Adhabu za wanajeshi

Adhabu za wanajeshi

Kuna mjeda mmoja pale maeneo ya Mwenge alimpush muuza machungwa na gari lake,sasa badala awe mpole si akataka kuleta utemi bhana,sasa alikuwa kavaa kiraia,si akaanza kufoka foka pale watu wote wanaogopa,kuna jamaa akaja akaanza kubishana nae,bahati mbaya yule mjeshi akamkunja yule jamaa,basi jamaa akampiga teke yule mjeda akaanguka chini,watu wakaamulizia,cha kushangaza yule mjeda kesho yake kaja na wenzake watano wanamtafuta jamaa wampige,yule mwamba wiki nzima hakutokea yale maeneo.ushauri wangu kama wewe ni mjeda na umeleta ukorofi mtaani ukachapika maliza mwenyewe,sio unapigwa na mtu mmoja alafu wewe unaenda kuleta kikosi kwa ajili ya kumpiga mtu mmoja.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Mimi sikubaligi upumbavu, huyo mwanajeshi mshamba na njaa Kali angekuja kwangu aone, ningevomjibu dry sitishiwi bunduki Mimi, Wala sitishiwi kifo hata siku moja

Angeenda ailete hata Kambi nzima, siogopagi kufa Mimi, liwalo na liwe na ndo wangejua kweli hii Dunia kuna watu watata, sio Dunia, Tanzania kuna watu watata. Mimi ndio MWAMBA.
Mwamba kavimba nyuma ya keyboard au sio ?
 
Pale Gogoni/Kiluvya upande wa pili Kuna kambi ya jeshi. Sasa karibu na pale Kuna jamaa alituambia anauza viwanja kwa Bei poa. Basi tukajikusanya ili tukaonyeshwe mipaka kumbe eneo Ni eneo la jeshi. Basi hatuna hili Wala lile wakaja baka baka kuuliza mbona tuko pale? Tukamjibu tumekuja kununua viwanja, mjeda akasema, mtatapeli maana hapa Ni eneo la jeshi. Tukamuambia no problem hatukujua. Basi skawaita ma MP na juwaambia Hawa jamaa walitaka kutapeeliwa, hebu waonyesheni mipaka ya eneo la jeshi. Basi zoezi likaanza kuzunguka Ile kambi. Tulianza Kama tunakwenda Mloganzila, tukapita usawa wa Mloganzila, jua nalo limepamba Moto, mpaka kuzunguuka Ile kambi kwa mguu Ni zaidi ya masaa manne.
 
Jaribu uende kuleta ujuaji wako, utasimulia hadi wajukuu kitakachokupata. Wanajeshi epuka sana akiwa yupo eneo la kazi na hapo ulimkuta alipangiwa jukumu fulani, kazi ikiharibika anaadhibiwa na kuliko litokee hilo ndiyo anakuzingua. Kama huyo wa lori aliyekutana na MP, wale kituo chao cha kazi ni hapo getini kama angekutwa na wakubwa geti limezibwa hivyo angezinguliwa na ndiyo hapo aliamua kumzingua yeye.

Cheza na mwanajeshi sehemu zingine zote ila si eneo lake la kazi, wanaadhibiwa adhabu mbaya sana wale jamaa au kutukanwa kabisa na wakubwa kama mambo yakienda hovyo
Hao wanajeshi unawachulia kama kina nani???unadhani wakikuta mtu anajielewa watamzingua??

Utazinguliwa ukiwa hujielewi tu.
 
Mimi Nina msimamo sitishiwi nyau, ukishaanza kigugumizi ndo wanakuchukulia poa, mwanaume ongea straight Kwa kujiamini na kunguruma kama simba, ikiwezekana unawatandika na maswali mpaka waone hii kichwa sio nyenzetu hii Wala sio ya kuchezea. Kudadeki mbona na salute wangenipigia.
Haujakutana nao kwenye himaya yao aisee nenda kanye kambini pale uonekane unakunya ndio utaeleza vizuri unayoyaeleza, unafikiri wanakusubisha bila sababu
 
Hao wanajeshi unawachulia kama kina nani???unadhani wakikuta mtu anajielewa watamzingua??

Utazinguliwa ukiwa hujielewi tu.
Hawakuzingui bila sababu wao sio vichaa, kambini usinye eneo la Jeshi usizingue eneo la Jeshi ile ni himaya yao ukizingua watakuosha tu, alafu nenda kashtaki ukiwa na kasimu mkononi
 
Mimi sikubaligi upumbavu, huyo mwanajeshi mshamba na njaa Kali angekuja kwangu aone, ningevomjibu dry sitishiwi bunduki Mimi, Wala sitishiwi kifo hata siku moja

Angeenda ailete hata Kambi nzima, siogopagi kufa Mimi, liwalo na liwe na ndo wangejua kweli hii Dunia kuna watu watata, sio Dunia, Tanzania kuna watu watata. Mimi ndio MWAMBA.
Usichokijua kuhusu hawa watu wao hawakupigi ili wakuuwe na wana nidhamu ya ajabu kuhusu silaha,usitegemee akushikie bunduki hata kiwembe tu hawakushikii huwa wanachotaka wao nidhamu izingatiwe na hata uwe mkorofi vipi wewe mbele yao ni mchumba tu,na wanaweza kuwa na njaa lakini hela yako hawachukui.

Usije siku ukakutana nao ukawajibu hovyo ukitegemea watakupiga ili wakuuwe nduguzo wakafungue jalada,hao utapewa adhabu mbalimbali ukitoka hapo wiki nzima kuna vitu hutaweza kuvifanya kama ulivyozoea.

Nina jamaa yangu tulivuka maji tukaenda Kigamboni na Starlet yake ina music mkubwa kuna kambi ipo sehemu inaitwa kitu kama Longoni au Ulongoni kuna kambi ya wanajeshi sasa tukapita pale sauti ipo juu,hatukujua walipotokea walitupeleka kwenye mess yao kikaletwa kindoo litre kumi kimejaa ubwabwa jamaa wakatuzunguka wakasema nanukuu "tunakunywa bia moja moja zikiisha hamjamaliza tunaleta ya litre 20 zingine"

Wakashauri atakaeshiba apige push ups ili chakula kijisage aendelee kula,cha kushukuru jamaa walikuwa wameshalewa na jamaa yangu nae alikuwa dizain amelewa so akili za kilevi zikakutana adhabu haikuzingatiwa sana,jamaa hupenda ukiwa mtiifu wanakuacha ukijifanya much know utaiva.
 
Afande akileta upuuzi huo unamgomea tu, maana ni kinyume cha maadili ya kazi za jeshi. Hawezi kukufanya lolote. Hawezi kukuua na kama Akikudhuru unamfikisha kwa wakubwa wake tu , uone kama kibarua chake hakijaota nyasi.

Tatizo watu hawajui haki zao na wanaogopa magwanda. Lakini nidhamu za kijeshi zinakataza kabisa askari kuonea raia.
Umeingia kwenye 18 zao, halafu uendelee kujikubali sijui sheria itakulinda, haloo we jamaa temea chini siyo juu, omba yasije kukukuta, utarudi kuja kufuta hii comment yako.
 
Hawakuzingui bila sababu wao sio vichaa, kambini usinye eneo la Jeshi usizingue eneo la Jeshi ile ni himaya yao ukizingua watakuosha tu, alafu nenda kashtaki ukiwa na kasimu mkononi
Nyinyi ndo mnqfanya upuuzi kuwanyenyekea,hao ni washkaji na ndugu tuko nao
 
Nyinyi ndo mnqfanya upuuzi kuwanyenyekea,hao ni washkaji na ndugu tuko nao
Nenda kanye pale eneo la Jeshi Lugalo, tena kunya kwenye lami ndio utawaonyesha ukichaa wako ulipoishia
 
Mimi Huwa napita lugalo mara nyingi nikitembea sijawahi kupewa adhabu sana huniuliza naenda wapi Hadi maafande wamekuwa rafiki acheni uoga wa wajeda
Hawakuzingui km hujazingua, pita Lugalo nenda kwenye zile bustani za pembeni vua sketi yako mwaga kojo alafu jamaa wakuone hakikisha wamekuona
 
Wapi kisonga makongo secondary school Sikusahau mzee baba ulinipiga banzi mmoja siku ya kupiga picha za passport
Mzee wangu stivu utakuw umestaafu sasa ulitusumbua sana kwenye joro
 
Sasa mimi kwanini ninye??

Hivi from no where tu waje waanze kunizingua ntakaa nawaangalia??

Sisi wabongo ni wapuuzi sanaa.
Hawakuzingui km hujazingua kua muelewa, na wanakua na molari sana sana ukiwazingua kambini au eneo lao la Jeshi ukiwa ndani ya eneo la Jeshi, nje unaweza hata umtukane au umtemee mate na asikufanye kitu, nenda eneo la Jeshi kamfanyie hivyo akupe fundisho
 
Hawa jamaa ni shida Kuna siku jamaa yangu alijichanganya huko kambini akapewa adhabu ya kuhamidha tofali 500 kuxitoa upande mmoja ma kuxipeleka upande mwingine akapambana na kuweza kuhamisha tofali 350 huku jasho likiwa limemtoka gafla akaonana na ndugu yake ambae ni mjeda na ana cheo kikubwa akamwelezea kosa na adhabu aliyopatiwa akawa anamuomba msaada huyo mjeda akasema nitakusaidia usijali hebu rudisha hizo tofali ilipozitoa nafikiri tatizo litakuwa limeisha! Da jamaa aliishiwa pozi
Daah sema sisi wabongo kwa story za vijiweni tuko vizuri hiyo story naisikia nahisi hii mara ya hamsini, watu wengi wanasimulia either wao au rafiki zao ndio yaliwakuta na kila mtu huweka idadi yake hapo kwenye matofali, eti jamaa yako daah
 
Afande akileta upuuzi huo unamgomea tu, maana ni kinyume cha maadili ya kazi za jeshi. Hawezi kukufanya lolote. Hawezi kukuua na kama Akikudhuru unamfikisha kwa wakubwa wake tu , uone kama kibarua chake hakijaota nyasi.

Tatizo watu hawajui haki zao na wanaogopa magwanda. Lakini nidhamu za kijeshi zinakataza kabisa askari kuonea raia.
Huo ulikuwa utemi wa kizamani sana.
 
Back
Top Bottom