Viongozi wa chama cha ACT Wazalendo wanaendelea na ziara zao katika Mikoa ya Kusini ambapo jana Januari 7, 2026 Kiongozi wa Chama, Dorothy Semu, aliwasili katika Jimbo la Mtwara Mjini na kufanya kikao na uongozi wa jimbo hilo pamoja na waliokuwa wagombea wa udiwani katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 2025. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Mangowela Inn uliopo Kata ya Chuno, Mtaa wa Ligula A.
Baadhi walitoa maoni wakiwasihi Viongozi wa Chama kuhakikishs wanapigania Katiba mpya kabla ya chaguzi zijazo.
Akiwahutubia viongozi hao, Semu alisema kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi mkuu, akibainisha kuwa baadhi ya watu waliuawa na wengine kufanyiwa vitendo vya kikatili. Amesema hali hiyo imeacha alama mbaya katika historia ya uchaguzi nchini.
Alieleza pia kuwa ACT Wazalendo ilipitia mitihani mizito wakati wa uchaguzi ikiwemo kuenguliwa mgombea wao wa urais, Luhaga Mpina, kuondolewa kwa mawakala wa chama vituoni, na wagombea wa ubunge na udiwani kuenguliwa bila kufuata sheria. Semu amesema hata madiwani wa chama hicho walinyimwa haki ya msingi ya kula kiapo cha kuwa wakala.
Katika hotuba yake, amesisitiza kwa kusoma nukuu ifuatayo kama ilivyo:
"Ni wazi kabisa uchaguzi haukuwa huru, haki na kuaminika. Haki ya mwananchi iliporwa kuchagua viongozi wanaowataka
Ni fedheha kuona Samia Suluhu anashinda Kwa asilimia 98% hata wakati wa chama kimoja enzi za mwalimu haijawahi kutokea." amesema Semu
Semu alisema ACT Wazalendo itaendelea na hatua zake za kimapambano bila kukata tamaa, akieleza kuwa tume mbalimbali za uchunguzi na maridhiano zinazoundwa ni za “kiini macho.”
Alifafanua kuwa chama hicho tayari kimeonyesha njia ya namna ya kutoka katika mtanzuko wa kisiasa uliopo.
Baadhi walitoa maoni wakiwasihi Viongozi wa Chama kuhakikishs wanapigania Katiba mpya kabla ya chaguzi zijazo.
Akiwahutubia viongozi hao, Semu alisema kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi mkuu, akibainisha kuwa baadhi ya watu waliuawa na wengine kufanyiwa vitendo vya kikatili. Amesema hali hiyo imeacha alama mbaya katika historia ya uchaguzi nchini.
Alieleza pia kuwa ACT Wazalendo ilipitia mitihani mizito wakati wa uchaguzi ikiwemo kuenguliwa mgombea wao wa urais, Luhaga Mpina, kuondolewa kwa mawakala wa chama vituoni, na wagombea wa ubunge na udiwani kuenguliwa bila kufuata sheria. Semu amesema hata madiwani wa chama hicho walinyimwa haki ya msingi ya kula kiapo cha kuwa wakala.
Katika hotuba yake, amesisitiza kwa kusoma nukuu ifuatayo kama ilivyo:
"Ni wazi kabisa uchaguzi haukuwa huru, haki na kuaminika. Haki ya mwananchi iliporwa kuchagua viongozi wanaowataka
Ni fedheha kuona Samia Suluhu anashinda Kwa asilimia 98% hata wakati wa chama kimoja enzi za mwalimu haijawahi kutokea." amesema Semu
Semu alisema ACT Wazalendo itaendelea na hatua zake za kimapambano bila kukata tamaa, akieleza kuwa tume mbalimbali za uchunguzi na maridhiano zinazoundwa ni za “kiini macho.”
Alifafanua kuwa chama hicho tayari kimeonyesha njia ya namna ya kutoka katika mtanzuko wa kisiasa uliopo.
