Adhabu za wanajeshi

Adhabu za wanajeshi

Mpaka umuone mkubwa wao labda iwe tu ni bahati yako

Kama askari tu anazinguliwa na akitaka zinapigwa na hakuna anaefukuzwa kazi(kuna mjeshi alizinguliwa na polisi,akaenda kambini akawashitua wana,wana wakavamia kituo cha polis kikapigwa),na sikusikia mtu katimliwa
Itakuwa enzi za mwalimu hizo au nao polisi waliokuwa kwenye kituo hicho walikuwa wapumbavu
 
Sasa hivi sifa ni pesa sio upot, aje na upot wake aje na mwenye pesa zake hata Dem, alaf tuwafungulie mbwa wakali tuone ni nani atakaeng'atwa

yani hapo lazma pot ang'atwe na upot Wake maana hana pesa.
Wewe ukifunguliwa mbwa mkali wale mbwa vichaa Germany shefad una uhakika utapona ?
 
Itakuwa enzi za mwalimu hizo au nao polisi waliokuwa kwenye kituo hicho walikuwa wapumbavu
Enzi hizi unakuaje wanafungulia kesi Mahakamani au sio au wanaongeza na kasimu ?
 
Unachokifanya ni kushangilia ujinga wa kutokujua haki zako, Askari wa jeshi lolote haruhusiwi kukushambulia hata kama umevunja sheria ilimradi tu hujakataa kutii amri ikiwa amekuja kukukamata haruhusiwi kukupiga Wala kukudhalilisha kwa adhabu yoyote chombo kinachotoa adhabu ni mahakama anachotakiwa kukifanya ni kukufikisha mbele ya vyombo vya sheria ili ukahukumiwe kwa kosa ulilofanya kama kweli hilo kosa lipo

Akikwambia chuchumaa/kaa chini we kubali ila akikwambia ruka kichura mwambie siwezi kwasababu za kiafya hapo sasa chochote atakacho kufanya ikiwa ni kukushambulia unaruhusiwa kumshitaki utaratibu wa kushtaki ni uleule
Shambulizi lolote atakalo kufanyia ni kosa kama makosa mengine ya shambulio na unaruhusiwa kufungua kesi dhidi yake na akawajibishwa

Huyo dereva alitakiwa akatae kwanzia amri ya kuambiwa ashukie dirishani kwakua siyo amri halali na ni kinyume na utaratibu kwakua ilikua inahatarisha usalama wake
Tanzania hadi ufungue kesi hio labda uende ukafungue kesi kwa kasimu bila hivyo unakusumbua tu, Mahakama inafanya kazi na Jeshi la Polisi usijifanye haujui, ushanielewa lakini au nikwambie tu ulichokiandika kipo kwenye CPA na kwenye Penal Code Ila wakikubanisha lazima wakuchangamshe damu kidogo ili uwe adabu siku nyingine usirudie kufanya ujinga, sawa na mama yako akwambie usichezee kiwembe hicho ukachezea kikakukata akiona umejikata anakuosha kwanza mabanzi ya sura km manne hivi au matano alafu ndio anakupa huduma ya kwanza ili siku nyingine usirudie kufanya ujinga wewe mtoto Mpumbavu, mwanajeshi ampi adhabu za kuchosha raia mtiifu, tembelea shule zilizo karibu na kambi za Jeshi asubuhi mtu km wewe wale watoto unaweza ukasema wanaonewa tena unaweza ukaingilia kati uwaambie jamàa waache kuwapigisha kwata wasiendelee kuburuzwa kwa kuwapigisha gwaride la kufanya kazi za usafi wa shule asubuhi asubuhi na baridi
 
Jaribu uende kuleta ujuaji wako, utasimulia hadi wajukuu kitakachokupata. Wanajeshi epuka sana akiwa yupo eneo la kazi na hapo ulimkuta alipangiwa jukumu fulani, kazi ikiharibika anaadhibiwa na kuliko litokee hilo ndiyo anakuzingua. Kama huyo wa lori aliyekutana na MP, wale kituo chao cha kazi ni hapo getini kama angekutwa na wakubwa geti limezibwa hivyo angezinguliwa na ndiyo hapo aliamua kumzingua yeye.

Cheza na mwanajeshi sehemu zingine zote ila si eneo lake la kazi, wanaadhibiwa adhabu mbaya sana wale jamaa au kutukanwa kabisa na wakubwa kama mambo yakienda hovyo
Akhil za mtanzania
 
02.Tukio la pili ni siku ya kwanza kwenda pale shuleni! Ilikuwa form five!
Aisee kwanza nilienda shule saa mbili ahsubui, nikamkuta MP anaitwa MSENGI. Akaniweka bakora nne, huwezi amini day one.
Hii kawaida.
Day 1 nilienda na sketi nimeshona kwa fundi Maiko, sikuvaa zile zao na viatu vyao sijavaa.
Kumaliga akanidaka.. akanipeleka kwa Matrons, anawaambia huyu hajavaa nguo zetu.
Kufika kwa Matrons nikiwa Dar hali ya hewa inanitakatisha flani hivi, kauso kanakuwa 👌Yule Matrons akaniangalia kwa wenge sijui akanambia nimejiremba 😂😂
Uwii niliambiwa kanawe uso urudi unatiririka maji.
Na bado nikachapwa kwanini sijavaa sketi zao na viatu vyao.
 
Mimi sikubaligi upumbavu, huyo mwanajeshi mshamba na njaa Kali angekuja kwangu aone, ningevomjibu dry sitishiwi bunduki Mimi, Wala sitishiwi kifo hata siku moja

Angeenda ailete hata Kambi nzima, siogopagi kufa Mimi, liwalo na liwe na ndo wangejua kweli hii Dunia kuna watu watata, sio Dunia, Tanzania kuna watu watata. Mimi ndio MWAMBA.
Kabla sijakuunga mkono kuhusu kutoogopa kifo kwako, tuambie ulishakufa mara ngapi ili tujue uhalisia wa kauli yako
 
Kuna jamaa alitaka kuovertake msafara wa wajeda barabara ya Iringa~Dar, kabla hajamaliza kuyapita magari yao mbele gari ikatokea ikabidi abane katikati ya wajeda. Aloo walimwambia nae Kawa part ya msafara wao Hadi DSM wakati jamaa alikua anaishia Moro.
 
Hawakuzingui km hujazingua, pita Lugalo nenda kwenye zile bustani za pembeni vua sketi yako mwaga kojo alafu jamaa wakuone hakikisha wamekuona
Napitaga zangu tu pembeni huku, ila Sasa Hadi avue nguo hadharani huyo si mgonjwa wa akili
 
Jamaa wana adhabu kali
But kuna mkuu XXX aliteuliwaga kwenda ule mkoa wa Kigoma na back ground yake alikuwa na cheo kikubwa tu huko baka baka.

Sasa kuna sehemu ziwani huko watu walikuwa wanalima nyanya na walikuwa hawaruhusiwi basi mheshimiwa akaenda na vijana wake wakaenda kufyeka nyanya zote ziwani.

Wazee walokuwa wanalima zile nyanya walikuwa wanaomba ziachwe ili wavune hivyo hvyo japo hazijakomaa waliambulia virungu na kuondoka lakini walitoa kauli moja tu kuwa tunaenda kukuroga jamaa kutokana na kujiamini na ile morali ya baka baka akawa anajibu mbovu wazee wakaondoka zao.

Baada ya week jamaa alipata mimba kila siku mimba inazidi kuwa kubwa kufika miezi 3 ikabidi wampeleke hosptal,wakamkuta kweli ana ujauzito kutokana na unyeti wa jambo alihamishwa mkoa kimya kimya na issue ilizimwa kimya kimya jpo watu wa mkoa huo baadhi wanakumbuka hilo.

So hapo kwa upande wangu ni kila mmoja asimame kwenye upande wake raia asimamie sehemu yake kama raia,na askari asimame kama mlinda raia na mipaka yake kama kiapo chake kinavyomtaka,ila kuendelea kuwasifia humu kwa wanavyofanya kinyume na sheria muwakumbushe pia kuna upande wa pili kwani si kila raia utamfanyia hilo atakubali.

Wengine utamfanyia hilo ataenda kukufanyia ya kukufanyia ukapoteza hata maisha huku ukiiacha familia yako ikiteseka kwa pension yako ya milioni 10 utayoiacha kutokana na mshahara wako wa laki 4

kadak-tea-500x500-500x500.jpg
 
Hiyo ninayokwambia ni miaka ya 90 ambapo wajeda waliogopeka zaidi ya yule malaika mtoa roho za watu.

Kwa sasa mambo hayo yamepungua baada ya wajeda wenyewe kutambua kwamba kwa sasa raia wengi wana uelewa mkubwa, wanajua sheria na haki zao. Lakini pia kuna hili swala la mjeda kumfanyia ushenzi raia afu kesho mjeda huyo anaanikwa katika mitandao fulan ya kijamii na kuchukuliwa hatua za kinidhamu kupitia sheria zao za jeshi.

Yani kwa sasa ukiona mtu anahenyeshwa na mwanajeshi kizembe zembe basi jua kwamba huyo jamaa ndo kwanza anaingia mjini siku kadhaa zilizopita.
Mie mwenyewe sikubali mtu anizalilishe kisa eti ni mjeda na Kuna wajeda wengine huzalilisha Hadi watu umri wa kuwazaa kabisa eti kisa mjeda. Jamani Mimi sifanyi adhabu yoyote tuone ka wataniua
 
Ukiwatii ndo umeumia kwa sababu utafanya adhabu ambazo siyo haki kwa mujibu wa sheria. Usiwatii kabisa ili option yao iwe ni wakupige wakuumize au wakuue, halafu waje waone kama Jeshi litawakingia kifua. Itakula kwao!.

Baadhi ya Wanajeshi hasa vijana wanaendeshwa na Mob psychology. Hizi tabia za kihuni huwezi kuzikuta kwa wanajeshi ambao ni matured!.
Siyo wanajeshi matured tu mkuu, bali na waliosoma yaani wenye elimu zao, utayakuta mambo haya kwa watoto wa masikini wenye elimu za fom foo tena za kuunga unga
 
Si unataka kujua km wanajeshi wanabutua au wanafanyaje, hawakupi adhabu km huna kosa au hujawakosea hususani unapokua mazingira ya eneo la Jeshi
Hekima ni hii, hakuna haja ya kujifanya mjuaji ukikosa. Tii na uwe mpole tu.
 
Askari wa Tanzania wengi - ingawa sio wote- hawana adabu, wanapenda kutumia uaskari wao kuonea watu.

Hizi habari zinanikumbusha mbali sana.

Kuna siku tulikuwa tumekaa maskani Upanga, muda wa jioni vijana wanakutana maskani. Mara paap, tukawa tumeaona askari kibao wanakuja kutoka mbali, wako doria kundi zaidi ya ishirini, wamebeba bunduki na marungu.

Basi nikawaambia madogo tuliokuwa tumekaa nao maskani, kama hamjiamini, ondokeni kabisa, wale wanakuja kutaka kututingisha hapa.

Basi kuna madogo wakaondoka, wengine tuliojiamini tukabaki.

Wakaja wakafika maskani, sisi kama kumi, wao zaidi ya ishirini. Mmoja akatuuliza "Haroo, mnafanya nini hapa?".

Basi hawakujua wanaongea na watu wa aina gani, jamaa mmoja wa maskani akamjibu "Afande hivyo ndivyo ulivyofundishwa kusalimia watu?". Ikabidi yule askari astuke kwanza. Alitegemea watu wataogopa, hakutegemea kujibiwa vile.

Sasa akaja askari mmoja, nafikiri ndiye alikuwa mkubwa wao yule, akaanza kuuliza watu, mmoja mmoja, "Wewe unakaa wapi?" Mtu anamwambia hapo, "Wewe unakaa wapi?" Mtu anamwambia hapo. Wakamfikia jamaa mmoja.Wakamuuliza "Wewe unakaa wapi?" Akajibu kwa Baba Ben.

Askari akauliza, "Kwa Baba Ben? Baba Ben gani?" Jamaa akajibu "Kwa Ben huyo huyo wa Jamhuri ya Muungano, kwani wewe unamjua Ben gani mwingine Tanzania?" (Hapo kipindi cha urais wa Ben Mkapa).

Yule Polisi akawa kastuka, kama hajaamini hivi, sasa kumbe kuna wenzake huwa walikuwa wanaenda kulinda kwa Mkapa, wakawa wamemjua yule kijana wa kwa Mkapa. Ikawa kama wanamwambia yule mkubwa wao kwamba huyu tunamjua anakaa kwa Mkapa, tunamuona tukienda kulinda pale.

Basi hapo hapo nikaona wale polisi wanabadilika mara moja, wanasema unajua wazee ni suala la kufahamiana tu, tulikuwa tunajuana tu, hamna tatizo, hamna tatizo tulikuwa tunatambuana tu.

Kuanzia siku hiyo mpaka kituoni kwao kile kijiwe walikiwekea alama ya X kisiguswe, wakasema hapa kuna watoto wa Mkapa huwa wanakaa.

Nikasema hapa ingekuwa wamewakuta watu wasio na majina wangewasumbua sana.
Kiranga sorry, wewe ulikuwa na jina au ulitumia tu jina la huyo mwenzako wa kwa Baba Ben?
 
Huo unakuwa mshamba mkuu. Hawawezi man to man
Man to man kuna watu wapo vizuri kuliko hawa wanajeshi,
Kisa kingine kuna mshikaji anaendesha bajaj hapa maeneo ya Mwenge,basi kuna siku anavuka tu barabara bila bajaji kuna gari ya wanajeshi walikuwa wawili wakampelekea mshikaji anaevuka kwa miguu zima zima,sasa yule mshikaji kuona anataka kugongwa na lile gari si akamind na wale wajeda wakamind mjeda mmoja akashuka kumfuata mshikaji,anataka kumkamata mshikaji bahati mbaya ikamtoka ngumi bhana ikampata yule mjeda usoni,bahati nzuri kabla ugomvi haujaendelea watu tukajaa tukawaamua wasipigane,yule mshikaji akapata upenyo akakimbia kumbe wale wanajeshi wakauliza wakaambiwa kuwa yule mshikaji anapaki bajaj pale Mwenge,kesho yake wakaja watatu wakamkuta mshikaji wakamchukua mpaka kwenye uwanja wa vinyago pale Mwenge huwa wanacheza mpira,wakaanza kumuogesha matope mshikaji bhana,kumbe pale kuna mkubwa wao akawauliza inaama huyu mtu aliepigana na mwanajeshi ndio huyu?embu muachane aondoke zake mnalidhalilisha jeshi tu,maana huyo mshikaji ukimuona ni mwembamba kichizi.mshikaji karudi kijiweni kalowa tope mwili mzima.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Man to man kuna watu wapo vizuri kuliko hawa wanajeshi,
Kisa kingine kuna mshikaji anaendesha bajaj hapa maeneo ya Mwenge,basi kuna siku anavuka tu barabara bila bajaji kuna gari ya wanajeshi walikuwa wawili wakampelekea mshikaji anaevuka kwa miguu zima zima,sasa yule mshikaji kuona anataka kugongwa na lile gari si akamind na wale wajeda wakamind mjeda mmoja akashuka kumfuata mshikaji,anataka kumkamata mshikaji bahati mbaya ikamtoka ngumi bhana ikampata yule mjeda usoni,bahati nzuri kabla ugomvi haujaendelea watu tukajaa tukawaamua wasipigane,yule mshikaji akapata upenyo akakimbia kumbe wale wanajeshi wakauliza wakaambiwa kuwa yule mshikaji anapaki bajaj pale Mwenge,kesho yake wakaja watatu wakamkuta mshikaji wakamchukua mpaka kwenye uwanja wa vinyago pale Mwenge huwa wanacheza mpira,wakaanza kumuogesha matope mshikaji bhana,kumbe pale kuna mkubwa wao akawauliza inaama huyu mtu aliepigana na mwanajeshi ndio huyu?embu muachane aondoke zake mnalidhalilisha jeshi tu,maana huyo mshikaji ukimuona ni mwembamba kichizi.mshikaji karudi kijiweni kalowa tope mwili mzima.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Haya hufanywa na askari wadogo tu
 
Mimi nimesoma shule ya jeshi pale jitegemee jkt mgulani.
1. kuna siku moja kuna captain × alinichapa bakora nne kisa ninamzidi urefu! Yani alikuwa anafundisha nikamwambia sir naomba ruhusa niende chooni! Yani hapo hapo akabadilika kabisa, ety kwann unanizidi urefu alafu mimi nina nyota tatu???

Mzee zilitembea bakora, kuanzia siku hiyo nilikuwa namshangaaa sana yule afande.

02.Tukio la pili ni siku ya kwanza kwenda pale shuleni! Ilikuwa form five!
Aisee kwanza nilienda shule saa mbili ahsubui, nikamkuta MP anaitwa MSENGI. Akaniweka bakora nne, huwezi amini day one.

Nikaanza kwenda mdogomdogo, kuna sehemu wanaita smart area hurusiwi kutembea yani unatakiwa kupita nduki.. sikuwa najua.
Alooo alikuwa afande mmoja anaitwa kiyarunzi ni coplo hapo hapo nilikula bakora sita.

Aisee nikaanza kuona hii shule sio machozi yananilenga, huyo mdogomdogo mpaka class.
Kufika class namkuta captain shemahonge anafundisha kwa machungu nikagonga mlango mfululizo akasema unatutukana akampigia afande dani akaja mbio na bakora nne.akamwambka huyo kaja hapa anatukana

Mpige sjta....huwezi amini nikasema nikitoka humu ndani sirudi tena.. nikala sita kila mtu ananishangaaa nalio kisa mboko sita.

Nikaingia class nakakutana na wana nikawaadisia msanga.basi saa nne ikafika tukaenda canteen.

Sasa mwisho wa kuingia canteen na kutoka ni saa nne na nusu.
Mimi nilikuwa nakunywa supu mpaka saa nne na 40 aloooooh

Nilipigwa bakora za mgongo nikamwaga supu mbio nikasema huu ni usenge..nkasepa class
Nashukuru Mungu sikifuata.

Siku ya kwanza nilipigwa zaidi ya bakora 16
Afandeeee K
Arando

Kuna siku ilikuwa ni mida ya kutoka sasa, ni jioni saa 11 nikakatiza pale Smart Area nikapaona peupe pee nikajua hakuna watu, nikaanza kutembea kiboss.
Kumbe bwana kuna watu nyomi wameshikwa wapo nyuma ya ofisi kwa kosa la kutembea na sio kukimbia. Ile kukatiza tu nakuta naitwa "Wee kuja hapa" ile kwenda tu nakuta watu nyomi wanapihishwa push up.
Aisee nilikoma.
2017 hiyo
 
Mimi sikubaligi upumbavu, huyo mwanajeshi mshamba na njaa Kali angekuja kwangu aone, ningevomjibu dry sitishiwi bunduki Mimi, Wala sitishiwi kifo hata siku moja

Angeenda ailete hata Kambi nzima, siogopagi kufa Mimi, liwalo na liwe na ndo wangejua kweli hii Dunia kuna watu watata, sio Dunia, Tanzania kuna watu watata. Mimi ndio MWAMBA.
Bangi haijawahi mwacha mtu salama
 
Back
Top Bottom