Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,503
- 51,099
Chama cha ACT Wazalendo kilijijengea jina kwa kusimama juu ya masuala muhimu na makubwa. Kilitoa chambuzi nyingi juu ya uchumi, hali ya kisiasa na mambo ya uongozi
Hata hivyo chama hicho kimegeuka bubu kwenye suala la Bandari. Chama kimeshindwa kutoa msiamamo wa chama katika suala hilo nyeti. Tunachosikia ni kauli binafsi za kiongozi mmoja mmoja na baadhi ya kauli hizo ziko "out of touch" na msimamo wa Wananchi katika suala hili.
1. Zitto asema mkataba huu wa IGA ni kama karatasi la kufungia vitumbua
Wakati, Wasomi wazito kwenye nchi hii wakionyesha matatizo makubwa ya mkataba huu, Wasomi wa sheria wa TLS, Profesa Shivji, Dr Nshala na wasomi wengine wa sheria , Kioingozi wa ACT Wazalendo ndugu Zitto yeye haoni kuwa huo mkataba ni hatari kwa mustakbali wa nchi yetu, Yeye anasema huo mkataba ni sawa na karatasi la kufungia vitumbua tu. Kauli hii imewashangaza wengi waliokuwa wakimuona Zitto ni mtu serious
2. Ukimya huu wa ACT unaonyesha dhahiri kuwa ACT ni chama cha kutetea maslahi ya Wazanzibari zaidi kuliko Watanganyika
Ukiwasikiliza viongozi wa ACT Wazalendo kuanzia kwa Zitto, Akina Mzee Duni, Jussa, Abdu Nondo, huwa ni wepesi sana kuonyesha madhila ambayo Zanzibar inapata katika muungano, lakini huwa hawajisumbui kuzungumza madhila ambayo Tanganyika inapata katika huu muungano.
Angalau Wazanzibari wa ACT ningewalewa, lakini Viongozi hawa wa kutoka Tanganyika ndani ya ACT wamegeuka kuwa bootlickers wa camp ya Wazanzibari ndani ya chama. Hawana Interest na mustakbali wa Tanganyika, wao wamegeuka kasuku wa kuimba madhila ya Wazanzibari ndani ya chama.
Pengine kwa sababu Ruzuku ya Chama inatoka Zanzibar ndiyo maana inabidi wamtumikie "Kafiri" wapate mradi wao. Lakini hii maana yake ni kwamba wanaonekana mbele ya umma kuwa hawa siyo wanasiasa wa kitaifa kama wanavyojaribu kujiportray bali ni special interest group.
3. Ukimya wa ACT unalenga kumnusuru Samia
Tunaambiwa Zitto yuko karibu sana na Samia, Tunaambiwa Juma Duni ni rafiki wa Samia. Urafiki na Ukaribu wa watu hao kwa raisi umekiteka nyara chama hicho kuacha kukosoa makosa makubwa kabisa anayofanya Samia kwa mustakbali wa nchi.
Matokeo yake hawa wamekigeuza chama kama Mercinery wa kisiasa. Yaani kukitumia chama kama conduit ya kumsaidia Samia kutawala smoothly licha ya makosa makubwa ya kiuonglzi hata ya kisiasa ambayo Samia anafanya. Hali hii imekigharimu sana chama cha ACT Wazalendo kuaminika na kuonekana kuwa ni chama serious chenye nia ya kuiondoa CCM madarakani.
4. CHADEMA wanakisulubu sana chama cha ACT mbele ya wananchi kwa hoja ya bandari
Kwenye ziara ambazo Chadema wanafanya nchi nzima, bila ya kutaja jina la chama chochote, wamekuwa wakiwaambia wananchi kuwa hakuna chama kilichobeba ajenda ya kutetea bandari zetu isipokuwa Chadema.
Message hii imekuwa ikiresonate ipasavyo kwa wananchi kiasi cha kujenga imani kubwa kwa chama hicho kwa kuamini kuwa ni chama kinachobeba ajenda kubwa. ACT itakuwa ni vigumu sana kupenetrate kwa wananchi kwa kupuuza ajenda nzito kama hii kisa tu ya urafiki wa Zitto na Duni Haji kwa Samia.
5. Watanganyika waanza kuamini kuwa ACT ni chama cha Wazanzibari
Kitendo cha Juma Duni kutoa kauli za kumtetea Samia kuhusuiana na udalali huu wa bandari zetu, na Kitendo cha Jussa kusema kuwa ishu ya bandari ni ya Watanganyika na watajijua wenyewe.
Huku viongozi watanganyika ndani ya chama hicho kudogosha ubovu wa mkataba huu. Kinawafanya Watanganyika waone kuwa hicho chama si chao, bali ni chama cha Wazanzibari, kwa ajili ya Wazanzibari na kwamba hawa viongozi wa Tanganyika ni front face to ya kumask Lengo halisi la chama hicho.
Mwisho:
Hiki chama cha ACT kilianza vizuri, lakini sasa kinapoteza muelekeo. Kimeshindwa kuwa fair kwenye kutetea pande zote mbili za muungano, bali kimeegemea kuisemea Zanzibar zaidi, wakati na Watanganyika kuna mambo wanayanung'unikia.
Pili uswahiba binafsi wa viongozi wake kwa watawala, umetia ukungu utendaji wa chama hicho kupigia kelele makosa makubwa ya kiuongozi yanayofanywa na watawala nchini.
Kwa muktadha huu nakiona hiki Chama kikiendelea kuwa Chombo cha Uchaguzi zaidi hasa huko Zanzibar badala ya kuwa chombo cha kuwa serikali mbadala nchini chenye kusimamia mambo makubwa kama ambavyo wakti kinaanzishwa kiliahidi au kiujipambanua kufanya.
Hata hivyo chama hicho kimegeuka bubu kwenye suala la Bandari. Chama kimeshindwa kutoa msiamamo wa chama katika suala hilo nyeti. Tunachosikia ni kauli binafsi za kiongozi mmoja mmoja na baadhi ya kauli hizo ziko "out of touch" na msimamo wa Wananchi katika suala hili.
1. Zitto asema mkataba huu wa IGA ni kama karatasi la kufungia vitumbua
Wakati, Wasomi wazito kwenye nchi hii wakionyesha matatizo makubwa ya mkataba huu, Wasomi wa sheria wa TLS, Profesa Shivji, Dr Nshala na wasomi wengine wa sheria , Kioingozi wa ACT Wazalendo ndugu Zitto yeye haoni kuwa huo mkataba ni hatari kwa mustakbali wa nchi yetu, Yeye anasema huo mkataba ni sawa na karatasi la kufungia vitumbua tu. Kauli hii imewashangaza wengi waliokuwa wakimuona Zitto ni mtu serious
2. Ukimya huu wa ACT unaonyesha dhahiri kuwa ACT ni chama cha kutetea maslahi ya Wazanzibari zaidi kuliko Watanganyika
Ukiwasikiliza viongozi wa ACT Wazalendo kuanzia kwa Zitto, Akina Mzee Duni, Jussa, Abdu Nondo, huwa ni wepesi sana kuonyesha madhila ambayo Zanzibar inapata katika muungano, lakini huwa hawajisumbui kuzungumza madhila ambayo Tanganyika inapata katika huu muungano.
Angalau Wazanzibari wa ACT ningewalewa, lakini Viongozi hawa wa kutoka Tanganyika ndani ya ACT wamegeuka kuwa bootlickers wa camp ya Wazanzibari ndani ya chama. Hawana Interest na mustakbali wa Tanganyika, wao wamegeuka kasuku wa kuimba madhila ya Wazanzibari ndani ya chama.
Pengine kwa sababu Ruzuku ya Chama inatoka Zanzibar ndiyo maana inabidi wamtumikie "Kafiri" wapate mradi wao. Lakini hii maana yake ni kwamba wanaonekana mbele ya umma kuwa hawa siyo wanasiasa wa kitaifa kama wanavyojaribu kujiportray bali ni special interest group.
3. Ukimya wa ACT unalenga kumnusuru Samia
Tunaambiwa Zitto yuko karibu sana na Samia, Tunaambiwa Juma Duni ni rafiki wa Samia. Urafiki na Ukaribu wa watu hao kwa raisi umekiteka nyara chama hicho kuacha kukosoa makosa makubwa kabisa anayofanya Samia kwa mustakbali wa nchi.
Matokeo yake hawa wamekigeuza chama kama Mercinery wa kisiasa. Yaani kukitumia chama kama conduit ya kumsaidia Samia kutawala smoothly licha ya makosa makubwa ya kiuonglzi hata ya kisiasa ambayo Samia anafanya. Hali hii imekigharimu sana chama cha ACT Wazalendo kuaminika na kuonekana kuwa ni chama serious chenye nia ya kuiondoa CCM madarakani.
4. CHADEMA wanakisulubu sana chama cha ACT mbele ya wananchi kwa hoja ya bandari
Kwenye ziara ambazo Chadema wanafanya nchi nzima, bila ya kutaja jina la chama chochote, wamekuwa wakiwaambia wananchi kuwa hakuna chama kilichobeba ajenda ya kutetea bandari zetu isipokuwa Chadema.
Message hii imekuwa ikiresonate ipasavyo kwa wananchi kiasi cha kujenga imani kubwa kwa chama hicho kwa kuamini kuwa ni chama kinachobeba ajenda kubwa. ACT itakuwa ni vigumu sana kupenetrate kwa wananchi kwa kupuuza ajenda nzito kama hii kisa tu ya urafiki wa Zitto na Duni Haji kwa Samia.
5. Watanganyika waanza kuamini kuwa ACT ni chama cha Wazanzibari
Kitendo cha Juma Duni kutoa kauli za kumtetea Samia kuhusuiana na udalali huu wa bandari zetu, na Kitendo cha Jussa kusema kuwa ishu ya bandari ni ya Watanganyika na watajijua wenyewe.
Huku viongozi watanganyika ndani ya chama hicho kudogosha ubovu wa mkataba huu. Kinawafanya Watanganyika waone kuwa hicho chama si chao, bali ni chama cha Wazanzibari, kwa ajili ya Wazanzibari na kwamba hawa viongozi wa Tanganyika ni front face to ya kumask Lengo halisi la chama hicho.
Mwisho:
Hiki chama cha ACT kilianza vizuri, lakini sasa kinapoteza muelekeo. Kimeshindwa kuwa fair kwenye kutetea pande zote mbili za muungano, bali kimeegemea kuisemea Zanzibar zaidi, wakati na Watanganyika kuna mambo wanayanung'unikia.
Pili uswahiba binafsi wa viongozi wake kwa watawala, umetia ukungu utendaji wa chama hicho kupigia kelele makosa makubwa ya kiuongozi yanayofanywa na watawala nchini.
Kwa muktadha huu nakiona hiki Chama kikiendelea kuwa Chombo cha Uchaguzi zaidi hasa huko Zanzibar badala ya kuwa chombo cha kuwa serikali mbadala nchini chenye kusimamia mambo makubwa kama ambavyo wakti kinaanzishwa kiliahidi au kiujipambanua kufanya.