Abiria unachelewaje Ndege (check-in) Airport?

Abiria unachelewaje Ndege (check-in) Airport?

Kqa uzoefu wangu wa kusafiri mara kwa mara na kuchelewa ndege na kadhalika, natamatisha kusema ni UZEMBE TUUUUUUUU. Zungukaaa koteee lakini jibu ni uzembe full stop, nukta bila koma wala mkato kama hutaki kunya tikiti la elfu kumi.
 
Ni uzembe tu kwa mtu kuchelewa airport kwa kutoa kisingizio kama foleni kwa nn usiwahi kutoka kwako ili uwah?
Sio uzembe nakukatalia inategemea na safari yenyewe, hebu fikiria tukio la Hamza ungewza kuchomòka kwenye daladala ili uwahi, hebu fikiria unàtaarifiwa usiku kuwa mazishi ni kesho saa 10 na unajua ukipata ndege ya asubuhi lazma uwahi lkn wakati huo lazma kuna kununua hiki na kile au kuacha mambo sawa hapo ofcn lkn aliyelala na funguo kachelewa. Ni katka hali hiyo waweza kuchelewa.
 
Sio uzembe nakukatalia inategemea na safari yenyewe, hebu fikiria tukio la Hamza ungewza kuchomòka kwenye daladala ili uwahi, hebu fikiria unàtaarifiwa usiku kuwa mazishi ni kesho saa 10 na unajua ukipata ndege ya asubuhi lazma uwahi lkn wakati huo lazma kuna kununua hiki na kile au kuacha mambo sawa hapo ofcn lkn aliyelala na funguo kachelewa. Ni katka hali hiyo waweza kuchelewa.
Umekunywa DOMPO?
 
Foleni, kusahau passport so you have to rush back home. Ni jambo la kawaida especially kama unasafiri mara kwa mara. Kutoka ofisini mbio kuelekea airport
Kwa mwanaume alikamilika kamwe hawezi sahau vitu muhimu kama passport,laptop,iPad nk
Wavulana wa miaka 20+ ndio zao kusahau sahau mara kasahau chaja mara simu.
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana, siku ya kwanza kuachwa nililia balaa, nilipiga mayowe utadhani nimefiwa na wazazi, ilibidi wale customer care staff swissport watumie muda mwingi kunituliza, ilikuwa the first time naenda nje ya Africa, dah, kitu emirates kikasepa kikaniacha.

Nilikuwa naona soo hata kurudi home, japokuwa nilisafiri the next day. Aisee, kumi na mbili kamili alfajiri nilikuwa tayari airport kwa safari ya saa kumi unusu jioni.

Dah nikikumbuka huwa nacheka mwenyewe, yaani airport ilisimama kwa mshangao wa kilio changu but kidume mpaka leo hii nimeshapata masomo ya kutosha kuhusu usafiri wa anga.
Mimi kwa kweli linapokuja suala la safari huwa nalala naiota kabisaa hata iwe ya basi. Sijawahi kuchelewa ktk safari yoyote ile.

Uchelewaji ni moja kati vitu vinavyosasabisha ajali.
 
Ndege kwa nchi zetu za dunia ya tatu si bahati tu bali ni jambo la Sifa na kukuza nafasi (status) yako kwenye jamii husika, wengine hutumia katika mitongozo.
...hahahaa, Mkuu! Hata kwenye mitongozo! [emoji16][emoji16]...Ikoje hii...!!![emoji16][emoji16]
 
Sasa Kama Ndiyo Kwanza Nimetoka Kijijini Kwetu KYAKA NKUNDE Jana Tu Na Leo Nasafirishwa Kwenda India Kutibiwa Moyo Unadhani Sitochelewa Kweli? Kusafiri Na Mbung'o ( Ndege ) Ni Habari Nyingine Mkuu Haswa Ukiwa MLUGALUGA Lazima Tu Utaachwa au Kuchelewa Unless Kuna Mtu Anakupeleka!
Aisee.. Ikiwa ndiyo Mara ya kwanza unaenda panda ndege uwezi achwa.
Wanao achwa na ndege ni wale wanaosafiri Mara kwa Mara.. Ikiwa ni Mara ya kwanza vibe na presha ya kupanda ndege utakufanya ukalale airport
 
Kwa msafiri anayepanda ndege mara ya kwanza, au anayeenda nje ya nchi mara ya kwanza, kuchelewa hakupo hata check-in ikiwa saa 8 usiku
Kwa msafiri anayesafiri mara moja moja naye kuchelewa ni nadra sana.
Makundi haya niliyoyataja juu wakichelewa inakuwa sio uzembe, kuna sababu tena kubwa.
Sasa kuna hawa "frikwenti flayaz", hawa wanaopanda ndege mara kwa mara mpaka wanajisifu wamezizoea. Mara nyingi hawa kuchelewa ni uzembe tu na dharau kisa wana uzoefu na ndege blah blah blah.
 
Kuna rafiki yangu aliwahi kukoswakoswa kuchelewa ndege tena siyo kwa masaa tu machache bali karibu siku nzima, siwezi kusema ni uzembe au ujinga, badala yake naweza kusema ilikuwa ni kwa sababu ya utofauti wa masaa kwa kizungu na kikwetu(Kiswahili).

Ilikuwa hivi; yeye ticket ya ilikuwa imeandikwa safari ni ijumaa saa 7 usiku yaani (departure Friday 1am) Maana yake ilitakiwa aende Airport siku ya Alhamisi walau saa4 usiku ili saa tano usiku aanze ku check in.

Yule jamaa ilifika around saa4:30 usiku akapigiwa simu na rafiki yake, “oya kamanda umeshafika Airport?” Jamaa, “mwanangu nilikwambia safari ni kesho saa7 usiku”. Mabishano yakaanza lakini jamaa akaona arudie tena kusoma ticket na kucheki mtandaoni kwenye booking status. Heeeeeh jamaa anaona check in imeshafunguliwa, kidogo achanganyikiwe. Thank God at the end alifanikiwa kufika airport kwa mda na aka check in vema na akasafiri.

Guess what? Ilikuwa tr 24 September 2015 kwa mara ya kwanza jamaa anaenda Switzerland kwa ajili ya masomo.
 
Back
Top Bottom