Huyu waziri kichaa, anajua maana ya kutengeneza ajira milioni 5?
Serikali kumwaga ajira milioni tano
2008-07-22 10:55:44
Na Mashaka Mgeta, Dodoma
Serikali inakusudia kutengeneza ajira mpya milioni tano, zikiwa ni zaidi ya zilizoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete, wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.
Akiwa kwenye kampeni hizo, alipogombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Kikwete, aliahidi kuwa serikali yake itatoa kipaumbele katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kutengeneza ajira mpya milioni moja.
Hata hivyo, akijibu hoja za Wabunge waliochangia hotuba ya bajeti ya wizara yake, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, alisema serikali inakusudia kufikia ajira milioni tano, kutokana na mkakati uliaondaliwa kuhusu ukuzaji wa ajira nchini.
Alisema mkakati huo uliandaliwa kwa ushirikiano wa serikali, Shirika la Kazi Ulimwenguni (ILO) na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Alisema mkakati huo unatoa fursa zaidi kwa watu wa kada na makundi mbalimbali, wakiwemo wenye ulemavu.
Aidha, Profesa Kapuya, alisema hivi sasa serikali inawasiliana na wadau kama taasisi zisizokuwa za kiserikali na mashirika mbalimbali, ili kupata takwimu halisi ya ajira mpya zinazotengenezwa nchini.
Alisema hadi kufikia sasa, takwimu zinaonyesha kuwepo ajira mpya 437,035, ambazo zinatarajiwa kuongezeka kupitia jitihada mbalimbali zinazofanywa na kutoa mfano wa Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA).
Profesa Kapuya, alisema fasihi ya elimu ya Ukimwi mahali pa kazi, ipo katika hatua ya uchapishwaji na itakapokamilika, itasambaza kwa ajili ya matumizi yake.
Aidha, alisema serikali inatambua kuwa viwango vinavyolipwa kutokana na madhara yanayotokea sehemu ya kazi, havilingani na athari zinazowakabili walengwa.
Alisema kutokana na hali hiyo, serikali inapitia sheria hiyo kwa ajili ya kuandaa mswada wa mabadiliko yake, utakaowasilishwa bungeni katika mkutano ujao mjini hapa.
Pia, Profesa Kapuya, alisema wizara yake inaendelea na mpango wa kukagua vibali vilivyoombwa na wageni kwa ajili ya kufanya kazi nchini, ili kubaini ikiwa vinakiuka taratibu zilizopo.
Alisema kwa mujibu wa taratibu hizo, kazi zinazopaswa kufanywa na wageni, hazitakiwi kuwa katika kiwango kinachoweza kufanywa na wazawa.
Wakati huo huo, Profesa Kapuya, alisema imebainika haja ya kuongeza wigo wa ushiriki wa vijana, kushiriki katika uundwaji wa baraza la vijana la Taifa.
Profesa Kapuya, alisema mchakato huo ulianza, ulisababisha kufanyika kwa mikutano miwili, ambapo iligundulika kuwepo haja ya kuwashirikisha vijana wengi zaidi, hasa kutoka maeneo ya vijijini.
Alisema mchakato wa sheria unaokidhi mkakati wa kuundwa kwa baraza hilo, utawasilishwa kwenye kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, mara utakapokamilika.
SOURCE: Nipashe
Tuma Maoni Yako
NITALETA AJIRA MILIONI MOJA...
ANYWAY SIJAWEZA HATA kuleta hata ajira laki moja/.....
lakini....
MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YANAWEZEKANA..
TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA...
SORRY GUYS - VUMILIENI MAUMIVU...
NIMEKUMBUKA...
KULETA AJIRA MILIONI TANO KABLA YA MWAKA 2010 INAWEZEKANA...
TEH !! TEH !! WADANGANYANYIKA BWANA!!!!
WENU ....
JANGALA MICHOSHO KIWETE..
CHAGUO la " mungu " AKA "JOHN WALKER[/SIZE]
[/I]
]
....
Ndugu Wananchi;
Mwaka uliopita ulikuwa mgumu sana kwa ustawi wa uchumi wa nchi yetu. Matarajio na malengo yetu makuu kuhusu ujenzi na maendeleo ya uchumi wetu hatukuweza kuyafikia. Mauzo yetu ya nje ya bidhaa na mazao ya kilimo, mifugo, viwanda na madini yalipungua kwa kukosa masoko katika nchi za Ulaya, Marekani na Asia. Bei za mazao na bidhaa zetu hizo iliporomoka sana. Watalii walipungua na mapato ya utalii kushuka pia. Wawekezaji wameahirisha uamuzi wa kuwekeza nchini. Biashara ya uchukuzi wa mizigo iendayo na itokayo nchi jirani ilipungua sana. Mapato ya Serikali yakapungua kwa asilimia 9. Jumla ya yote kasi ya kukua kwa uchumi inatarajiwa kushuka kutoka lengo la asilimia 7.8 na kuwa asilimia 5. Hii ni athari kubwa sana kwa taifa letu.
Pamoja na kuwepo kwa sababu nyingine, hali hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na matatizo makubwa na ya aina yake yanayoukabili uchumi wa dunia kuanzia mwaka 2007 na kuwa mbaya zaidi tangu mwaka 2008 hadi sasa.