Afande Sele: Nitapambana na Abood

Afande Sele: Nitapambana na Abood

Sina hakika kama watu wa morogolo wanaweza wakafanya ujinga wa kumchagua mtu ambaye hamnazo,ATAENDA KUVUO NGUO NGUO BUNGENI HUYO OOHHH,si mmemuona yule anamiaka chini ya kumi na 8 alivyo fanya!hiyo ndio jamii ya wabunge tunaowataka wana M4c

si kosa lako mkuu.
 
[TABLE="width: 100%"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]

HUU NDO UJINGA NA AIBU ZA MFALME WA MISTARI AFANDE SELE

SELE.jpg
 
Msanii wa kizazi kipya, mfalme wa rymes, Selemani msindi a.k.a baba tunda, simba dume, AFANDE SELE amesema sasa yupo tayari kwaajili ya mapambano ya kweli katika kuhakikisha jimbo la morogoro linapata kile walichokikosa kwa miaka 50 sasa.

Akizungumza ofisin ya chadema kata ya msufini, mkali huyo mwenye nyimbo za kuelimisha kasema sasa watanzania twahitaji kubadilika na kuangalia mbele kwani ni muda mrefu sasa tumechoshwa na unyanyasaji wa uongozi wa ccm, tumehaidiwa mengi na bwana mkuu lkn hakuna anachokitekeleza zaidi ya kutembea nchi za watu.

Anasema taifa haliwezi kuendelea kwa kuomba misaada nchi za nje bali kwa jasho la mtanzania mwenyewe ambaye atapata elimu bora itakayo mwezesha kujiajiri mwenyewe na sio mfumo wa sasa wa elimu unao tegemea ajira kutoka serikalini. Akiongeza kua nimejiunga chadema kupambana na wasiopenda haki na demokrasia, wasiojali utu na umasikini wa mtanzania, wasiojua shida ninin hasa, wasio jua uchungu wa vifo vya wa mama wajawazito na watoto wanaokufa kwa malari kutokana na huduma duni zinazo tolewa na serikali isiyowajali watu wake kwa mda mrefu tangu serikali ya awamu ya tatu.

Anasema sasa yupo fiti kuungana na watanzania wapenda haki na wanademokrasia kuzunguka nchi nzima kuelimisha jamii kuhusu serikali hii mbovu ya ccm.Akizungumzia mgoogoro unaokikumba chama anasema ni vema mh.zitto akawa mpole na kujishusha ilikufikisha chama salama,, anaongeza kuwa haoni sababu ya malumbano yasio kuwa ya msingi hasa wakati huu ambao tunaukaribia uchaguzi wa serikali za mtaa kwahiyo ni bora zitto akapatana na mwenyekiti wake ili tutimize ndoto ya watanzania 215.

Akizungumzia nia yake yakugombea ubunge jimbo la morogoro mjini anasema watakavyoona wananchi ndivyo atakavyo fanya yeye kwani anatamani jimbo hilo lisiwe chini ya ccm 2015 tena chini ya abood.Anasema abood kageuka kuwa mfazili na sio mbunge wakupeleka matatizo ya wananchi bungeni, wananchi wa morogoro hawataki msaada wa magari ya kusafirisha maiti kwakuwa hata iwevipi maiti haiwezi kuozea ndani kisa hakuna ufadhili wa magari ya abood na nitahakikisha abood analiacha jimbo hilo kwa watu wanaojali utu wa mtanzania, aliongeza afande sele.

piiipoooozzzzzz!!!,
Je ayatollah mtei atakubali mtu wa kambi ya Zitto kugombea!?
 
Last edited by a moderator:
mkuu mimi ngoja nisiseme kitu kama huyu sele naye anataka ubunge.



Ajabu sana mkuu wangu, lakini ni sawa tu.Kama tuna waganga wa kienyeji na waimba bongoflava bungeni basi muache tu na KAMANDA KIPENSI atest zali lake.
 
Kuna wakati bunge lilikuwa na walimu wengi tukawa tunagawana umasikini kila mtu akaridhika, wakaja madakatari, maprofesa na wafanya biashara wanapeleka pesa kwenye mabenki ya nje zikakopeshe watu wa nje. Wapika vitumbua wetu hawana pa kukopa. ngoja tuchague na hizi bongo flava labda tutapata nafuu
 
Kila la kheri king of rhymes lakini msumeno wa mbunge awe na degree utakukata,mr 11 naye yuko kitanzini mbowe imemkosa kidogo........,lema ni muhanga pia

Maji marefu humwoni?et prof hata kapuyo yo yo namashaka naye
 
Katiba inasema mbunge awe na digrii moja;
sijui kama baba tunda atakuwa nayo.
 
Unaweza ukawa domo zege bungeni lakini maendendeleo yakapatikana. Mimi nipo Morogoro, toka Huyu SUNCHE achukue Ubunge, Barabara za lami zimejengwa kwa kasi sana hapa Morogoro mjini. Mfano. Toka Iringa Road kwenda Mazimbu Ndani. Toka Ipoipo (Kijiewe cha Nguruwe) Kwenda Dodoma Road ikipitia KIHONDA magorofani. Toka daraja la Mji Mpya kwenda Kichangani na kwenda Mtawala. Toka sabasaba kwenda Msikiti wa Mahita kuunganisha barabara ya kwenda Mzumbe.n.k n.k. Lakini wabunge waliopita Waswahili wenzangu hakuna chochote cha maana walichokifanya.
Okay lingine analofanya Abood ni tu-personal: Anatoa mabasi yake bure kubeba watu kuwenda kwenye Mazishi ndani ya Manispaa ya Morogoro. Hata kama kuna misiba 10 maadamu mwenyekiti wa serikali ya mtaa aendee kutoa taarifa ofisini kwake basi litatolewa. Kwahiyo wanao sema ABOOD haja fanya kitu sidhani kama ni wakazi wa Morogoro. Afande SELE anahaki ya Kugombea Ubunge kama raia mwingine yoyote yule; mwisho wa siku wenye maamuzi ni wananchi.
 
Ujinga wake mwingine ni upi? kisha fananisha kikazi kati yake na yule Prof. wa Kaliua.

ni yupi atakua na ujinga mwingi ama ni yupi atakuwa na nafuu kwa jamii.
 
Afande sele mtafute Lema akupeleke "cambridge" alipopatia degree yake. Ili katiba mpya ikija "vibaya". tayari una gamba lako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom