbroad Slaa anaendelea na ziara yake nchini. Leo hii, Dr. Wilbroad Slaa akiambatana na ujumbe wake wameanza ziara ya kichama Mkoani Singida. Awali, Dr. Slaa alipanga kufanya mkutano Kiomboi leo jioni. Hata hivyo, katika hali isiyo ya kawaida, Mbunge wa Iramba magharibi, Mwigulu Nchema aliialika timu ya Simba kucheza na timu ya Kiomboi bila kiingilio. Hii ilikuwa ni strategy ya makusudi ya kupunguza mahudhurio katika mkutano wa CHADEMA. Lakini pamoja na mbinu hiyo mufilisi, mkutano wa CHADEMA ulioanza majira ya saa nane Mchana ulifurika kupita kawaida, na wananchi walibaki katika hali ya utulivu mpaka pale Dr. Slaa alipomaliza kuhutubia na kupanda Helikopta kuelekea Singida Mjini kwenye mkutano mwingine. Katika mechi hiyo ambayo ilichelewa sana kuanza kutokana na gari waliyokuwa wamepanda timu ya Simba kupata matatizo ya kiufundi njiani ambayo imemalizika hivi punde, Simba S.C ilifanikiwa kuwakung'uta mahasimu wao kwa mabao matatu pasipo majibu.

Ndugu yangu Mwigulu, siku baada ya siku mambo yanazidi kukuendea vibaya. Huoni umuhimu wa kujirekebisha na kutimiza majukumu yako ya kibunge? Hizi gharama za kuwaleta Simba S.C hapa Kiomboi zingeweza kuwaleta Kindai Shooters au Magic F.C kutoka pale Singida Mjini na bado zikatosha kuwasaidia wananchi wa Urughu pale wanaojifungulia majumbani mpaka leo kwa kukosa kituo cha afya.. Badala yake, ulijitafutia utukufu kwa kuileta Simba yenye jina na uwezo mkubwa, sio ili kuwaburudisha wananchi au ili kujipima kimchezo, bali ili uizuie CHADEMA.
Sina shaka mfululizo wa kushindwa kwako kutakufundisha jambo.
"Akili ndogo vs. Akili kubwa"..
Naomba kuwasilisha.

Siunajua tena pale dimba mkuu wao mzee wa bastola rage.. si ni mshirika wa mwigulu
 

Attachments

  • uploadfromtaptalk1376759558887.jpg
    uploadfromtaptalk1376759558887.jpg
    10.5 KB · Views: 362
Sasa hiyo aibu ya mwaka iko wapi mmechanganyikiwa naona umeandika mashudu baada ya kuona Babu anahutubia mavumbi
 
Simba wana njaa kali sana wapo tuyari hata kuwatembeza uchi wachezaji ili mladi wapate hela
 
Yani Simba wamefikia kucheza game za mchangani. Nadhani wana Simba ni wakati wa kujiuliza huyu Rage anapoipeleka timu yenu.
 
Mwachen ajiishie mwenyewe aliona bonge la akili kuwaleta simba. Na hapo is chini ya m20 zimesepa.
 
Tangu jana nilipopata taarifa hii nilijivua rasmi uanachama wa simba, na pia nimejivua rasmi ujumbe wa kamati ya ufundi , huyu Rage asidhani simba anaweza kuitumia kisiasa . SHAME ON HIM !
 
Amekula za uso savimbi huo mda na fedha alizotumia angeweza kutengeneza uji wa lishe ili aendelee kumlisha mwanae apate akili za ziada asije akarithi akili za baba yake.
Usimpe kichwa huyo Mburula.
Uji wenyewe anamlishia mtoto kwenye kitanda cha gest house, tena kitanda kimejaa mapampers na inzi kibao.
Amezowea kulisha watu sumu nadhani hata akipagawa anaweza kumpa mtoto tindikali huyu.
 
nauliza tu
hivi kuna hospitali za kisasa na mashule ya kisasa katika jimbo la Mwigulu?
hizo fedha za kuwaalika timu ya simba kwanini asingenunua madawati,vitabu na madawa katika jimbo lake?
Labda kipaumbele cha wana Iramba ni michezo zaidi na sio huduma muhimu kama afya na elimu.
Huyo ndio Mwigulu mzee wa first class ya udsm
 
Mwigulu Kwisha habari yake, mbinu zake ni za kitoto, aende china tena akasome upya
 
Mwigulu akili yake aina akili chezeaaaaaa chadema weeeeeeeeeeeeee viva cdm viva slaa
 
Wangekataa hela kamanda; wapo kikazi zaidi. Siasa za kishamba kabisa. Ni vigumu kuwaghilibi wananchi wa leo ambao njia za kupata taarifa zipo kibao.

SONGELA
Nijuavvyo kwa Wanyiramba jina la Mwiguluhuwa la kina mama/dada zetu tu! Linawapendeza.Huyu jamaa aliliporaje? Ni aibu kutumia mbinu za chini namna hii
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom