Adhabu za wanajeshi

Adhabu za wanajeshi

Mataifa ambayo yana amani ndio utasikia hizi habari za adhabu Kali za RAIA kutoka kwa wanajeshi na hii ni sababu watu wamekuwa trained mda mrefu mambo ya kivita na bila kuiona vita yenyewe kwa hiyo watu wanakuwa na kihemu hemu cha demonstrate waliyojifunza .Dawa pekee ya kuondoa hii ni serikali kuhakikisha wanajeshi wenye balehe ya uwanajeshi wanashiriki utunzaji Wa amani katika katika mataifa yenye machafuko ya kisiasa.
 
Mataifa ambayo yana amani ndio utasikia hizi habari za adhabu Kali za RAIA kutoka kwa wanajeshi na hii ni sababu watu wamekuwa trained mda mrefu mambo ya kivita na bila kuiona vita yenyewe kwa hiyo watu wanakuwa na kihemu hemu cha demonstrate waliyojifunza .Dawa pekee ya kuondoa hii ni serikali kuhakikisha wanajeshi wenye balehe ya uwanajeshi wanashiriki utunzaji Wa amani katika katika mataifa yenye machafuko ya kisiasa.
Jeshini unapotoka mafunzoni kunakuwaga na kimuhe muhe flani na munkari wa kijinga, usipojizuia unaweza kuleta madhara uraiani hasa unapochokozwa.

Rafiki zangu wawili waliwahi fanya ukatili sana.
Mmoja alimkata kibaka vidole vya mkono.
Mwingine alimvunja kijana mtukutu mguu.
Lakini kwasasa ni wapole sana na wana rank...nzuri so wametulizana
 
Jeshini unapotoka mafunzoni kunakuwaga na kimuhe muhe flani na munkari wa kijinga, usipojizuia unaweza kuleta madhara uraiani hasa unapochokozwa.

Rafiki zangu wawili waliwahi fanya ukatili sana.
Mmoja alimkata kibaka vidole vya mkono.
Mwingine alimvunja kijana mtukutu mguu.
Lakini kwasasa ni wapole sana na wana rank...nzuri so wametulizana
Huo waliofanya huwezi kuuita ukatili kaka. Huyo vibaka na huyo kijana mtukutu huwezi kujua walitaka kumdhuru vipi huyo jamaa yako. Vijana watukutu na vibaka ni washenzi mno kwenye anga zao, ilikuwa ni haki yao kufanywa waliyofanywa. Usiuite ukatili mkuu.
 
Tanzania hadi ufungue kesi hio labda uende ukafungue kesi kwa kasimu bila hivyo unakusumbua tu, Mahakama inafanya kazi na Jeshi la Polisi usijifanye haujui, ushanielewa lakini au nikwambie tu ulichokiandika kipo kwenye CPA na kwenye Penal Code Ila wakikubanisha lazima wakuchangamshe damu kidogo ili uwe adabu siku nyingine usirudie kufanya ujinga, sawa na mama yako akwambie usichezee kiwembe hicho ukachezea kikakukata akiona umejikata anakuosha kwanza mabanzi ya sura km manne hivi au matano alafu ndio anakupa huduma ya kwanza ili siku nyingine usirudie kufanya ujinga wewe mtoto Mpumbavu, mwanajeshi ampi adhabu za kuchosha raia mtiifu, tembelea shule zilizo karibu na kambi za Jeshi asubuhi mtu km wewe wale watoto unaweza ukasema wanaonewa tena unaweza ukaingilia kati uwaambie jamàa waache kuwapigisha kwata wasiendelee kuburuzwa kwa kuwapigisha gwaride la kufanya kazi za usafi wa shule asubuhi asubuhi na baridi
Huna unachojua usijidai mjuaji
 
Ilitokea wapi hii brother?
Screenshot_20230510-091229_Opera Mini.jpg
 
Huo waliofanya huwezi kuuita ukatili kaka. Huyo vibaka na huyo kijana mtukutu huwezi kujua walitaka kumdhuru vipi huyo jamaa yako. Vijana watukutu na vibaka ni washenzi mno kwenye anga zao, ilikuwa ni haki yao kufanywa waliyofanywa. Usiuite ukatili mkuu.
Wewe kila kitu unabisha,ulipitia malezi mabaya,wazaz wako wanashida mahala
 
Mie mwenyewe sikubali mtu anizalilishe kisa eti ni mjeda na Kuna wajeda wengine huzalilisha Hadi watu umri wa kuwazaa kabisa eti kisa mjeda. Jamani Mimi sifanyi adhabu yoyote tuone ka wataniua
Ukigoma kupewa adhabu hawakufanyi lolote, maana watahisi wewe ni mzaliwa wa mjini, unajielewa na unafahamu haki zako na pengine unajua sheria kabisa.

So wataishia kukupiga piga mkwara fulani mwisho wa siku watakuacha uondoke kwa kukupa onyo kwamba siku nyingine usirudie kufanya kosa ulilolifanya siku hiyo.

Wakuja akiona gwanda tu anakimbilia kulia na kumshika miguu mjeda mwenyewe kwamba amsamehee, na mjeda akiona hivyo ana take advantage ya kumuonesha kwamba yeye ni nani kwa kumpa adhabu ambazo zipo kinyume na sheria.
 
Hawa Jamaa usiombe uingie kwenye 18 zao, utajuta kuwafahamu.

Siku moja Tulikuwa kwenye foleni ya kuelekea mjini, kuna jamaa wa Lori akaziba geti la kuingilia pale kambi ya Abdallah Twalipo uhasibu. MP akamfuata kistaarabu kabisa "mambo vipi Kaka?" Jamaa akaitikia "Safi kabisa afande". Afande akamuuliza hapa uliposimama si unajua Kama ni getini? Mwamba kwa kujiamini kabisa akaitikia ndiyo afande ila tatizo foleni haitembei, Sina jinsi, samahani sana.

Kama kawaida ya wanajeshi kujifanya wastaarabu kwenye matukio ya aina hii. Afande akamwambia sasa ndugu kwa kuwa foleni haiendi shuka tu hapa upumzike tupige stori, foleni ikitembea utaendelea na safari yako. Dereva wa Lori kwa mbwembwe akafungua mlango ashuke eti apumzike na wanajeshi. Hapo ndiyo 'ntiti' ulipoanza!!

MP akamwambia "kaka sijasema ushuke mlangoni, shukia dirishani" lilikuwa ni tukio la kuchekesha Sana kwa sisi wapita njia ila kwa lililomtokea lilikuwa ni tukio mbaya na la kufedhehesha.

Picha linaanza,gari anayoendesha jamaa ni Scania R 420,Chuma mpya kabisa ya Transit alafu imepanda hewani Kama farasi, imebeba mafuta inaelekea nje. Gari ikisimama dereva unamwona yule kuleee ghorofani. Sasa vuta picha dereva ameambiwa ashuke kupitia dirisha badala ya mlangoni. Sisi wengine wa pembeni Tulicheka Sana maana jamaa kwanza ni bonge alafu ili ashuke kwa kutumia dirisha inabidi ajikusanye awe Kama fungu la nyanya Kisha ndiyo atoe miguu nje. Ilimchukua karibia dakika 15 kushuka. Wakati huo MP alikuwa siriazi hacheki wala haongei. Yeye anamsubiri jamaa tu ashuke wapige stori. Dereva akadondoka chini Kama mzigo wa viazi mbatata vya Mbeya..Tiii!!

Suruali yote imechanika kwenye maungio ya miguu. Aliposhuka huku kijasho kinamtoka mjeda akaanza kupiga nae stori Kama hakuna kilichotokea "naona chuma imeshakunywa wese inasepa?" Dereva kinyonge akajibu yeah inaelekea Ndola, Zambia. Wakapiga stori Mara foleni ikafunguka magari yakaanza kutembea. Afande akamwambia dereva Sasa unaweza kwenda tu maana gari zinatembea. Dereva akatoa shukrani Kisha akaelekea kwenye gari yake asepe.

Cha ajabu wakati dereva anafungua mlango Mjeda akamwambia mzee baba si tulikubaliana tunapitia dirishani? Ahahahhaha kazi ya kupanda dirishani ikaanza tena. Nina uhakika Yule dereva alimtukana mjeda matusi yote ya hapa duniani ila kimoyomoyo.. Ile siku yule dereva hataisahau kamwe maishani.

Unakumbuka kisa chochote Cha wanajeshi na adhabu zao kwa raia pindi raia akijichanganya kwenye anga zao?
Mjeda unafurahia jinsi mnavyowahenyesha raia.
 
Kumbe inawezekana kuwashtaki kunawale wa kututishia tidhia kutukosesha amani dawa Yao n ipi😀
Wanajeshi wengi huwa hawajui sheria atakunyanyasa akikutana na wewe ambae umelelewa kwenye misingi ya uoga uoga ila ukikomaa nae mwisho huwa wanaomba radhi na hata fidia unalipwa maana anajua kazi yake inaenda kuharibika

Kuna askri mmoja wa jwtz private ndugu yake aligongwa na pikipiki baada ya kugongwa na pikipik kesi ilienda hadi mahakamani kesi ikaisha kwa maamuzi ya mahakama lakini aliegongwa akawa bado anaendelea na matatibabu.

Jamaa huyo private wa jwtz akiwa likizo alichoamua kukifanya akiwa yupo likizo akaenda kumkamata yule jamaa aliemgonga ndugu yake na baada ya kumkamata akaenda kumfungia kwao hilo Ni kosa la kwanza alifanya kinyume na sheria(utekaji)

Kosa la pili akiwa anamuhoji akampiga yule jamaa akishinikiza kuwa jamaa amuhudumie mgonjwa wao hilo ni kosa la pili (shambulio la kudhuru mwili) kilichotokea hapo ni kuwa ndugu wa yule ndugu yao ambae amefanyiwa hivyo walikua wanajua haki zao wakakusanya ushahidi wote na mashahidi wakawepo ndugu yao alivyoaachiwa tu akiwa na majeraha wakaenda kuchukua pf 3 polisi ikaenda kuthibishwa na daktari kuwa jamaa kweli kashambuliwa na kapata madhara (hapa tayari shahidi wa 3 ambae ni daktari kapatikana)

Baada ya kutoka hospitali Sasa wakaenda kufungua kesi ya shambulio polisi kwakua ushahidi wote upo polisi ikabidi waende kumkatamta katika kumuhoji kumbe kweli alikua ni Askari wa jwtz, kilichotokea hapo taarifa ikatumwa kikosini kwake, utaratibu ulivyo ni kuwa Askari yeyote hapelekwi mahakama za kawaida kwa makosa ya jinai hadi kwanza apitie mahakama za kijeshi na afukuzwe kwanza kazi ndo apelekwe akiwa kama raia wa kawaida

Hali ilipofikia hapo na ndugu wa yule mwanajeshi wakaona kibarua cha mtoto wao kinaenda kuharibika ikabidi wajishushe wakaenda kuomba msamaha kwa yule alieshambuliwa wakabembeleza sana ili aifute hiyo kesi mwisho jamaa alikubali akapokea fidia lakini muda huo yule private wa jeshi kashakaa lockup ya polisi siku 6 maana utaratibu ilikua kikosini kwake ndo waje wamchukue lakin hawakuja kwa siku zote 6

Baadae kesi ilifutwa lakin Kama jamaa wangekomaa nae alikua anaenda kufukuzwa kazi kwasababu ameiingilia hadi mahakama kwa kesi ambayo ilishatolewa maamuzi,lakin pia alifanya makosa ya jinai kuteka na kushambulia

Sasa watu wanatakiwa wajue haki zao na siyo kutishwa tishwa wanakua Kama kondoo mwisho wa siku tunakua na taifa la wajinga
 
Afande akileta upuuzi huo unamgomea tu, maana ni kinyume cha maadili ya kazi za jeshi. Hawezi kukufanya lolote. Hawezi kukuua na kama Akikudhuru unamfikisha kwa wakubwa wake tu , uone kama kibarua chake hakijaota nyasi.

Tatizo watu hawajui haki zao na wanaogopa magwanda. Lakini nidhamu za kijeshi zinakataza kabisa askari kuonea raia.
We jidanganye, kwa taarifa yako hayo yana badaka za wakubwa hayo.
 
Akiwa Askari eneo la kazi na wewe umeenda ndivyo sivyo eneo hilo hata kesi ifike wapi hakuna litakalofanyika
 
Nyumbu na Msangani malori ya mchanga yalimamishwa na mp halafu dereva akaambiwa amwage mchanga 2ote halafu aujaze kwenye gari kwa viganja vya na mwingine akaambiwa amwage halafu aendeshe gari mita 50 halafu arudi kuchota mchanga koleo 1 akamwage mita 50 mpaka uishe....aliishiwa mafuta ndo akaruhusiwa kuondoka
Sa kilometa 50 sinaishilia huko huko ata hivyo mi sifanyi nawaambia nipelekeni mahakamani kama hamtaki niueni mnile na nyama kabisa
 
Askari wa Tanzania wengi - ingawa sio wote- hawana adabu, wanapenda kutumia uaskari wao kuonea watu.

Hizi habari zinanikumbusha mbali sana.

Kuna siku tulikuwa tumekaa maskani Upanga, muda wa jioni vijana wanakutana maskani. Mara paap, tukawa tumeaona askari kibao wanakuja kutoka mbali, wako doria kundi zaidi ya ishirini, wamebeba bunduki na marungu.

Basi nikawaambia madogo tuliokuwa tumekaa nao maskani, kama hamjiamini, ondokeni kabisa, wale wanakuja kutaka kututingisha hapa.

Basi kuna madogo wakaondoka, wengine tuliojiamini tukabaki.

Wakaja wakafika maskani, sisi kama kumi, wao zaidi ya ishirini. Mmoja akatuuliza "Haroo, mnafanya nini hapa?".

Basi hawakujua wanaongea na watu wa aina gani, jamaa mmoja wa maskani akamjibu "Afande hivyo ndivyo ulivyofundishwa kusalimia watu?". Ikabidi yule askari astuke kwanza. Alitegemea watu wataogopa, hakutegemea kujibiwa vile.

Sasa akaja askari mmoja, nafikiri ndiye alikuwa mkubwa wao yule, akaanza kuuliza watu, mmoja mmoja, "Wewe unakaa wapi?" Mtu anamwambia hapo, "Wewe unakaa wapi?" Mtu anamwambia hapo. Wakamfikia jamaa mmoja.Wakamuuliza "Wewe unakaa wapi?" Akajibu kwa Baba Ben.

Askari akauliza, "Kwa Baba Ben? Baba Ben gani?" Jamaa akajibu "Kwa Ben huyo huyo wa Jamhuri ya Muungano, kwani wewe unamjua Ben gani mwingine Tanzania?" (Hapo kipindi cha urais wa Ben Mkapa).

Yule Polisi akawa kastuka, kama hajaamini hivi, sasa kumbe kuna wenzake huwa walikuwa wanaenda kulinda kwa Mkapa, wakawa wamemjua yule kijana wa kwa Mkapa. Ikawa kama wanamwambia yule mkubwa wao kwamba huyu tunamjua anakaa kwa Mkapa, tunamuona tukienda kulinda pale.

Basi hapo hapo nikaona wale polisi wanabadilika mara moja, wanasema unajua wazee ni suala la kufahamiana tu, tulikuwa tunajuana tu, hamna tatizo, hamna tatizo tulikuwa tunatambuana tu.

Kuanzia siku hiyo mpaka kituoni kwao kile kijiwe walikiwekea alama ya X kisiguswe, wakasema hapa kuna watoto wa Mkapa huwa wanakaa.

Nikasema hapa ingekuwa wamewakuta watu wasio na majina wangewasumbua sana.
Kingekuwa kijiwe cha kawaida siyo wangesumbuliwa tu Kama ulivyoandika,bali pia wangewekewa Hadi vipisi vya bangi mifukoni na mitama wangechezea na kwenye difenda mngepanda.

Mimi nilishawahi kuchanganywa kwenye kundi la wazurulaji kisa tu nilikuwa napita njia naelekea stendi,huko chochoroni polisi wakawakurupusha wahuni,ile kimbizana wakamchanganya kila mtu waliyekutana naye mbele Hadi mpita njia,Mimi nikiwemo. Ile siku nilimind vibaya mno,nikakunjana na Askari ila akaja afande mmoja akasema "afande sogea nimshuti huyo jambazi aliyetuvamia tusifanye kazi yetu". Nikawa mpole na mikono juu ila jamaa hakuridhika,akanitia kibao Cha sikio shadi nikawa sisikii.

Ile siku nililala chang'ombe polisi nikaja kutolewa asubuhi na fine 50k ya uzurulaji. Askari wa bongo waonevu na wanateteana Sana,nashangaa wanaopigizana kelele humu eti sababu wabongo hatujui haki,Askari akikuletea za kuleta unamchukulia hatua za kisheria.
 
Nenda kauze Vitumbua Jeshini..Alafu uviite vitumbua vya kijeshiAu jeshi lenye vitumbua..Utakuja kusimulia hapa
 
Kuna jamaa alitaka kuovertake msafara wa wajeda barabara ya Iringa~Dar, kabla hajamaliza kuyapita magari yao mbele gari ikatokea ikabidi abane katikati ya wajeda. Aloo walimwambia nae Kawa part ya msafara wao Hadi DSM wakati jamaa alikua anaishia Moro.
Nimecheka Sana asee.
 
Huna unachojua usijidai mjuaji
Wewe unajua nini ulichoandika kipo kwenye CPA na imeelezwa vizuri Kanuni ya Adhabu pia imeelezea adhabu zipi zitolewe kwa wanaoenda kinyume na sheria zilizowekwa kwa ulinganifu na CPA, unapoelezea sheria ujue na statue zake sio kukariri tu kwenye Kibanda Cha kashata na kahawa ukisikia hili umenasa km sumaku

CPA ni Criminal Procedure Act [R.E 2002]

Nisije nikawa nakuchanganya ubongo
 
Ukigoma kupewa adhabu hawakufanyi lolote, maana watahisi wewe ni mzaliwa wa mjini, unajielewa na unafahamu haki zako na pengine unajua sheria kabisa.

So wataishia kukupiga piga mkwara fulani mwisho wa siku watakuacha uondoke kwa kukupa onyo kwamba siku nyingine usirudie kufanya kosa ulilolifanya siku hiyo.

Wakuja akiona gwanda tu anakimbilia kulia na kumshika miguu mjeda mwenyewe kwamba amsamehee, na mjeda akiona hivyo ana take advantage ya kumuonesha kwamba yeye ni nani kwa kumpa adhabu ambazo zipo kinyume na sheria.
Mie nimekosea sitaki kuzalilishwa waniadhibu kiutaratibu na ikiwa mwanaume namgeuzia kesi kabisa yakutaka kunibaka kabisa.
 
Back
Top Bottom