ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

ni chizi tu ndo anayeweza kuiamini habari hii. kweli nimeamini kuna watu wengine wanaviwanda vya kutunga uongo.

Chanzo: Habari247

MYTAKE:
1) yaani mbwembwe zote zile za zitto na wenzake kuzunguka nchi nzima wameambulia wanachama 700 tu??? hata kura za kata moja hawajafikisha?? huu sasa utani....ndio maana zzk amekata tamaa na ziara ya pili???

2) Kwani kiongozi Mkuu zitto sialisema Ukawa ni wasakatonge??? na yeye anataka kujiunga na wasakatonge ???

3) Huyu mama sialisema "Nimarufuku Mwana Act kushabikia Ukawa"???

.....................
Professor kilaza.
 
Ukawa msiruhusu huo mchwa ujiunge nanyi. Mkiruhusu tu mjue habari yenu kwishney maana hao ACT ni pandikizi lenye malengo ya kusambaratisha na kuangamiza nguvu ya upinzani hapa tanzania.
 
Ukawa msiruhusu huo mchwa ujiunge nanyi. Mkiruhusu tu mjue habari yenu kwishney maana hao ACT ni pandikizi lenye malengo ya kusambaratisha na kuangamiza nguvu ya upinzani hapa tanzania.

Mbona CCM B(Cuf) wapo kwenye Ukawa!
 
Kusema kweli katika hili hata mimi ACT wamenishanga sana na sitosema uongo. Ni sababu gani hawa viongozi wa ACT hawakujiunga na vyama vingine ikiwa wanaamini katika UKAWA maana UKAWA sio Chadema pekee, walikuwa na option nne za kuwa washiriki wa UKAWA badala yake wakaenda wamefungua chama kingine? Kuna siri gani hapa ambayo pengine sisi wananchi hatuifahamu maana najaribu kupima kila njia za tafakari sipati jibu zaidi ya kwamba pengine huu ni mpango maalum.

Leo hii kundi zima la CCM na UKAWA wanajiongezea mafao japo yalokuwepo tu yanatutia wazimu wananchi kwa miaka. Tulitegemea pengine ACT itasimama imara kwa nia yake dhidi ya UNYONYAJI HUU wa viinua mgongo, sijui usumbufu, uhamaji kama kwamba wabunge hawa walikuwa wakiishi Dodoma. Leo ACT inakuja jiunga na kundi lile lile ambalo sisi wananchi tunataka kuona yanatokea mageuzi ya kweli juu ya mfumo huu kumbe ni yale yale!

ACT walianza vizuri sana lakini kama hakuna mpango maalum wa kisiasa juu ya kujiunga na UKAWA ambao sisi wananchi hatuujui isipokuwa viongozi wa UKAWA na ACT basi nimenawa mikono na siasa za Bongo....
 
muda ndo utasema kama ilivyokuwa kwa CUF......lazma kuwe na sababu ya kutuunganisha kwasasa bado hamna sababu ya kutuunganisha...sasa hivi kwa afya ya UKAWA ni lazima kutoiingiza mtu kama ACT na wafuasi wake ambao bado wanamatatizo na uuongozi wa CHADEMA.ni sawa kumkaribisha mzee wa wawi alieenguliwa CUF Hamad Rashid
 
Kuna watu wanashindwa kutoa maoni yao chanya kisiasa hapa jukwaani kwa kuogopa kutukanwa ama kuitwa Ndumilakuwili.

Ngoja niseme kidogo, kama nitamkwaza somebody then It's my Opinion.!

Watu wazima hukaa chini na kuzungumza, Ni mazungumzo Makini hayo ndiyo yaliyotuweka hapa Wanaukawa tukijadiri namna ya kumuondoa ccm madarakani. Kwa hali ya kisiasa ilivyokuwa hapo mwanzo, hakuna aliyewahi kudhani itakuwapo siku Cdm watakaa chini na Cuf kupanga mikakati mbalimbali ya ushirikiano ili kumwondoa ccm. Iko hivyo kwa Nccr dhidi ya Cdm Na hata NLD ambacho ni chama kidogo sana kisiasa dhidi ya Chama kikubwa kikuu cha upinzani Bungeni na Nchini kwa ujumla Chadema. Kilichofanyika hapa ni umakini wa watu wazima kuzika tofauti zao na kuangalia Malengo na Vipaumbele vyao. Wakajikuta wote kipaumbele na Malengo yao ni mamoja, kumuondoa mtu/chama kimoja kilichoshindwa kuongoza na kuendelea kung'ang'ania kutawala. Kwa kweli ni Mazungumzo Makini toka kwa Watu Makini dhidi ya Malengo Makini, ndiyo yaliyo yifikisha hapa. Na hiki ndicho tunachokihitaji kwa wakati huu.

Kama ni kweli hili limefanyika kwa ACT kutuma Maombi ya kujiunga UKAWA, ni vyema maombi yao yakatathiminiwa na hatimaye kukubaliwa. Katika kipindi hiki ni wazi UKAWA hawatakiwi kukosa hata kura moja, iwe ya Urais,Ubunge au Udiwani. Ni wakati wa kuzileta kura za Wapinzani wote dhidi watawala. Ni wakati tunaohitaji nguvu za uhakika na zile za ziada hata zile ambazo hatuna ili kuhakikisha kweli Ccm inaondoka madarakani kama kweli tuna nia ya dhati kumuondoa huyu Mkoloni mweusi.

Kwa hapa ilipo UKAWA, hakuna siri ambazo kwa hakika zikijulikana na ccm zitaweza kuleta madhala kwa umoja huo kiasi tuogope kuwaingiza ACT kwa hofu ya kuuza siri za Umoja huo kwa Ccm. Mpaka sasa hakuna propaganda yoyote itakayofanikiwa kuwatenganisha UKAWA itakayokubalika kwa wananchi. UKAWA mpaka sasa inawapiga kura wengi ambao hawako tayari kubadirishwa kwa lolote, hawa wanaitwa wafia chama. (UKAWA) Kinachofanyika hapa ni kuwashawishi wale ambao hawana misimamo rasmi na wale ambao ni Die hard Ccm. Wapo wale ambao ni die hard Zitto ambao licha ya uchache wao, kura zao ni muhimu sana. Mtu hata kama ulikuwa na Bilioni moja mtu akaja kukuongezea Milliom moja, pesa zako zitakuwa zimeongezeka kiasi cha kukuhakikishia maisha kwa siku kadhaa kulingana na maisha unayoishi.

Kwahiyo wakuu tusiwe na Misimamo mikali, isiyoyumba kwani mara kadhaa huwa haina faida. Kama hawa jamaa wamejitambua na kuomba kujiunga waruhusiwe na kupimwa nguvu zao ikiwezakana wapewe kulingana na nguvu zao hasa ukizingatia wamechelewa kujiunga. Iko wazi, mtu ukitokea somewhere na kukuta watu wanakula na ukakaribishwa chakula, utakula kulingana na pale ulipokikuta chakula hicho. Hapa pia Cdm,Cuf,Nccr na Nld wawe tayari kupunguza matonge kwaajili ya mgeni aliyefika.

Nirudie tena hii ni kama kweli ACT wametuma maombi hayo, maana awali walidai kutuma maombi, ilhali viongozi wa UKAWA wakidai hawajapokea maombi toka kikundi chochote cha siasa. Hapa ilionekana kama ni ACT kujaribu kununua huruma kwa wananchi kwa kigezo cha kukataliwa na Viongozi wenzao toka UKAWA.

Ni hayo tu wadau.

BACK TANGANYIKA
 
Mbona Cuf waliyowahi kuitwa CCM B wapo kwenye Ukawa?
muda ndo utasema kama ilivyokuwa kwa CUF......lazma kuwe na sababu ya kutuunganisha kwasasa bado hamna sababu ya kutuunganisha...sasa hivi kwa afya ya UKAWA ni lazima kutoiingiza mtu kama ACT na wafuasi wake ambao bado wanamatatizo na uuongozi wa CHADEMA.ni sawa kumkaribisha mzee wa wawi alieenguliwa CUF Hamad Rashid
 
Mbona Cuf waliyowahi kuitwa CCM B wapo kwenye Ukawa?
muda ndo utasema kama ilivyokuwa kwa CUF......lazma kuwe na sababu ya kutuunganisha kwasasa bado hamna sababu ya kutuunganisha...sasa hivi kwa afya ya UKAWA ni lazima kutoiingiza mtu kama ACT na wafuasi wake ambao bado wanamatatizo na uuongozi wa CHADEMA.ni sawa kumkaribisha mzee wa wawi alieenguliwa CUF Hamad Rashid
 
zitto muongo mkubwa alisema ziara iliingiza wanachama 6000+ kumbe 700 tu
 
muda ndo utasema kama ilivyokuwa kwa CUF......lazma kuwe na sababu ya kutuunganisha kwasasa bado hamna sababu ya kutuunganisha...sasa hivi kwa afya ya UKAWA ni lazima kutoiingiza mtu kama ACT na wafuasi wake ambao bado wanamatatizo na uuongozi wa CHADEMA.ni sawa kumkaribisha mzee wa wawi alieenguliwa CUF Hamad Rashid

Kwahiyo Chadema ndiyo wenye maamuzi wa nani wa kujiunga na Ukawa?
 
Napendekeza ACT Wazalendo ya ayatorah waungane kwanza na ACT Tanzania ya Limbu thenly ndio waje waungane na UKAWA
 
Chanzo: Habari247

MYTAKE:
1) yaani mbwembwe zote zile za zitto na wenzake kuzunguka nchi nzima wameambulia wanachama 700 tu??? hata kura za kata moja hawajafikisha?? huu sasa utani....ndio maana zzk amekata tamaa na ziara ya pili???

2) Kwani kiongozi Mkuu zitto sialisema Ukawa ni wasakatonge??? na yeye anataka kujiunga na wasakatonge ???

3) Huyu mama sialisema "Nimarufuku Mwana Act kushabikia Ukawa"???

.....................
Professor kilaza.

HUYO MWANAMKE ALIPOKUWA IRINGA AALISEMA ATAKAYE SHABIKIA UKAWA ATAFUKUZWA NDANI YA CHAMA. AU AMESAHAU? HUYO MFALME WAO ZITTO AKIWASILIANA KISIRI SIR NA WALE ANAOWAOMBA MIL 700 ILI KUFANYA ZIARA ZA KUGAWA WAPIGA KURA ANASEMA CHADEMA IS DYING. HALAFU WANASEMA WANAUNGA MKONO UKAWA. WANAFIKI WAKUBWA
hata kule makambako walichangisha hela kwenye mkutano wakaambulia TSH 6500
 
Kwahiyo Chadema ndiyo wenye maamuzi wa nani wa kujiunga na Ukawa?
sawa na huyo wa Hamad Rashid wa CUF atake kujiunga na UKAWA lazima CUF ndo itakuwa na busara kubwa ya kumkubali au kumkataa kwenye muungano huo
 
zitto muongo mkubwa alisema ziara iliingiza wanachama 6000+ kumbe 700 tu

mkuu hawa ili wapate wanachama 20000 wanahitaji miaka 2. Ambapo hao 6000 hata idadi ya watu walio kwenye nyingine ni wengi zaidi ya hao 6000 wanachama act kwa mikoa kumi waliotembea kwa mbwembwe
 
CHADEMA at it's best. Kuamulia vyama vingine cha kufanya na kutokufanya. Naona dalili za stroke kwa mbali kwenye ubongo wa UKAWA.
 
Wawakubalie kujiunga na UKAWA kuanzia January 2016. Kama nia yao ilikuwa kuunganisah nguvu kwanini walianzisha chama kipya badala ya kujiunga na vyama vilivyopo. Ukiwaingiza kipindi hiki itakuwa sawa na kumkaribisha nyoka chumbani.
 
Hamad Alipofukuzwa Ccm Alikuwa Mkali Kama Pilipili, Alipofukuzwa Cuf Na Kuanzisha Adc Jana Ameomba Kugombea Urais Znz Kwa Upole Akitafuta Huruma Toka Ccm. Tukija Kwa Zzk Nae Kapunguza Makali Yake Sasa Najiuliza Kumbe Wakitoka Ktk Vyama Makini Huwa Wanaomba Huruma Kwa Ccm Ili Kuungwa Mkono
 
Back
Top Bottom