Adhabu za wanajeshi

Adhabu za wanajeshi

Afande akileta upuuzi huo unamgomea tu, maana ni kinyume cha maadili ya kazi za jeshi. Hawezi kukufanya lolote. Hawezi kukuua na kama Akikudhuru unamfikisha kwa wakubwa wake tu , uone kama kibarua chake hakijaota nyasi.

Tatizo watu hawajui haki zao na wanaogopa magwanda. Lakini nidhamu za kijeshi zinakataza kabisa askari kuonea raia.
Wewe waongopee wenzio,Pale Twalipo kuna kibao kabisa kinazuia wenye magari wasizibe geti,ukiziba ni lazima adhabu ndogo ndogo kama hizo zikupate,wadanganye wenzio wagome wapate adhabu kubwa. wanajeshi wanakera sana Mie niliwahi kuvaa koti la jeshi kiomboi nikijua hakuna wanajeshi kule ntakuwa salama,nikakutana na mwamba yupo likizo.
 
Wewe waongopee wenzio,Pale Twalipo kuna kibao kabisa kinazuia wenye magari wasizibe geti,ukiziba ni lazima adhabu ndogo ndogo kama hizo zikupate,wadanganye wenzio wagome wapate adhabu kubwa. wanajeshi wanakera sana Mie niliwahi kuvaa koti la jeshi kiomboi nikijua hakuna wanajeshi kule ntakuwa salama,nikakutana na mwamba yupo likizo.
Hebu nikuulize, ukigomea adhabu hizo za kihuni, wanajeshi wanakufanya nini?, wanakuchoma kisu?, wanakupiga mangumi?, wanakuua?
 
Hebu nikuulize, ukigomea adhabu hizo za kihuni, wanajeshi wanakufanya nini?, wanakuchoma kisu?, wanakupiga mangumi?, wanakuua?
Unaweza kupata fedheha mkuu,wanashindwa kukumwagia ndoo ya maji? au kukuburuza kwenye mtaro wa maji machafu kinguvu? Si heri ushukie dirishani yaishe.
 
We jidanganye, kwa taarifa yako hayo yana badaka za wakubwa hayo.
Unataka kuniambia mnadhimu wa Jeshi la JWTZ amebariki uvunjaji wa sheria na katiba ya nchi?- Hakuna kitu kama hicho. Ukiamua kukomaa unakomaa nao kwelikweli hadi kuhakikisha hiyo ishu inafika mbali.
 
Unaweza kupata fedheha mkuu,wanashindwa kukumwagia ndoo ya maji? au kukuburuza kwenye mtaro wa maji machafu kinguvu? Si heri ushukie dirishani yaishe.
Sasa wakikuburuza chini hiyo ndo violence yenyewe ambayo itawacost.
Unakumbuka wale maofisa wa jeshi la uhamiaji walioagiza raia agalegale chini live kwenye camera kisa eti ni kishoka wa passport, unakumbuka jeshi la uhamiaji lilivyolaani ujinga wao?- Kuna taarifa kuwa maafande wale walipewa adhabu za kinidhamu.
 
Mimi nimesoma shule ya jeshi pale jitegemee jkt mgulani.
1. kuna siku moja kuna captain × alinichapa bakora nne kisa ninamzidi urefu! Yani alikuwa anafundisha nikamwambia sir naomba ruhusa niende chooni! Yani hapo hapo akabadilika kabisa, ety kwann unanizidi urefu alafu mimi nina nyota tatu???

Mzee zilitembea bakora, kuanzia siku hiyo nilikuwa namshangaaa sana yule afande.

02.Tukio la pili ni siku ya kwanza kwenda pale shuleni! Ilikuwa form five!
Aisee kwanza nilienda shule saa mbili ahsubui, nikamkuta MP anaitwa MSENGI. Akaniweka bakora nne, huwezi amini day one.

Nikaanza kwenda mdogomdogo, kuna sehemu wanaita smart area hurusiwi kutembea yani unatakiwa kupita nduki.. sikuwa najua.
Alooo alikuwa afande mmoja anaitwa kiyarunzi ni coplo hapo hapo nilikula bakora sita.

Aisee nikaanza kuona hii shule sio machozi yananilenga, huyo mdogomdogo mpaka class.
Kufika class namkuta captain shemahonge anafundisha kwa machungu nikagonga mlango mfululizo akasema unatutukana akampigia afande dani akaja mbio na bakora nne.akamwambka huyo kaja hapa anatukana

Mpige sjta....huwezi amini nikasema nikitoka humu ndani sirudi tena.. nikala sita kila mtu ananishangaaa nalio kisa mboko sita.

Nikaingia class nakakutana na wana nikawaadisia msanga.basi saa nne ikafika tukaenda canteen.

Sasa mwisho wa kuingia canteen na kutoka ni saa nne na nusu.
Mimi nilikuwa nakunywa supu mpaka saa nne na 40 aloooooh

Nilipigwa bakora za mgongo nikamwaga supu mbio nikasema huu ni usenge..nkasepa class
Nashukuru Mungu sikifuata.

Siku ya kwanza nilipigwa zaidi ya bakora 16
😂😂😂 nimecheka kama mazur,ww naye inaonekana mvivu mvivu
 
Mie mwenyewe sikubali mtu anizalilishe kisa eti ni mjeda na Kuna wajeda wengine huzalilisha Hadi watu umri wa kuwazaa kabisa eti kisa mjeda. Jamani Mimi sifanyi adhabu yoyote tuone ka wataniua
We wanaweza kukutembezea miti kabisa na ushirikiano ukautoa.
 
Jw hana maajabu kutana magereza kwenye 18
pale goms kuna kambi ya jeshi,sasa kuna jamaa mmoja alikutwa juu ya mnazi akiangua nazi!!! akaambiwa ashuke alaf akaulizwa kwa nini anafanya ivo akajibu kwamba ni njaa tu inamsukuma!!!,,,basi akapelekwa kambini alaf akapewa supu kaama sufuria kubwa kabisa,,,,,,akala mpaka akashindwa,akalazimishwa amalize,,,jamaa alikomaa mpaka akamaliza,alipoamaliza akaambiwa avue nguo zote alaf aruke kichurachura,,,,,lahaula!!!!!.....jamaa kila akiruka akawa anashuksha kifusi cha kinyesi
 
Wewe unajua nini ulichoandika kipo kwenye CPA na imeelezwa vizuri Kanuni ya Adhabu pia imeelezea adhabu zipi zitolewe kwa wanaoenda kinyume na sheria zilizowekwa kwa ulinganifu na CPA, unapoelezea sheria ujue na statue zake sio kukariri tu kwenye Kibanda Cha kashata na kahawa ukisikia hili umenasa km sumaku

CPA ni Criminal Procedure Act [R.E 2002]

Nisije nikawa nakuchanganya ubongo
Mbona unajikanyaga kanyaga tu lakini hueleweki unandika nini au unataka tujue kuna neno linaitwa CPA unalijua? Sasa lina maajabu gani? CPA kwa kiswahili ni sheria ya mwenendo wa makosa ya jidai unang'ang'ania tu CPA R.E 2002
Sasa CPA hiyo ya 2002 imefanyaje? Maana Revised Edition ipo hadi 2022na zote hakuna ambayo inamfanya raia akose haki zake
Kama zipo hizo sheria sema.

Kinacho kusumbua wewe ni ushamba na maneno ya vijiweni ila hauna unachojua, makosa yote ya jinai yanaamuliwa mahakamani na hakina sheria inayo mruhusu mwanajeshi atoe adhabu kwako, hizo adhabu wanapeana wao kwa wao huko kambini pindi wanapofanya makosa ya utovu wa nidhamu, wewe raia unatakiwa upelekwe mahakamani ndo sehem unayotakiwa upewe adhabu.

Adhabu yoyote anayotaka kukupa unaweza kukataa kuifanya ilimradi tu haujakataa kukamatwa na wakikukamata wanatakiwa wakukabidhi polisi huko ndo utaenda kufunguliwa mashtaka na siyo wao kukupiga au kukudhalikisha, huyo dereva alieambiwa ashukie dirishani alitakiwa akatae kushukia dirishani na hakuna kitu chochote ambacho angemfanya, kumuua hawezi Wala kumpeleka mahakamani hawezi maana hakuna kosa la jinai kusimama mbele ya kambi ya jeshi kwasababu ya foleni na wakati serekali imepitisha barabara hapo.
 
Afande akileta upuuzi huo unamgomea tu, maana ni kinyume cha maadili ya kazi za jeshi. Hawezi kukufanya lolote. Hawezi kukuua na kama Akikudhuru unamfikisha kwa wakubwa wake tu , uone kama kibarua chake hakijaota nyasi.

Tatizo watu hawajui haki zao na wanaogopa magwanda. Lakini nidhamu za kijeshi zinakataza kabisa askari kuonea raia.

Unaleta Mgomo wa JamiiForums nenda live
 
Mimi sikubaligi upumbavu, huyo mwanajeshi mshamba na njaa Kali angekuja kwangu aone, ningevomjibu dry sitishiwi bunduki Mimi, Wala sitishiwi kifo hata siku moja

Angeenda ailete hata Kambi nzima, siogopagi kufa Mimi, liwalo na liwe na ndo wangejua kweli hii Dunia kuna watu watata, sio Dunia, Tanzania kuna watu watata. Mimi ndio MWAMBA.
Sawa Mwamba wewe Kibondo🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤗🤗🤗👋👋👋
 
Wajuaji Wenzio walipita eneo la jeshi pale Lugalo mida ya saa 12 jioni kigiza kimeshaanza kuingia,na Sheria ya like eneo halifuhusiwi watembea kwa miguu kukatiza mida mibovu(enzi hizo sijui siku hizi utaratibu upoje). Walikuwa wanapiga kigoma Cha Uruguay wakitokea kawe wanakatiza Lugalo wanaelekea kule juu makongo.

Walipofika mitaa ya Lugalo wakakutana na Askari wakaulizwa mnaenda wapi saa hizi,wakajibu makongo kwenye shughuli. Afande akawaambia sasa mnaonaje mngetuburudisha kidogo kabla hamjaondoka? Jamaa kwa sifa wakaona hakuna shida,kigoma kikapigwa.

Kigoma kikapigwa Hadi usiku,jamaa walipojisikia njaa wakapewa na msosi, wajomba wakawaambi endeleeni kutoa burudani. Wazee walipiga ngoma mpaka asubuhi hadi wakaanza kulia. Kesho take ndiyo waliachiwa wakiwa mikono imevimba kwa kupiga ngoma.

Ungekuwepo katika hili kundi ungezichapa?

Kipo mpk leo
 
Wajuaji Wenzio walipita eneo la jeshi pale Lugalo mida ya saa 12 jioni kigiza kimeshaanza kuingia,na Sheria ya like eneo halifuhusiwi watembea kwa miguu kukatiza mida mibovu(enzi hizo sijui siku hizi utaratibu upoje). Walikuwa wanapiga kigoma Cha Uruguay wakitokea kawe wanakatiza Lugalo wanaelekea kule juu makongo.

Walipofika mitaa ya Lugalo wakakutana na Askari wakaulizwa mnaenda wapi saa hizi,wakajibu makongo kwenye shughuli. Afande akawaambia sasa mnaonaje mngetuburudisha kidogo kabla hamjaondoka? Jamaa kwa sifa wakaona hakuna shida,kigoma kikapigwa.

Kigoma kikapigwa Hadi usiku,jamaa walipojisikia njaa wakapewa na msosi, wajomba wakawaambi endeleeni kutoa burudani. Wazee walipiga ngoma mpaka asubuhi hadi wakaanza kulia. Kesho take ndiyo waliachiwa wakiwa mikono imevimba kwa kupiga ngoma.

Ungekuwepo katika hili kundi ungezichapa?
👀👀🙄🙄😀😀😂😂🤣🤣🤣🤣 Jaman kweli kwa wenzetu yanachekesha ila yasitukute tu,nilivyo mvivu mvivu watanizika tu
 
Hawa Jamaa usiombe uingie kwenye 18 zao, utajuta kuwafahamu.

Siku moja Tulikuwa kwenye foleni ya kuelekea mjini, kuna jamaa wa Lori akaziba geti la kuingilia pale kambi ya Abdallah Twalipo uhasibu. MP akamfuata kistaarabu kabisa "mambo vipi Kaka?" Jamaa akaitikia "Safi kabisa afande". Afande akamuuliza hapa uliposimama si unajua Kama ni getini? Mwamba kwa kujiamini kabisa akaitikia ndiyo afande ila tatizo foleni haitembei, Sina jinsi, samahani sana.

Kama kawaida ya wanajeshi kujifanya wastaarabu kwenye matukio ya aina hii. Afande akamwambia sasa ndugu kwa kuwa foleni haiendi shuka tu hapa upumzike tupige stori, foleni ikitembea utaendelea na safari yako. Dereva wa Lori kwa mbwembwe akafungua mlango ashuke eti apumzike na wanajeshi. Hapo ndiyo 'ntiti' ulipoanza!!

MP akamwambia "kaka sijasema ushuke mlangoni, shukia dirishani" lilikuwa ni tukio la kuchekesha Sana kwa sisi wapita njia ila kwa lililomtokea lilikuwa ni tukio mbaya na la kufedhehesha.

Picha linaanza,gari anayoendesha jamaa ni Scania R 420,Chuma mpya kabisa ya Transit alafu imepanda hewani Kama farasi, imebeba mafuta inaelekea nje. Gari ikisimama dereva unamwona yule kuleee ghorofani. Sasa vuta picha dereva ameambiwa ashuke kupitia dirisha badala ya mlangoni. Sisi wengine wa pembeni Tulicheka Sana maana jamaa kwanza ni bonge alafu ili ashuke kwa kutumia dirisha inabidi ajikusanye awe Kama fungu la nyanya Kisha ndiyo atoe miguu nje. Ilimchukua karibia dakika 15 kushuka. Wakati huo MP alikuwa siriazi hacheki wala haongei. Yeye anamsubiri jamaa tu ashuke wapige stori. Dereva akadondoka chini Kama mzigo wa viazi mbatata vya Mbeya..Tiii!!

Suruali yote imechanika kwenye maungio ya miguu. Aliposhuka huku kijasho kinamtoka mjeda akaanza kupiga nae stori Kama hakuna kilichotokea "naona chuma imeshakunywa wese inasepa?" Dereva kinyonge akajibu yeah inaelekea Ndola, Zambia. Wakapiga stori Mara foleni ikafunguka magari yakaanza kutembea. Afande akamwambia dereva Sasa unaweza kwenda tu maana gari zinatembea. Dereva akatoa shukrani Kisha akaelekea kwenye gari yake asepe.

Cha ajabu wakati dereva anafungua mlango Mjeda akamwambia mzee baba si tulikubaliana tunapitia dirishani? Ahahahhaha kazi ya kupanda dirishani ikaanza tena. Nina uhakika Yule dereva alimtukana mjeda matusi yote ya hapa duniani ila kimoyomoyo.. Ile siku yule dereva hataisahau kamwe maishani.

Unakumbuka kisa chochote Cha wanajeshi na adhabu zao kwa raia pindi raia akijichanganya kwenye anga zao?
🤣🤣😂😂😂
 
Unaleta Mgomo wa JamiiForums nenda live
Tunatofautiana. Wewe wakikumata wakasema galagala chini kwenye tope watii, Sisi wengine hatuko tayari kutii ujinga huo , Watupige risasi kama wanataka!. Katika mazungumzo nao Tutakuwa tukiwakumbusha tu katiba ya nchi inasema nini juu ya haki za wananchi na wajibu wao kama askari kuwa jukumu lao kuu ni kuilinda katiba ya nchi.

Wakifanya uhuni hilo goma halitoishia hapo, litafika hadi kwa CDF AU MAHAKAMANI NO MATTER LITACHUKUA MUDA GANI
 
Mkuu nina watu tunafahamiana humu hawapungui 20 nikiongea uongo najiharibia...niamini huwa sina sababu ya kudanganya..
Rafiki ulitoka ukiwa na cheo gani huko
 
Mimi nimesoma shule ya jeshi pale jitegemee jkt mgulani.
1. kuna siku moja kuna captain × alinichapa bakora nne kisa ninamzidi urefu! Yani alikuwa anafundisha nikamwambia sir naomba ruhusa niende chooni! Yani hapo hapo akabadilika kabisa, ety kwann unanizidi urefu alafu mimi nina nyota tatu???

Mzee zilitembea bakora, kuanzia siku hiyo nilikuwa namshangaaa sana yule afande.

02.Tukio la pili ni siku ya kwanza kwenda pale shuleni! Ilikuwa form five!
Aisee kwanza nilienda shule saa mbili ahsubui, nikamkuta MP anaitwa MSENGI. Akaniweka bakora nne, huwezi amini day one.

Nikaanza kwenda mdogomdogo, kuna sehemu wanaita smart area hurusiwi kutembea yani unatakiwa kupita nduki.. sikuwa najua.
Alooo alikuwa afande mmoja anaitwa kiyarunzi ni coplo hapo hapo nilikula bakora sita.

Aisee nikaanza kuona hii shule sio machozi yananilenga, huyo mdogomdogo mpaka class.
Kufika class namkuta captain shemahonge anafundisha kwa machungu nikagonga mlango mfululizo akasema unatutukana akampigia afande dani akaja mbio na bakora nne.akamwambka huyo kaja hapa anatukana

Mpige sjta....huwezi amini nikasema nikitoka humu ndani sirudi tena.. nikala sita kila mtu ananishangaaa nalio kisa mboko sita.

Nikaingia class nakakutana na wana nikawaadisia msanga.basi saa nne ikafika tukaenda canteen.

Sasa mwisho wa kuingia canteen na kutoka ni saa nne na nusu.
Mimi nilikuwa nakunywa supu mpaka saa nne na 40 aloooooh

Nilipigwa bakora za mgongo nikamwaga supu mbio nikasema huu ni usenge..nkasepa class
Nashukuru Mungu sikifuata.

Siku ya kwanza nilipigwa zaidi ya bakora 16
 
Naona mnajifagilia siku hizi hatuwashobokei ni wa kawaida sana,,,migwanda tu mpaka mashoga wapo jeshini cku hz,,,vijana wengi wengi saizi unfit jeshi limekuwa ajira kama ajira nyingine
khaaaah
 
Back
Top Bottom