Yaani Ab-Titchaz, Kule West Africa wenzetu walishazoea kuongea mambo ya ndani hadharani na yanaandikwa kwenye magazeti mpaka kichefuchefu.
Kinachowaponza, kule kwa wenzetu, utamaduni wa wake wengi haujafa kabisa. Kwa mfano Rais wa Togo (kama sikosei) ana wake nane na hadi sasa hakuna anayesimama kama first lady. Haya Obasanjo naye ndio usiseme, yaani marehemu Stella, alikuwa kama mke wa 10 kwenda mbele na ana watoto kama utitiri. Mbaya zaidi kavunja ndoa ya mwanaye na kulala na mkwewe.
Huyu wa Gambia ni malaya wa kutupwa na hilo linajulikana waziwzi kabisa. Ila alipompata kimwana wa Kimorrocco. Akapiga stop mke mkubwa kamtupa nje kwa talaka. Akaanza kuvinjari na nyumba ndogo kama first lady. Ila sasa nadhani akawa anammiss mke wake wa kwanza hadi akawa anamfuata kwa siri. Ila sasa mambo yakaaza kufanyika kiwazi hadi amemnunulia jumba kubwa sana la kifahari (kumbuka ni tax za wananchi). Nyumba ndogo hasira juu kafunga vilago na hajulikani alipo ila wanahisi karudi kwao.
Siwezi kusema ni tabia za wanaume wa kiafrika japokuwa ndio asilimia kubwa tunasikia story ndio hizi hizi. Ila pale inapofanyika kwenye high offices, inatia mashaka.
Lucy Kibaki ndio kabaki kituko huko Kenya. Huku kwetu East Africa kidogo kuna kale ka-aibu sijui niseme ila tukiamua kufungua paa za nyumba za watu tuone kinachoendelea- maumivu matupu.
Kwa ubora wa 1st ladies, Kwa kweli I will stick with Salma Kikwete. She is a huge improvement kutoka kwa Anna Mkapa, Japokuwa wa Mali naye ni mzuri ila kuna picha kadhaa za huyu bibie wa Mali nazo zinatia shaka kuhusu rangi yake ya ngozi kama ni halisi. Picha yake tuliyonayo naona it has been doctored na ndio formal picture ya first lady, need we say more.