Adhabu za wanajeshi

Adhabu za wanajeshi

Dogo acha ujinga we na huyo bro wako wazazi walipoteza ada wakapeleka ng'ombe shuleni unatoa mfano wa bro wakati mimi binafsi nimeshawaonya hao wanajeshi kufanya vitendo ambavyo viko kinyume na maadili ya jeshi na kuvunja sheria? Hivi unajua kosa lolote la jinai ikiwepo kumshambulia mtu ni kosa la kufukuzwa kazi kwenye majeshi ya ulinzi?

Sasa kawatishe wajinga wenzako mtaani usituletee utoto hapa
Akome kabisa
 
Rejea hiyo story yangu kisha mengine jiongeze. Huyo bro wangu alifanya kila ujanja, kilichomtokea hakisimuliki ww.
Jamaa baada ya kwenda kwa viongozi kaongezewa adhabu nyingine.
Haya mambo tuyaache tu
Nani alikuwa na kosa?
 
Kuna mjeda mmoja pale maeneo ya Mwenge alimpush muuza machungwa na gari lake,sasa badala awe mpole si akataka kuleta utemi bhana,sasa alikuwa kavaa kiraia,si akaanza kufoka foka pale watu wote wanaogopa,kuna jamaa akaja akaanza kubishana nae,bahati mbaya yule mjeshi akamkunja yule jamaa,basi jamaa akampiga teke yule mjeda akaanguka chini,watu wakaamulizia,cha kushangaza yule mjeda kesho yake kaja na wenzake watano wanamtafuta jamaa wampige,yule mwamba wiki nzima hakutokea yale maeneo.ushauri wangu kama wewe ni mjeda na umeleta ukorofi mtaani ukachapika maliza mwenyewe,sio unapigwa na mtu mmoja alafu wewe unaenda kuleta kikosi kwa ajili ya kumpiga mtu mmoja.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Huo unakuwa mshamba mkuu. Hawawezi man to man
 
Haujakutana nao kwenye himaya yao aisee nenda kanye kambini pale uonekane unakunya ndio utaeleza vizuri unayoyaeleza, unafikiri wanakusubisha bila sababu
Sasa kunya kambini si ni kosa kisheria? Kwa nini unye kambini?
 
Mungu aniepushe tu maana kiukweli watu tupo tofauti mioyo mimi sipendi kunyanyaswa hasa likija ni suala la fedhea ni bora uniue au unibebe ukaniulie mbali ila hakika hutoninyanyasa na Fedhea juu kisa kosa la kibinadamu tu.
 
Sitaki kukumbuka huo ufedhuli...zaidi aliutenda rafiki yangu.
Nakumbuka siku tunarudi kambini jioni tukiwa tumepakiana kwenye pkpk XL250.

Nyuma yetu tulifuatwa na lori la mchanga na juu yake walikuwa na vijana sita wakielekea kupakia mchanga.

Mbele yetu kulikuwa na beria ya kambi yetu ambayo hufanya ukaguzi wa magari ya kiraia.

Sasa sisi tulikuwa tunaendesha mwendo wa kawaida tu lkn lori lilikuwa na fujo na speed likitaka kutupita

Kwa vile tulikaribia hiyo beria hatukuwapisha...sasa vijana juu ya gari wakaanza kuporomosha mitusi kama ujuavyo wavuta bangi.

Kwa vile tulikuwa tunaongea kwa sauti kama ujuavyo mkiwa na pikpiki mnalazimika kuongea kwa sauti hatukuweza kusikia hayo matusi lkn askari aliyekuwa getini alisikia na tulipofika getini alusema...afande mbona mnatukanwa na hawa vijana wapuuzi?

Yule rafiki yangu kusijia vile aligeuka kichaa kwa hasira...

Geti likafunguliwa ile beria na kuamuriwa wapaki pembeni...
Wote wakaamuriwa kushuka pamoja na dereva wao.

Amri ikatolewa wavue mashati na suruali.

Wakaulizwa...hawa mnaowatukana mnawafahamu? Au kwa vile wamevaa kiraia?
Jamaa yangu akaruka juu ya mti akavunja tawi...

Ghafla wote wakapokea fimbo 6 kila mmoja mgongoni.

Akawaamuru walale chini kwenye kokoto
Na waviringike...daah jamaa walitokwa damu hadi niliwaonea huruma.

Ndani ya dakika 10 hawafai kutazama.

Niliingilia kati kuzuia kuendekea kuteswa kidogo tuzipige na jamaa yangu.

Mengine...yabaki tu
Una utu mno kaka. Hongera mno! Hao vijana hawakuonewa bali malezi yao mabovu kutoka kwa mama na baba zao ndiyo yaliyofanya waadhibiwe. Huo haukuwa uonevu.
 
Mimi nimesoma shule ya jeshi pale jitegemee jkt mgulani.
1. kuna siku moja kuna captain × alinichapa bakora nne kisa ninamzidi urefu! Yani alikuwa anafundisha nikamwambia sir naomba ruhusa niende chooni! Yani hapo hapo akabadilika kabisa, ety kwann unanizidi urefu alafu mimi nina nyota tatu???

Mzee zilitembea bakora, kuanzia siku hiyo nilikuwa namshangaaa sana yule afande.

02.Tukio la pili ni siku ya kwanza kwenda pale shuleni! Ilikuwa form five!
Aisee kwanza nilienda shule saa mbili ahsubui, nikamkuta MP anaitwa MSENGI. Akaniweka bakora nne, huwezi amini day one.

Nikaanza kwenda mdogomdogo, kuna sehemu wanaita smart area hurusiwi kutembea yani unatakiwa kupita nduki.. sikuwa najua.
Alooo alikuwa afande mmoja anaitwa kiyarunzi ni coplo hapo hapo nilikula bakora sita.

Aisee nikaanza kuona hii shule sio machozi yananilenga, huyo mdogomdogo mpaka class.
Kufika class namkuta captain shemahonge anafundisha kwa machungu nikagonga mlango mfululizo akasema unatutukana akampigia afande dani akaja mbio na bakora nne.akamwambka huyo kaja hapa anatukana

Mpige sjta....huwezi amini nikasema nikitoka humu ndani sirudi tena.. nikala sita kila mtu ananishangaaa nalio kisa mboko sita.

Nikaingia class nakakutana na wana nikawaadisia msanga.basi saa nne ikafika tukaenda canteen.

Sasa mwisho wa kuingia canteen na kutoka ni saa nne na nusu.
Mimi nilikuwa nakunywa supu mpaka saa nne na 40 aloooooh

Nilipigwa bakora za mgongo nikamwaga supu mbio nikasema huu ni usenge..nkasepa class
Nashukuru Mungu sikifuata.

Siku ya kwanza nilipigwa zaidi ya bakora 16
Mim na hiki kichwa changu 😂😂😂
 
Mtu yeyote anayekuonea na kukufedhehesha kwa makusudi, huyo naamini unatakiwa kufa naye kabisa, hatakiwi kusamehewa pasipo kuadhibiwa.
Huwezi amini kuna unafiki mtu anakutendea ubaya unacheka tu
 
Back
Top Bottom