ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

ACT - Wazalendo waomba kujiunga na UKAWA

Zitto aunde Ukawa ya Zitto,Mrema,Cheyo,Hamadi Rashid,Dovutwa,Ccm ya akina Lowasa plus ya akina Membe nadhani itanoga zaidi
 
mbona takwimu zake zinapishana na bosi wake tulewelewe nani kati yao hawa watu usaliti ni zambi mbatii zambo
 
hivi Zitto anafikiri Watanzania ni wajinga kiasi hicho?anasahau kwamba wote tunajua kilichomfukuza ni usaliti?aanzishe ukawa yake na Mrema wa Tlp itanoga sana

hahaaa aanzishe ukawa yake?????????? nimecheka sana
 
Hawa ndiyo waliosema kwamba UKAWA ni Muungano wa wasaka tonge!

Kwanini basi wasiwaandikie barua ADC ya kuomba kujiunga nao na badala yake wanawaandikia wasaka tonge?!

Ukishaanza kula nyama ya mtu (read USALITI) hutaacha kamwe.
 
Binafsi ninapata mashaka na hawa jamaa ACT. Kwani walikuja na hoja kutoitambua UKAWA, na wakaenda mbali zaidi kwa kusema "KWA GHARAMA ZOZOTE WATAHAKIKISHA WANAYANYAKUA MAJIMBO YA KAWE, UBUNGO, UKONGA NA MAJIMBO YOTE YANAYOMILIKIWA NA CUF HUKO MAENEO YA KUSINI MWA TANZANIA"

Nashindwa kuwaelewa leo wakisema kuwa wanatamani kujibu barua yao.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Waache wasalitiane lkn cha msingi ni kumpigia kura Kiongozi mwny hadhi ya kua kiongozi.... na si chama...
 
Kweli kujenga Chama sio lelemama kama inavyochukuliwa na wengi, Zitto sasa hivi amekuwa Mwenyekiti na ndio alichokuwa anakitafuta toka akiwa chadema.

Ni muda muafaka kuonyesha kile alichoshindwa akiwa Chadema, Mbowe, Lipumba, Mbatia na Makaida tumeona uzoefu wao na misukosuko dhidi ya siasa za Tanzania.

Na yeye aonyeshe uwezo ambao alizuiwa , pamoja na mshauri wake Kitila. Sio anapenda kukwea lifti badala ya kupanda ngazi.

Act sio taasisi ni kikundi fulani cha watu, akijengee kwanza mizizi ndio aanze kuangalia nje.
 
ndio maana aya.to.lla.h anataka aongee peke yake ili wafuatiliaji wa mambo wasijue uhalisia wa hiki chama. Anachosahau ni kuwa you can fool some people so some time but you can't fool all.....!


You can't fool people All the time stand up for your lights by bob marley

swissme
 
Naomba kujua, hivi tofauti ya ACT-TANZANIA na ACT- WAZALENDO ni ipi?
 
Ninachokiona hapa ni ccm kutaka kupenyeza mamluki ndani ya UKAWA. kamwe msikubali kuingiza virus ndani ya UKAWA.
 
Chanzo: Habari247

MYTAKE:
1) yaani mbwembwe zote zile za zitto na wenzake kuzunguka nchi nzima wameambulia wanachama 700 tu??? hata kura za kata moja hawajafikisha?? huu sasa utani....ndio maana zzk amekata tamaa na ziara ya pili???

2) Kwani kiongozi Mkuu zitto sialisema Ukawa ni wasakatonge??? na yeye anataka kujiunga na wasakatonge ???

3) Huyu mama sialisema "Nimarufuku Mwana Act kushabikia Ukawa"???

.....................
Professor kilaza.

Mtoa Maada ,inayotaka kujiunga na ukawa ni ACT-Tanzania au ACT-Wazalendo? Sisi tunachojua ni kwamba ACT-Tanzania ni ya LIMBU na ACT-wazalendo ni ya Zitto kabwe na wenzake , weka ufafanuzi hapo.
 
Washabiki wa siasa mnatabu sana,kabla ya ukawa hivyo vyama vilishaitana ccm B,mashoga na wengine hadi walimsaidia Kikwete ashinde. Lakini leo hii wote kwa pamoja et ndiyo wameunda ukawa,hivyo hata si ajabu pia kuona ACT wamejiunga na ukawa.
 
ACT Wasaliti walifikiri kuwa huko field ni rahisi, kumbe kunahitaji support ya makamanda wa ukweli sio mchezo. Sasa huyo ZZK alipokuwa akihutubia, watu walikuwa wanamtolea macho tu bila yeye kujijua. Ni aibu wakuu.
 
Chanzo: Habari247

MYTAKE:
1) yaani mbwembwe zote zile za zitto na wenzake kuzunguka nchi nzima wameambulia wanachama 700 tu??? hata kura za kata moja hawajafikisha?? huu sasa utani....ndio maana zzk amekata tamaa na ziara ya pili???


Professor kilaza.


Kama ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania hoja yako inakosa mashiko, kwa kuwa siasa za Tanzania zimekaa kishabiki sio kwa kufuata idadi ya wanachama, mara zote kipimo ambacho kimekuwa kikitumika ni kuangalia muitikio wa watu katika mikutano ya hadhara ya chama husika, kwa mantiki hii hauwezi kukipima chama kwa uangalia idadi ya wanachama labda kama hoja hii itakuwa katika kuzungumzia jambo lingine.


Hizi ndizo sera halisi za Tanzania yetu iko mifano mingi katika kuthihirisha hilo, binafsi nimekuwa shabiki wa chadema toka mwaka 2000 lakini nimejiunga rasimi kwa kumiliki kadi ya chama na kuwa mwanachama mwaka 2014, na hiyo siyo kwangu tu kuna kundi kubwa la watu kama nilivyokuwa kabla;


Na hata maeneo mengi upinzani unapo shinda siyo kama wana wanachama wengi hapana, wana washabiki wengi na ushabiki huwa una kawaida ya kuhama hama ni kama upepo haukai sehemu moja.
 
Wakishajiunga UKAWA halafu waanze upya kugawanq majimbo au hapa inakuwaje tena?
 
Huyu mama hajielewi si ndio huyu aliyesema kuwa namnukuuu " NI MARUFUKU KWA MWANA-ACT YEYOTE KUSHABIKIA UKAWA"

Kweli usaliti ni sawa na mchawi

Hivi hawa ACT-Wazalendo ni chama kipya kinataka kuanzishwa au?? Maana nina mtu pale kwa msajiri wa Vyama vya Siasa anadai bado Tanzania hakuna chama kiitwacho ACT-Wazalendo ila kuna chama flani kinaitwa ACT-Tanzania, wanachoshangaa hawakioni kikiendelea na shughuli za kisiasa. :A S-coffee:
 
Kitila na Mwl Kajage ambao ni viongozi wa ACT kila siku ni wa kukejeli viongozi wa Chadema na chama chenyewe ambacho ni sehemu ya Ukawa, sasa jee hauta kuwa upuuzi kuungana na mtu anaye kukejeli kila kukicha?

Hawa wanatakiwa wakataliwe,wakikubaliwa watagawa ukawa nakujiita ukawa wazalendo
 
Back
Top Bottom